CHADEMA kataeni kuonewa tena , unyonge wenu sasa basi , wala Msiogope maana Shetani hajawahi kumshinda Mungu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426



Unyama mliofanyiwa dunia nzima imeona na wala hakutakuwa na mshangao wowote iwapo mtakataa kuonewa tena , mmeuawa waziwazi , mmeteswa waziwazi , mmekamatwa hovyo hovyo , mmekatwa mapanga kwa namna walivyotaka , mmebambikwa kesi nyingi za kutunga , mmefungwa bila huruma , mmenyanyaswa kwa kiwango ambacho hakuna binadamu anayeweza kuvumilia

Hujuma za uchaguzi mnazofanyiwa nchi nzima na hasa kwenye Majimbo ya Chato , Mlimba , Kilombero na kwingineko itoshe kuwaamsha na kuanza KUMTUKUZA MUNGU kwa kukataa dhuluma kwa vitendo , ama hakika subira yavuta heri , hakuna tena nafasi ya kukubali kuonewa na watendaji wachovu wasiojua lolote kuhusu Demokrasia .

Mungu ibariki Chadema
 
Yeah, huu ni ujinga kuwaendekeza Hawa mbwa! This time around ni big No!
Naona keyboard warrior uliyekimbia maandamano ya UKUTA na ya Mange Kimambi ukajifungia chooni ukisingizia unaharisha naona uko hewani
 
Mwezi wa kumi mwanzono nilikua Makete, kwenye Lodge niliyofikia kulikua na viongozi wa CCM! Ujinga waliokua wanaongea ni hatari tupu!

Kilichoniuma zaidi ni pale niliposikia wakisema kuwa "ikibidi kumpoteza MTU itabidi iwe hivyo". Nilihisi mwili kutetemeka...
 
Hahahahaha kama wewe hunijui kuna wenzio wananijua
Naona keyboard warrior uliyekimbia maandamano ya UKUTA na ya Mange Kimambi ukajifungia chooni ukisingizia unaharisha naona uko hewani
 
Ukweli kabisa huu! CCM hasa mwenyekiti wao kishawona waoga na anaweza kuwafanya chochote!

Watawala wