Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Status
Not open for further replies.
Kama kutakuwa na objectivity katika kulijadili suala hili basi huenda lawama dhidi ya Chadema zingeweza kuwa tofauti.Chama hiki kinakabiliwa na dilemma ya demokrasia,na sio kosa lao.Nitoe mfano japo sio wa kisiasa.Hivi timu inapopanda daraja na kufanikiwa kucehza ligi kuu,je ikitaka kutwaa ubingwa (na sio kushiriki tu kwenye ligi hiyo) haitopaswa kuunda timu ya ushindi?Of course,itakuwa sio haki kuwatosa wachezaji walioipandisha timu daraja lakini what if viwango vya wachezaji hao haviwezi kustahimili mikikimikiki ya ligi kuu?Na what if kama kuna wachezaji mahiri wenye potential ya kuleta kombe kwenye timu hiyo wapo willing kujiunga nao?

Tukija kwa Chadema,tunafahamu kuwa kura zao za maoni licha ya kujumuisha wanachama wachache (kutokana na idadi ndogo ya active members) pia sio sample mwafaka sana ya potential voters kwenye uchaguzi mkuu.Hilo sio kosa hasa ikizingatiwa kuwa hata CCM imekuwa ikipata kura nyingi zaidi ya idadi ya wanachama wake milioni 5 or so.Tutambue kuwa siasa za Tanzania,na sehemu nyingi Afrika bado zinaelemea zaidi kwa mgombea kuliko chama.Huo ni mfumo ambao utachukua miaka mingi kubadilika.

Ni kwa kutambua hivyo basi Chadema wanalazimika kufanya maamuzi magumu ya kupata wagombea wenye potential ya kutoa upinzani kwa CCM na pengine kukiwezesha chama hicho kupata idadi kubwa ya wabunge.Sasa je mnaoitakia mema Chadema mngependa "waridhishe demokrasia kwa kupitisha wagombea wenye uwezo haba wa kushinda" au waje na wagombea wanaoweza kuipatia ushindi?Tukumbuke huu ni mwaka wa uchaguzi na la muhimu zaidi ni ushindi HALALI.Mnaolinganisha udikteta wa CCM na "huu wa Chadema" mnasahau kuwa wakati "udikteta huu wa Chadema" unalenga kupata wagombea wenye potential ya ushindi (na process hii haisukumwi na rushwa au ufisadi) CCM hufanya mchezo huo kwa vile tu flani ana fedha za kutosha,anaweza kuhonga wapiga kura wengi na pengine anakidai chama hicho fadhila flani.

Pengine ni muhimu kwetu kutafakari kwa mapana zaidi dhima ya demokrasia hasa kwenye mwaka wa uchaguzi a kujiuliza,kwa mfano je linapokuja suala la kuteua wagombea kipi kiwe muhimu zaidi: wagombea walioteuliwa kwa njia za demokrasia au nafasi ya wagombea hao kushinda kwenye uchaguzi husika alimradi uteuzi wao haufanywi kwa njia zisizo halali?Au,kipi kiwe kipaumbele kwa chama katika mwaka wa uchaguzi kati ya kuenzi demokrasia na nafasi ya chama kufanya vizuri alimradi processes hizo zinafanywa kihalali na transparent?

Nami pia naona kuna kasoro fulani katika kujadili hili suala. Watu tunataka kulazimisha democracy and nothing but absolute democracy. Ukiangalia suala hili positively, inaonekana kama Chadema wanatumia busara. Ukienda kwenye extreme nyingine, inaonekana chama kinatumia ubabe. Hapo naona kizungumkuti tu.

Binafsi naamini Chadema hakina nia mbaya, ila kuweka wagombea watakaoshinda kwenye hayo majimbo. Kama wengine walivyosema, vyama vya upinzani havina nguvu sehemu nyingi. Hivi fikiria, kura za maoni ziendeshwe DP, chama cha Mtikila katika jimbo fulani huko Dodoma. Halafu ghafla bin vuu mzee Malecela anahamia hicho chama, na anakuwa kati ya wagombea wa kupigiwa kura za maoni. Anaangushwa katika kura hizo. DP itafanya vema kufuata demokrasia kwa kumwacha mzee Malecela pembeni? Thubutu!

With young democracy in a fragile political party, prudence and wisdom is of paramount importance in the party. That is strategic!
 
Hapana hakukosea Heading; heading ni yangu. Kuna maneno ambayo si yangu: Makala ya awali niliyotuma kwa mhariri ni hii hapa:

Wana CCM kwenye kura za maoni watafanya makosa makubwa endapo wataamua kuondoa wachezeaji uwanjani..............
Wana CCM wafanyie taifa hisani kwa kurudisha kundi hili zima Bungeni ili wakamalizie mechi waliyoianzisha.
Makala iliyochapishwa hii hapa...
Wana CCM kwenye kura za maoni wamefanya makosa makubwa kuamua kuwaondoa wachezeaji uwanjani.................
NEC ifanyie taifa hisani kwa kurudisha kundi hili zima bungeni ili wakamalizie mechi waliyoianzisha.

Nimeona, kama kweli hiyo ndiyo ilikuwa original ya Makala yako basi mhariri kafanya makosa, kwa mfano wewe uliandika wanaCCM watafanya makosa mhariri kaandika wamefanya makosa hilo ndilo lilikuwa tatizo langu. Vile vile wewe uliandika wanaCCM waifanyie hisani taifa mhariri kaandika NEC ifanye hisani kitu ambacho ni tofauti kabisa.

Ukweli mhariri kapotosha habari nzima ingawa alijitahidi kutobadili body yake lakini ukipotosha conclusion basi wasomaji wataenda na ulicho hitimisha. Sielewi ulichukua hatua gani ili isitokee tena mbeleni lakini hilo si kusudio langu. Shukrani kwa kunielewesha.
 
Invicible
Umesema vema kabisa.
Kwanza, tunawaonea CHADEMA kwa kudai tupate details zote za vikao hapa jamvini. Hakuna chama kitafanya hivyo.
Pili, demokrasia si mwarobaini wa matatizo ya kisiasa hapa Tanzania. Kupitia demokrasia, tumepata mafisadi as well as wapiganaji. Tatu, kura za maoni zimegubikwa na rushwa na wapiga kura za maoni ni sehemu ndogo sana ya wapiga kura za jumla. Tuwape nafasi Chadema waonyeshe ukomavu wao katika mazingira yaliyojaa mabomu ya ardhini.
 
Mlalahoi

Nimeupenda mfano wako wa timu iliyopanda daraja, ni kweli ni vizuri kuwa keep wachezaji ikiwezekana wote walioipandisha timu daraja lakini ukweli ni kwamba mikiki mikiki ya daraja la kwanza say ni tofauti na ya daraja la chini yake ndiyo maana hata timu kubwa kama ManU kila baada ya kipindi fulani hubadilisha au kununua wachezaji wapya.

Tukirudi kwa Chadema, kama The Invincible alivyosema Chadema bado ni chama kichanga kinahitaji kupata strong fighters kwa mbinu yeyote hata ku lobby kutoka chama kingine. Kama inawezekana ku lobby toka chama kingine je hatuoni ni rahisi sana kitendo hicho kufanyika ndani ya chama chenyewe kwa kujipanga wenyewe kwa wenyewe wewe nenda kule mimi niwe hapa kama inavyofanyika sasa, hatujui kina Regia na Rachel watapangiwa nini maana nasikia Rachel kagombea viti maalum pia.

Regia na Rachel ambao ndio wamekuwa icon yetu naelewa hata wao wanaelewa uzito wa kazi iliyo mbele yao sawa siwezi kuwa under estimate lakini kampeni inahitaji mikiki mikiki si support ya wanachama tu vile vile Head office iridhie. Hata kama umechaguliwa kwa kura za maoni 20 say wakati jimbo lina wapigakura 55,000 hadi laki moja mengine, ni bora kupanga na head office ambayo inaweza kuwa na macho ya kuona mbali zaidi ya kampeni uliyoifanya ya watu 20 tu.
 
Jamani mbona mkanganyiko ulishaanza na kukubalika siku nyingi!

Mfano ni pale ambapo matumizi ya kanuni moja isemayo "lete chanzo chako hapa" inasisitizwa kwa watu wengine wakati kwa mwingine hiyo kanuni inayeyuka kama barafu ipatapo joto endapo tu utasoma tungo isemayo "ka-inzi kangu kamenijulisha".


Wapo wanaoandika mengi humu huku wanajua machache na wapo wanaoandika machache huku wanajua mengi!
 
Invicible
Umesema vema kabisa.
Kwanza, tunawaonea CHADEMA kwa kudai tupate details zote za vikao hapa jamvini. Hakuna chama kitafanya hivyo.
Pili, demokrasia si mwarobaini wa matatizo ya kisiasa hapa Tanzania. Kupitia demokrasia, tumepata mafisadi as well as wapiganaji. Tatu, kura za maoni zimegubikwa na rushwa na wapiga kura za maoni ni sehemu ndogo sana ya wapiga kura za jumla. Tuwape nafasi Chadema waonyeshe ukomavu wao katika mazingira yaliyojaa mabomu ya ardhini.

Hapa hakutakuwa na maelewano kwani siasa za mtandaoni ni tofauti kabisa na hali halisi.
 
Mh! Maelezo ya Kina yanahitajika Otherwise CHADEMA will be equal to CCM
 
Mh! Maelezo ya Kina yanahitajika Otherwise CHADEMA will be equal to CCM

jamani nivizuri mambo kama haya ukayafuatilia kwa undani sana kwa sababu kuan sababu muhimu sana zinazoendelea chini ya carpet ila hili swala la hawa wakina dada nimelifuatilia na kulikuwa na sababu nzuri tu za kufanya hivyo siewezi kuziweka hapa kwa sababu ya kumwaga kuku wengi kwenye mtama kidogo!
 
Duh mkuu hii ya kumwaga kuku wengi kwenye mtama kidogo imeniacha haoi!
 
jamani nivizuri mambo kama haya ukayafuatilia kwa undani sana kwa sababu kuan sababu muhimu sana zinazoendelea chini ya carpet ila hili swala la hawa wakina dada nimelifuatilia na kulikuwa na sababu nzuri tu za kufanya hivyo siewezi kuziweka hapa kwa sababu ya kumwaga kuku wengi kwenye mtama kidogo!

Asante mkuu nimeelewa kwenye post ile ingine

Wewe jimbo harina kabisa network ya chama halafu anakuja mtu ambaye anayo network na ni muadirifu ambaye amechezewa faulo na nia yake nii kuwawakirisha watu wa jimbo lake eti akatariwe si ni kituko kutoa kauri blanketi kama hiyo?Halafu utaona huyu jamaa yuko well informed ni kweli wana ccm wengi wameomba kugombea kupitia chadema na viongozi wanahaha kuweza kuweka mambo sawa huyu anajaribu kuharibu.
 
jamani nivizuri mambo kama haya ukayafuatilia kwa undani sana kwa sababu kuan sababu muhimu sana zinazoendelea chini ya carpet ila hili swala la hawa wakina dada nimelifuatilia na kulikuwa na sababu nzuri tu za kufanya hivyo siewezi kuziweka hapa kwa sababu ya kumwaga kuku wengi kwenye mtama kidogo!

We dare speak openly hapa, otherwise hata mafisadi wenye sababu zao za kifisadi wanaweza kutumia kichaka hiki cha "kumwaga mchele kwenye kuku wengi" kujificha. What is the point of joining a forum if you can't share information ?

Now you do not want to be identified with them, do you ?

Kama kitu kina umuhimu wa kufichwa hivyo, then usituambie chochote, ukisema tu na kuleta habari za "kumwaga mchele kwenye kuku wengi" unaonekana huna interest za wengi, una interest za watu fulani ambao wanataka kukalia information kwa sababu zao.

Rev. Masanilo naona huyo mjomba mjomba wako herufi ya "l" inagomba kichizi.
 
Nami pia naona kuna kasoro fulani katika kujadili hili suala. Watu tunataka kulazimisha democracy and nothing but absolute democracy. Ukiangalia suala hili positively, inaonekana kama Chadema wanatumia busara. Ukienda kwenye extreme nyingine, inaonekana chama kinatumia ubabe. Hapo naona kizungumkuti tu.

Binafsi naamini Chadema hakina nia mbaya, ila kuweka wagombea watakaoshinda kwenye hayo majimbo. Kama wengine walivyosema, vyama vya upinzani havina nguvu sehemu nyingi. Hivi fikiria, kura za maoni ziendeshwe DP, chama cha Mtikila katika jimbo fulani huko Dodoma. Halafu ghafla bin vuu mzee Malecela anahamia hicho chama, na anakuwa kati ya wagombea wa kupigiwa kura za maoni. Anaangushwa katika kura hizo. DP itafanya vema kufuata demokrasia kwa kumwacha mzee Malecela pembeni? Thubutu!

With young democracy in a fragile political party, prudence and wisdom is of paramount importance in the party. That is strategic!

CHADEMA wanataka kushinda, sawa, sikatai, kushinda ni muhimu na hakuna chama chochote cha upinzani kinachoweza kufanya mabadiliko bila kushinda viti vingi.

Tatizo linakuja, mnataka kushinda kwa gharama gani ? Mnataka kuweka nini rehani ili kuhakikisha ushindi ? Mko tayari kuweka rehani core principles za chama na integrity ya chama ili kusudi mshinde? Mko tayari kumkubali mtu yeyote ambaye ana chance ya kushinda bila kujali kama kweli huyu mtu anaamini katika principles za chama ? Vipi kesho mtu huyu akijiona ameshinda yeye kama mtu binafsi na wala si kama muwakilishi wa CHADEMA ? Vipi akianza kubishana na manifesto ya chama baada ya kushinda ubunge kwa kudai kwamba hakujulishwa vilivyo in the first place? Vipi akianza kuleta factions katika chama ? Vipi kama akianza kutumiwa na CCM tena kuleta mfaraganyiko katika CHADEMA ? Vipi akiwa haamini katika sera ya majimbo ya CHADEMA na nyinyi mnampa ubunge tu? Vipi akiwa ana vote na CCM bungeni, atakuwa ana represent agenda ya CHADEMA au ni CHADEMA jina tu ?

Ndiyo maana nasema kuna haja ya kuwachuja na kuwapiga msasa hawa wagombea, sio kutumia policy ya "shoot first, ask questions next" = "win first, ask questions next". CHADEMA ikijionyesha kuwa iko desperate kushinda chaguzi hivi tutaona ni chama kisicho integrity, kinataka kushinda tu bila kuangalia gharama za ushindi, na kwa extension ya logic hiyo, kitajionyesha kwamba hakiwezi kuongoza, kwa sababu kinaweza kuweza rehani core principles za nchi yetui kikiwa deperate.
 
Tatizo la arm chair generals ni kutaka kuendesha battle kinadharia.Laiti Chadema wakiamua kupitisha kila aliyeshinda kura za maoni kisha wagombea hao wakawa too weak to pose any opposition to CCM then Chadema italaumiwa kwa ku-field weak candidates
Yani kweli chama ki-risk maelfu ya kura kwa vile tu flani kashinda kura 40 za maoni kati ya 45 ilhali kura zinazosakwa ili kushinda ubunge ni maelfu kama sio laki kadhaa?

Na tukiweka kando potential ya wagombea hao kushinda,je Chadema ifanyeje itakapobaini,kwa mfano, ushindi wa mgombea kwenye kura za maoni ulifadhaliwa na mafisadi wa CCM?Imwache mgombea huyo kwa vile tu ni kuridhisha demokrasia au wamstopishe sasa kabla hajasababisha maafa makubwa huko mbeleni?

Let's not forget sio kila anayeimba "chadema,chedema" au " Dkt Slaa,Dkt Slaa" hawezi kuwa na ajenda zake binafsi.Lakini kubwa zaidi ni uwezekano wa CCM kupenyeza rupia zake kwa baadhi ya potential candidates ili pengine washinde kura za maoni na kupitishwa kisha wajitoe!Je laiti Chadema wakishtukia mkakati wa aina hiyo waheshimu kura za maoni au wanusuru kura za jimbo?
 
Tatizo la arm chair generals ni kutaka kuendesha battle kinadharia.Laiti Chadema wakiamua kupitisha kila aliyeshinda kura za maoni kisha wagombea hao wakawa too weak to pose any opposition to CCM then Chadema italaumiwa kwa ku-field weak candidates
Yani kweli chama ki-risk maelfu ya kura kwa vile tu flani kashinda kura 40 za maoni kati ya 45 ilhali kura zinazosakwa ili kushinda ubunge ni maelfu kama sio laki kadhaa?

Na tukiweka kando potential ya wagombea hao kushinda,je Chadema ifanyeje itakapobaini,kwa mfano, ushindi wa mgombea kwenye kura za maoni ulifadhaliwa na mafisadi wa CCM?Imwache mgombea huyo kwa vile tu ni kuridhisha demokrasia au wamstopishe sasa kabla hajasababisha maafa makubwa huko mbeleni?

Let's not forget sio kila anayeimba "chadema,chedema" au " Dkt Slaa,Dkt Slaa" hawezi kuwa na ajenda zake binafsi.Lakini kubwa zaidi ni uwezekano wa CCM kupenyeza rupia zake kwa baadhi ya potential candidates ili pengine washinde kura za maoni na kupitishwa kisha wajitoe!Je laiti Chadema wakishtukia mkakati wa aina hiyo waheshimu kura za maoni au wanusuru kura za jimbo?
==============
Kama ulikuwapo ndugu yangu!

Huo mchezo umechezwa sana hata ndani ya CCM: yaani baadhi ya wagombea wa CCM walioshinda kura za maoni ni weak na waliwezeshwa na kadi feki zilizogawiwa kwa wapinzani. Tusubiri tuje tuone kitachowatokea mbele ya safari. Wale waliobainika wakaondolewa, ndiyo maana unaona watu wanachoma moto kadi.
 
Tatizo la arm chair generals ni kutaka kuendesha battle kinadharia.Laiti Chadema wakiamua kupitisha kila aliyeshinda kura za maoni kisha wagombea hao wakawa too weak to pose any opposition to CCM then Chadema italaumiwa kwa ku-field weak candidates
Yani kweli chama ki-risk maelfu ya kura kwa vile tu flani kashinda kura 40 za maoni kati ya 45 ilhali kura zinazosakwa ili kushinda ubunge ni maelfu kama sio laki kadhaa?

Na tukiweka kando potential ya wagombea hao kushinda,je Chadema ifanyeje itakapobaini,kwa mfano, ushindi wa mgombea kwenye kura za maoni ulifadhaliwa na mafisadi wa CCM?Imwache mgombea huyo kwa vile tu ni kuridhisha demokrasia au wamstopishe sasa kabla hajasababisha maafa makubwa huko mbeleni?

Let's not forget sio kila anayeimba "chadema,chedema" au " Dkt Slaa,Dkt Slaa" hawezi kuwa na ajenda zake binafsi.Lakini kubwa zaidi ni uwezekano wa CCM kupenyeza rupia zake kwa baadhi ya potential candidates ili pengine washinde kura za maoni na kupitishwa kisha wajitoe!Je laiti Chadema wakishtukia mkakati wa aina hiyo waheshimu kura za maoni au wanusuru kura za jimbo?

Mimi nishasema hapa kwama, kama kitu kinacho matter ni "popular support" tu, then hamna hata haja ya vyama. Vyama vya nini wakati tunaweza kuwashindanisha watu?

Umuhimu wa vyama ni sera, na inawezekana kabisa mtu akawa na popular support lakini katika chama kwa sababu moja au nyingine akawa hafai, sasa hapo chama kina wajibu wa kutetea principles zake na kusema huyu hatufai kwa sababu ingawa kashinda lakini hatufai (mathalani hata kushinda kwenyewe katumia rushwa) au kuogopa kwamba tusipomuweka mshindi wa primaries tutashindwa kura.

Hapo ndipo mtajua kama chama kinasimamia principles au kura.
 
demokrasi bila busara nayo ni hatari, tunajua chadema bado ni chama kichanga hakijafika kila sehemu, chukulia mfano jimbo fulani chama kipo kama hakipo ofisi iko nyumbani kwa mwenyekiti, siku ya primaries watu 12 tu wanajitokeza kuchagua mgombea mmoja kati ya watatu waliojitokeza, mgombea x anapata kura 6 mgombea y kura 4 wa tatu z kura 2, definitely mgombea x kapita.

Hapo demokrasia imetumika mgombea x ameteuliwa kugombea kwa kupata kura 6 na kuwazidi wapinzani wake wote. Tuseme jimbo zima lina wapigakura 25,000 na huyo mgombea x wa chadema aliyepata kura 6 anatarajiwa kupambana na mgombea wa ccm aliyemaliza muda wake ambaye ameteuliwa kulitetea jimbo lake.

Sasa jamani mkjj na wengine tujiulize na tujaribu kutumia busara akitokea mtu potential figure ameombwa na chama kugombea dakika za mwisho tutamkataa kwa kuhofia kuvunja demokrasia au zile kura 6 alizozipata x tutazipoteza? Hebu tuwe wakweli.

Mimi bado naendelea kusema na nitasema kwa sauti kubwa lengo la mkjj si kutetea demokrasia au jinsia ndani ya chadema lengo lake ni ku create co motions ndani ya chama na jamii, lakini bora naona watu wengi wamemshtukia mapema na nashukuru kitila amejitokeza mapema na kuliweka sawa jambo hili.

chadema wakimsikiliza huyu bwana wamekwisha maana ana mission yake na kama usemazwa luteni nadhani wameshamjua ila wana busara sana.

Ningekushauri usihangaike kumueleza maana anaelewa vizuri sana ila ana lengo lake kama ulivyosema ni sahihi sana na mwenye macho anaona na kusoma.
Tutakiona hiko ccj chama cha watu makini kilishoshindwa kusajiliwa kwa uzembe wa hali ya juu,ahaa viongozi wenyewe hawana kadi nikikumbuka siamini........
 
Tatizo la arm chair generals ni kutaka kuendesha battle kinadharia.Laiti Chadema wakiamua kupitisha kila aliyeshinda kura za maoni kisha wagombea hao wakawa too weak to pose any opposition to CCM then Chadema italaumiwa kwa ku-field weak candidates
Yani kweli chama ki-risk maelfu ya kura kwa vile tu flani kashinda kura 40 za maoni kati ya 45 ilhali kura zinazosakwa ili kushinda ubunge ni maelfu kama sio laki kadhaa?

Hoja yako hii ina nguvu endapo Chadema ingekuwa haijui idadi ya wanachama ilionao kwenye eneo fulani. kwa mfano ili kura ya maoni ifanyike inahitajika angalau wanachama wangapi? Katiba ya Chadema (ambayo nimeisoma vizuri sana) haisemi the minimum threshold ya wanachama wanaohitajika ili kufanyika kura ya maoni. Kama hili ni kweli, ina maana endapo wanachama wamefuata taratibu zote za kura za maoni na kutoka miongoni mwao wakamchagua mtu x dhidi ya y na z basi kura zao ziheshimiwe. Sasa isije kuja suala la idadi baadaye wakati chama kilikuwa kinajua mapema (kabla ya kura ya maoni) idadi ya wanachama waliopo mahali fulani.


Na tukiweka kando potential ya wagombea hao kushinda,je Chadema ifanyeje itakapobaini,kwa mfano, ushindi wa mgombea kwenye kura za maoni ulifadhaliwa na mafisadi wa CCM?Imwache mgombea huyo kwa vile tu ni kuridhisha demokrasia au wamstopishe sasa kabla hajasababisha maafa makubwa huko mbeleni?

Well, hili ni swali zuri lakini si swali makini. Ngoja nikumpe mfano wa utaratibu mzuri ambao haufanani na wa CCM.

a. Kila anayetaka kugombea Ubunge anawekewa masharti yafuatayo: Elimu japo ya Sekondari, mwanachama wa Chadema kwa muda usiopungua mwaka mmoja, hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote, hajawahi kutuhumiwa kwa makosa ya rushwa na awe na sifa za mpiga kura kama zilivyo kwenye Katiba ya Muungano.

b. Wanaotaka kugombea wanalipia fomu na kujiandikisha katika kila eneo la jimbo.

c. Jimbo linaweka utaratibu wa wagombea kujitangaza mbele ya wanachama. Matawi yanapanga tu taratibu za kuwaleta wagombea wote pamoja. Wagombea wanafanyiwa midahalo mbele ya wagombea juu ya masuala mbalimbali ya jimbo. Gharama ya kuandaa midahalo na mikutano inaingiwa na Jimbo.

d. Wagombea wanaruhusiwa kujipigia debe kwa wanachama kwa namna yoyote ile. Suala la rushwa linaachiwa vyombo vya sheria. Period.

e. Inapigwa kura ya maoni kwa utaratibu wa wazi kabisa na kura zinahesabiwa kila kituo na kutangazwa papo hapo. Matokeo ya jumla ya jimbo ndiyo yanampa mshindi kura. Mshindi ni yeyote anayepata simple majority.

f. Aliyeshinda ndiyo anakuwa mgombea.

Hakuna kikao kingine cha juu cha kutengua au kuhoji maamuzi hayo ya wananchi.

Hii itasababisha umakini katika kura za awali na wananchi wenyewe kujua wasitegemee kugombolewa mbele ya safari na wagombea watajua kabisa kuwa ukicheza vibaya ni pingu (siyo kamati ya maadili) na ukishindwa umeshinda hakuna kubebwa.


Let's not forget sio kila anayeimba "chadema,chedema" au " Dkt Slaa,Dkt Slaa" hawezi kuwa na ajenda zake binafsi.Lakini kubwa zaidi ni uwezekano wa CCM kupenyeza rupia zake kwa baadhi ya potential candidates ili pengine washinde kura za maoni na kupitishwa kisha wajitoe!Je laiti Chadema wakishtukia mkakati wa aina hiyo waheshimu kura za maoni au wanusuru kura za jimbo?

Jamani hii ndiyo demokrasia. Demokrasia ni pamoja kuacha makosa yatokee na wananchi wakosee, na wagombea wakosee. Demokrasia siyo lazima mtu tunayemtaka ashinde bali mchakato utoe uwezekano wa mtu tunayemtaka kushinda kushindwa. Demokrasia inayombeba fulani siyo demokrasia ni idumughasia.
 
(1) Rachel au Regia wamelalamika? Hapana. Wameelewa na kukubaliana na maamuzi ya chama chao. Tuwaunge mkono basi.

(2) Lengo ni kuleta mabadiliko Tanzania mwaka huu. Wananchi wamechoshwa sana na utawala wa miaka 49 wa TANU na CCM. Wengi hapa tunamkubali Slaa aongoze hayo mapambano. Mbona wengine mnatafuta namna ya kutugawa tena? Tuungane ili kushinda kwa sasa, na tukubali maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA.

(3) Watanzania wataunda Katiba Mpya ya Tanzania na hata ya CHADEMA, baada ya kuing'oa CCM.

(4) Wale wanaoutumia muda wao hapa kuikosoa CHADEMA kwa namna ya kutaka kuiongezea nguvu wanafanya vyema. Wale wanotaka kuidhoofisha wanapigania CCM ibaki madarakani.

(5) Nadhani CCM wanapata ahueni wanopoona namna akina MMKJ wanavyojitahidi kupooza nguvu ya CHADEMA.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom