Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Elections 2010 CHADEMA iwaachilie walioshinda kura za maoni wagombee

Status
Not open for further replies.
Sasa wajifunze kutumia common sense zao na si kusubiri hadi watu wa JF wawakemee. Wakija kuchukua madaraka ya nchi sitaki wawe wanasubiri kusikia akina NN wanasemaje huko JF.

Wawe tayari kufanya maamuzi mazito na magumu na si kusikilizia upepo unavuma wapi kwanza halafu ndio wanaamua.

Na kutofautiana na CCM ni kazi ndogo sana. Sijui wao walikuwa wanafikiria nini tu.
Napingana na mawazo yako kwa misingi ifuatayo, Kwa hili Chadema kimeonyesha usikivu kutoka kwa watu mbalimbali wakiwemo wanaJF na nashauri waendelee hivyo hivyo si kama unavyosema wawe kujiamulia mambo wenyewe. Wakifanya hivyo tutakuwa tunarudi kule kule kwa CCM kutokuwa wasikivu, maamuzi magumu ni pamoja na kuwasikiliza wananchi.
 
Exactly my objection.

Now nimeongea sana kuhusu weakness za Regia hapa, kwa hiyo kama namtetea simtetei kwa basis ya kwamba ni mgombea anayefaa na yuko strong.Lakini at least Regia wanamjua, ni mtu wa chama chao, kafanya kazi miaka mingi, ana loyalty kwa chama, na kama kuna matatizo ya exposure anaweza kufundishwa -I hope anafundishika-. Lakini hawa mamluki mapandikizi wa kuja kutokea siku moja kabla ya primaries wanaweza hata kuwa ma spy wa CCM hawa, vyama inabidi viwe makini nao sana, na kama kweli wanataka kufanya kazi za chama wapewe muda kujionyesha mpaka 2015.

CHADEMA kukubali mamluki hawa ni kukubali kwamba wako desperate, hawana principles na wanajali kushinda kwa njia yoyote bila kujali wana sacrifice nini katika ushindi wao.

Mwanachama wa CHADEMA ni mtanzania yeyote aliyeamua kuchukua kadi ya Chadema, akiwa ametokea kwenye kundi lolote ndani ya Tanzania. Ukiwa tayari mwanachama wa Chadema hubaguliwi kwa ugeni, rangi, kabila, mkoa, jinsia elimu, nk. Kwa haki za mwanachama hata ukichukua kadi leo ukaonekana unafaa kwenye nafasi mbalimnbali za chama utatumiwa. Ukiwa msaliti utakuwa unajisaliti mwenyewe.

Chama hakijengi msingi wa woga bali ya kujiamini na kuweza kumfanya kila mtu aamini Tanzania ni nchi yake anayo haki ya kuijenga kwa ajili yake na kizazi kijacho.

Karibuni wote chadema tujenge nchi yetu.
 
Mwanachama wa CHADEMA ni mtanzania yeyote aliyeamua kuchukua kadi ya Chadema, akiwa ametokea kwenye kundi lolote ndani ya Tanzania. Ukiwa tayari mwanachama wa Chadema hubaguliwi kwa ugeni, rangi, kabila, mkoa, jinsia elimu, nk. Kwa haki za mwanachama hata ukichukua kadi leo ukaonekana unafaa kwenye nafasi mbalimnbali za chama utatumiwa. Ukiwa msaliti utakuwa unajisaliti mwenyewe.

Chama hakijengi msingi wa woga bali ya kujiamini na kuweza kumfanya kila mtu aamini Tanzania ni nchi yake anayo haki ya kuijenga kwa ajili yake na kizazi kijacho.

Karibuni wote chadema tujenge nchi yetu.

Umesoma sura ya tano ya Katiba ya CHADEMA kuhusu uanachama na sifa zake ?


5.1.4 Awe anakubaliana na katiba, sera, kanuni na maadili ya Chama.
5.1.5 Awe anakubaliana na Itikadi na falsafa ya Chama.

Sasa wewe mtu kaja leo leo, hata kukaa naye chini kujua kama kajua sera, kanuni, maadili, itifaki na falsafa za chama bado, unataka kumpa kazi ya chama, wewe utasema una akili kweli ?

Hata huko kanisani wanakufundisha katekisimu kwanza na kukubatiza kabla ya kukupa kazi yoyote ya kanisa.
 
Umesoma sura ya tano ya Katiba ya CHADEMA kuhusu uanachama na sifa zake ?


5.1.4 Awe anakubaliana na katiba, sera, kanuni na maadili ya Chama.
5.1.5 Awe anakubaliana na Itikadi na falsafa ya Chama.

Sasa wewe mtu kaja leo leo, hata kukaa naye chini kujua kama kajua sera, kanuni, maadili, itifaki na falsafa za chama bado, unataka kumpa kazi ya chama, wewe utasema una akili kweli ?

Hata huko kanisani wanakufundisha katekisimu kwanza na kukubatiza kabla ya kukupa kazi yoyote ya kanisa.

Its depend how you define akili.
Mission in kutwaa dola,ww uko kwenye taratibu itifaki na mambo kama hayo ya nakshi na kuremba,hii haina kuremba .
Thats what happens alongs the way upon accomplishing the mission.
 
Its depend how you define akili.
Mission in kutwaa dola,ww uko kwenye taratibu itifaki na mambo kama hayo ya nakshi na kuremba,hii haina kuremba .
Thats what happens alongs the way upon accomplishing the mission.

Kama mission ni kutwaa dola hata Hitler alikuwa na mission ya kutwaa dola, akatwaa tukaona matokeo yake. Ndiyo tunayotaka hayo? Kuchukua dola bila kujua tunataka kufanya nini ?

Swali, wanataka kutwaa dola ili wafanye nini? Na ili kufikia malengo yao inawabidi wafanye nini hata kabla ya kutwaa dola ?

Kutwaa dola hakuwezi kuwa lengo la mwisho la mwanasiasa, mwanasiasa mwenye lengo la mwisho la kutwaa dola ni mufilisi na wa kuogopwa kama kina Stalin na Mao, kutwaa dola ni mwanzo tu wa kufikia malengo unayotaka mwanasiasa.

Wewe unaposema "hakuna kuremba" mimi naweza kukuambia "huangalii zaidi ya urefu wa pua yako" na unakimbia "mbio za sakafuni" ziishiazo ukingoni.

Lazima ujue ukipata viti bungeni au hata erikali unataka kufanya nini, na wabunge wako watakusaidiaje kufikia malengo hayo, sio unataka kushinda tu hujui nia ya ushindi, au unajua nia ya ushindi lakini hujui kama wabunge hawa mamluki wakiingia bungeni watapiga kura ku support manifesto yako au la.

Utakuwa unacheza tu. Utasababisha migogoro kila siku katika chama na chama kinaweza kufa hata kabla ya 2015.

Sasa tunataka chama kitakachoendelea na kukua naturally au chama kitakacholipuka kama supernovae kwa kuwa na mastar wengi leo lakini kisifie hata 2015 ?
 
Kama mission ni kutwaa dola hata Hitler alikuwa na mission ya kutwaa dola, akatwaa tukaona matokeo yake. Ndiyo tunayotaka hayo? Kuchukua dola bila kujua tunataka kufanya nini ?

Swali, wanataka kutwaa dola ili wafanye nini? Na ili kufikia malengo yao inawabidi wafanye nini hata kabla ya kutwaa dola ?

Kutwaa dola hakuwezi kuwa lengo la mwisho la mwanasiasa, mwanasiasa mwenye lengo la mwisho la kutwaa dola ni mufilisi na wa kuogopwa kama kina Stalin na Mao, kutwaa dola ni mwanzo tu wa kufikia malengo unayotaka mwanasiasa.

nashukuru umeuliza wewe hili swali maana miye nilipoliuliza nilionekana sitaki mabadiliko ati nataka CCM iendelee kukaa madarakani...
 
Umesoma sura ya tano ya Katiba ya CHADEMA kuhusu uanachama na sifa zake ?


5.1.4 Awe anakubaliana na katiba, sera, kanuni na maadili ya Chama.
5.1.5 Awe anakubaliana na Itikadi na falsafa ya Chama.

Sasa wewe mtu kaja leo leo, hata kukaa naye chini kujua kama kajua sera, kanuni, maadili, itifaki na falsafa za chama bado, unataka kumpa kazi ya chama, wewe utasema una akili kweli ?

Hata huko kanisani wanakufundisha katekisimu kwanza na kukubatiza kabla ya kukupa kazi yoyote ya kanisa.
Kiranga unapobatizwa au kusilimu huwa viongozi wanasubiri hadi utakapo ijua dini au ni kukiri kwako kuamini dini hiyo ndicho wanakitazama!

Na hakika kama umewahi kuisoma Biblia vizuri na kuweza kuizungumzia kwa ufasaha nina hakika utapewa nafasi ya kuzungumza au hata kuvuta watu wengine. Tunaona kila siku kwenye TV watu wapya walioingia dini na kwa elimu zao au matukio yao wamepewa nafasi kuitangaza dini.

Kisha hao Wzungu au Waarabu walipokuja Hapa kwetu Afrika aliweza vipi kuwavuta wananchi ikiwa hawakuweza kuzungumza lugha yetu. Na kwa hesabu kubwa wananchi hawakujua hata kusoma!

Mimi nimejiunga na Chadema kwa sababu moja tu..kuwa mstari wa mbele kupigana vita hii pasipo kujali mengine yoote isipokuwa kuwaondoa CCM na Ufisadi nchini..Na maadam swala kubwa linalochukua nafasi kubwa ya uchumi wetu ni Ufisadi basi yeyote yule awe jhata mgombea binafsi anapiga vita Ufisadi atachukua kura yangu na pengine nitajiunga naye. Unapoingia vitani mkuu wangu hujali yanayokuja kwanza ushindi kisha mengine yatajipanga taratibu kwa wakati wake. Ndivyo tulivyoppata Uhuru wewtu na ndivyo nchi zote duniani zilianza na mageuzi.

Kwangu mimi, huu sii uchaguzi wa kutafuta sera bora zaidi kwangu ikiwa musrtakabali wa Taifa letu upo hatarini. kwanza okoa jahazi kisha ndio tafuta dira ya kwenda hata iwe kisiwa kilicho karibu.. Uhai kwanza ndio muhimu. Tukianza kubishana kuhusu itikadi, sera na ilani hali jahazi linajaa maji sote tutaishia kuliwa na Papa...
 
Kiranga unapobatizwa au kusilimu huwa viongozi wanasubiri hadi utakapo ijua dini au ni kukiri kwako kuamini dini hiyo ndicho wanakitazama! Na hakika kama umewahi kuisoma Biblia vizuri na kuweza kuizungumzia kwa ufasaha nina hakika utapewa nafasi ya kuzungumza au hata kuvta watu wenmgine. Tunaona kila siku kwenye TV watu walioingia dini na kwa elimu zao au matukio yao wameopewa nafasi kuitangaza dini. Kisha hao Wzungu au Waarabu walipokuja Hapa kwetu Afrika aliweza vipi kuwavuta wananchi ikiwa hawakuweza kuzungumza lugha yetu. Na kwa hesabu kubwa wananchi hawakujua hata kusoma!

Kwa hiyo unaweza kuikubali imani leo, ukabatizwa leo, na kupewa uaskofu leo siyo ?
 
Kwa hiyo unaweza kuikubali imani leo, ukabatizwa leo, na kupewa uaskofu leo siyo ?
Inategemea na dini. Uislaam kama umesoma kuran na kuifahamu vema, ukaisetiri na kuonyesha uwezo mkubwa wa kufundisha unapewa nafasi hiyo kwani ktk dini ELIMU ndio inakupa wadhifa na sio muda ulojiunga na dini hiyo. Wapo Mapadre waliokuwa wakiisoma Kuran toka wakiwa Ukristru na wameingia Uislaam wakaweza kuizungumzia Kuran kama inavyofundisha na wazuri kuliko hata baadhi ya viongozi wa kiislaam waliobobea, wamepewa mamlaka ya kufundisha dini japokuwa ktk Uislaam hatuna vyeo vya Uaskofu kama katoliki.
Kwa hiyo inawezekana. na nakuhakikishia wapo watu nje ya chama waliosoma katiba, sera na ilani za Chadema na kuzisetiri kuliko kina sisi tulioingia chama muda. Ingekuwa hivyo unavyosema basi bila shaka rais anayetufaa ni Kingunge!
 
Umesoma sura ya tano ya Katiba ya CHADEMA kuhusu uanachama na sifa zake ?


5.1.4 Awe anakubaliana na katiba, sera, kanuni na maadili ya Chama.
5.1.5 Awe anakubaliana na Itikadi na falsafa ya Chama.

Sasa wewe mtu kaja leo leo, hata kukaa naye chini kujua kama kajua sera, kanuni, maadili, itifaki na falsafa za chama bado, unataka kumpa kazi ya chama, wewe utasema una akili kweli ?

Hata huko kanisani wanakufundisha katekisimu kwanza na kukubatiza kabla ya kukupa kazi yoyote ya kanisa.
Kiranga

Mtu kujiunga leo Chadema au CCM si kuwa hajasoma katiba wala sera za chama husika, au kubadili dini leo si kwamba hajasoma Biblia au Quran. Kuna watu tuna vitabu hivyo viwili na huwa tunavisoma vyote mara kwa mara. Huwezi kuniambia kuwa Makamba leo akibadili dini kwenda ukristo atakuwa haijui biblia.

Mfano mimi si mwana CCM wala Chadema lakini ninazo katiba na sera zao zote na huwa nazisoma kwa pamoja na kuzilinganisha, hata humu JF zipo na tunazichambua kila siku, kwa hiyo nikiamua leo nijiunge na CCM huwezi niambia siijui katiba ya CCM, au unataka kutuambia kujua katiba za vyama lazima u-attend special kozi na unatakiwa kuonekana unahudhuria.

Kama wewe ni mwanasiasa makini mfano mbunge sidhani kama utakuwa unasoma katiba ya chama chako tu bila kulinganisha na za vyama vingine, kama unasoma katiba ya chama chako tu utakuwa single minded. Kwa hiyo kujiunga kwa mtu katika chama ni kitendo cha kujionyesha wazi kwa jamii tu na si kuwa hajui kitu kuhusu chama hicho.
 
Kwa hiyo unaweza kuikubali imani leo, ukabatizwa leo, na kupewa uaskofu leo siyo ?
Kiranga tusiongelee mambo ki ujumla jumla, kuamini ni kitu kingine na kubatizwa ni kitu kingine vilevile kupewa uaskofu ni kitu kingine kabisa kuna procedures zake.
 
Exactly my objection.

Now nimeongea sana kuhusu weakness za Regia hapa, kwa hiyo kama namtetea simtetei kwa basis ya kwamba ni mgombea anayefaa na yuko strong.Lakini at least Regia wanamjua, ni mtu wa chama chao, kafanya kazi miaka mingi, ana loyalty kwa chama, na kama kuna matatizo ya exposure anaweza kufundishwa -I hope anafundishika-. Lakini hawa mamluki mapandikizi wa kuja kutokea siku moja kabla ya primaries wanaweza hata kuwa ma spy wa CCM hawa, vyama inabidi viwe makini nao sana, na kama kweli wanataka kufanya kazi za chama wapewe muda kujionyesha mpaka 2015.

CHADEMA kukubali mamluki hawa ni kukubali kwamba wako desperate, hawana principles na wanajali kushinda kwa njia yoyote bila kujali wana sacrifice nini katika ushindi wao.

Kulekule kwa CCM kujuana, oooh ni mwenzetu ..! bla bla, yaani mkuu hata sijui unataka nini? Tuangalie Merit au Kujuana...? Halafu we ndiye unajivika kofia ya ku advocate principles...!
 
(1) Rachel au Regia wamelalamika? Hapana. Wameelewa na kukubaliana na maamuzi ya chama chao. Tuwaunge mkono basi.

Hapana, mi sitaki kuamuliwa mambo na vikao vya chama kama tumeshapigishwa kura, nataka kudumisha Katiba ya chama na misingi ya demokrasia huru.

Wanasiasa wachanga, siku ingine Regia akienda kuomba kura ataambiwa wewe huwezi kupigania kura yangu maana utaenda pembeni kupozana na wenyeviti wa vikao.

Ndio maana watu Iringa na Mwakalebela wao wako mitaani na mahakamani pamoja wanapigania kura yao kuhesabiwa. CHADEMA, upinzan, eti ndio hawaelewi hivi vitu.
 
Kulekule kwa CCM kujuana, oooh ni mwenzetu ..! bla bla, yaani mkuu hata sijui unataka nini? Tuangalie Merit au Kujuana...? Halafu we ndiye unajivika kofia ya ku advocate principles...!

Ultimately chama kinasimamisha mtu kinayemjua, chama hakiwezi kusimamisha mtu kisiyemjua au kitakuwa kinaenda kwenye wehu.

Nilishasema kama mnatafuta watu wenye popular support tu, then vyama vina kazi gani? Tufute vyama tushindanishe watu then.

Mgombea ni lazima awe na imani ya chama, ama sivyo mnaalika chaos tu.
 
Ultimately chama kinasimamisha mtu kinayemjua.
Wapiga kura, sio Chama, ndio wanatakiwa kumjua mtu, wapiga kura ndio wanasimamishi mtu!

Katiba inatamka nani anaweza kuwa mwanachama.

Katiba haikatazi watu wanaotoka chama kingine.

Mwanachama ana haki ya kugombea kiti chochote.

Nataka kujenga jamii ya kuheshimu misingi ya sheria, Katiba na demokrasia huru.
 
Kiranga tusiongelee mambo ki ujumla jumla, kuamini ni kitu kingine na kubatizwa ni kitu kingine vilevile kupewa uaskofu ni kitu kingine kabisa kuna procedures zake.

Exactly my objection, I draw a parallel between religion and politics hapa.

Kuamini = Kuamini
Kubatizwa = Kupewa uanachama
Kuwa Askofu = Kupewa uongozi

Kama "kuamini ni kitu kingine na kubatizwa ni kitu kingine vilevile kupewa uaskofu ni kitu kingine kabisa kuna procedures zake." kwa nini usi apply principle hii hii kwenye vyama vya siasa? Kwamba mtu anatakiwa kupita katika phase ya kuamini (kubadili imani si kitu kidogo unachoweza kufanya kama kubadili nguo, within minutes or a day) kubatizwa/ kupewa uanachama nayo ni process, ideally unatakiwa ukae kusomeshwa ima ni za chama na katiba yake, not something you can do in a hurry, na kupewa uongozi ndio kabisaa, unahitaji kuingia katika manifesto za chama na ma document mengine kama hayo.

Sasa huyu mtu anayeikubali imani, sera, katiba na maadili ya chama, kusoma na kukukubali manifesto, itikadi na falsafa ya chama in a quick minute mimi lazima niwe na mashaka naye kama kweli anakubali kwa dhati au kwa sababu anataka kitu fulani tu, especially kama tunajua wazi kwamba anajiunga na chama baada ya kupigwa kibuti na chama kingine.

Na huwezi kusema eti mtu alikuwa anasoma hivi vitu hata kabla hajajiunga na chama, this is a chance that serious party cannot take, this is a loophole of convenience.

Tuseme tu CHADEMA hawana wagombea na wako desperate kuchukua makapi yeyote ya CCM wanayoweza kupata, no principles or scruples. Hii ndiyo sababu ya kweli, mengine yote longolongo tu.
 
Kiranga,
Mkuu wangu uchaguzi nchini unawapa ushindi wagombea wenye popular vote sasa unachouliza haswa ni kipi?
Chama ni shirika la usafiri lenye vyombo vya usafiri kama mabus na kadhalika, kuwafikisha wananchi kule wanakotaka kwenda lakini hawawezi kufika huko pasipo dereva. Na kila bus linahitaji dereva. Usinambie dereva wa Scania hawezi kuendesha Volvo.. hiki ndio sisi tunachokataa.

Kama Chadema wanahitaji dereva anayeweza kuongoza msafara wa wakazi wa Segelea yupo na kaachishwa kazi na shirika la CCM.. hakuna sababu Chadema wasimpe kazi unless sababu zenyewe zitokane na utovu wa adabu au criminal record. Kinyume cha hapo kama ni mzuri na anaweza kuongoza isipokuwa kumetokea rabsha za unafiki kumuengua, Chadema wanaweza kumtumia mtu huyo (kuimpa ajira) kufika wanakotaka kufika.

Ila kitu kimoja Chadema hawawezi kukifanya.. Chadema hawawezi kuwapa hawa jamaa wadhifa wa juu kukiongoza CHAMA. Yaani kama lile swali lako linalohusiana na kumpa mgeni Uaskofu. Kiongozi yeyote wa Chama ni lazima awe amebobea siasa za chama na kuaminiwa zaidi na sio swala la Ubunge au Udiwani kwani nafasi hizi zinagombewa na mtu yeyote mwenye kufikiri anaweza kushawishi na kushinda kura za popular.
Maadam hawa wageni wote hawashiki madaraka ya juu ya chama sioni ubaya wowote kuwapa udereva wa bus ikiwa wao wataweza kuwafikisha abiria wetu tunakotaka kwenda.
 
Kiranga,
Mkuu wangu uchaguzi nchini unawapa ushindi wagombea wenye popular vote sasa unachouliza haswa ni kipi?
Chama ni shirika la usafiri lenye vyombo vya usafiri kama mabus na kadhalika, kuwafikisha wananchi kule wanakotaka kwenda lakini hawawezi kufika huko pasipo dereva. Na kila bus linahitaji dereva. Usinambie dereva wa Scania hawezi kuendesha Volvo.. hiki ndio sisi tunachokataa.

Kama Chadema wanahitaji dereva anayeweza kuongoza msafara wa wakazi wa Segelea yupo na kaachishwa kazi na shirika la CCM.. hakuna sababu Chadema wasimpe kazi unless sababu zenyewe zitokane na utovu wa adabu au criminal record. Kinyume cha hapo kama ni mzuri na anaweza kuongoza isipokuwa kumetokea rabsha za unafiki kumuengua, Chadema wanaweza kumtumia mtu huyo (kuimpa ajira) kufika wanakotaka kufika.

Ila kitu kimoja Chadema hawawezi kukifanya.. Chadema hawawezi kuwapa hawa jamaa wadhifa wa juu kukiongoza CHAMA. Yaani kama lile swali lako linalohusiana na kumpa mgeni Uaskofu. Kiongozi yeyote wa Chama ni lazima awe amebobea siasa za chama na kuaminiwa zaidi na sio swala la Ubunge au Udiwani kwani nafasi hizi zinagombewa na mtu yeyote mwenye kufikiri anaweza kushawishi na kushinda kura za popular.
Maadam hawa wageni wote hawashiki madaraka ya juu ya chama sioni ubaya wowote kuwapa udereva wa bus ikiwa wao wataweza kuwafikisha abiria wetu tunakotaka kwenda.

First off, uchaguzi nchini hauwapi ushindi wagombea wenye popular vote, unawapa ushindi wagombea waliopitishwa na vyama na kupata popular vote, big difference, so do not try to misrepresent that.

Ninachouliza ni kwamba, kama watu ni purist wa democracy kihivyo na wanataka watu wenye popular support bila chujio la chama, what is the point of having these parties? Kwa nini tusiviondoe vyama vyote na kuwashindanisha wagombea kama watu tu, na atakayepata popular vote awe mbunge, no chama no middleman's b.s ?

Chama kina umuhimu gani kama mnachojali ni popular vote na direct democracy? Next thing you know hata hii nayo mtasema si democracy iliyo direct enough, tutataka turudi kama Athens ya kale, nchi nzima iende Dodoma ku debate budget.

How do you like that now? Si unataka pure democracy bwana?

Democracy iliyo ordered ni lazima iwe na mipaka ya common sense, otherwise itakuwa anarchy. Na moja kati ya mipaka hii ni vyama kuwa na uwezo wa kumkubali au kumkataa mtu kutokana na sababu zake. Kama kuna wanachama wa chama hiki wanampenda sana huyu mtu wanaweza kukubali maamuzi ya chama au kuamua vingine (kuhama chama na huyu mtu etc).

At the end of the day, kama mnaamua kuwa na vyama, vipeni role ya ku play. Haina maana kuwa na vyama wakati maamuzi yote yanafanywa directly na wananchi, kama ni hivyo - tunataka direct democracy- ondoeni vyama vyote, wananchi waamue directly kwa kuwashindanisha watu.

Halafu assertion yako ya ku distinguish uongozi w chama na ubunge katika context ya upinzani bongo sasa hivi ni laughable.Vyama hivi visivyo na visibility, mbunge wa chama ni kiongozi wa chama tayari, ataenda bungeni kutetea sera za chama sasa sijui una maana gani hapo.
 
Kwa hiyo unaweza kuikubali imani leo, ukabatizwa leo, na kupewa uaskofu leo siyo ?

hukusoma " maji haya kwa nini nisibatizwe?"

Sera utaratibu mzuri sana mnaoutaka tatizo ni tofauti na tunavyotaka sisi sisi wengine tunataka CCM itoke hata kama watakao kuja ni wabaya itatatudhuru nini kama pia waliopo wabaya,tuacheni tujirizishe nafsi kuwatoa waliotukandamiza muda murefu "it healthy kukonga nyoyo yako"

Acheni bwana rais bongo akiwa fair na kutoshikilia mafisadi afadhali itapatikana yaani hata mbunge,waziri ...... wakileta mzaa,ufisadi vyombo kama Takukuru ,mahakama ,polisi vikiachwa huru itakuwa bomba hili hamlioni nyie mko kwenye perfection na kuremba .

So sera na urembo wote unao hubiri Kiranga na kupata support toka kwa Mwanakijiji hivi vyote vitafanyika katika ufalme wa CCJ.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom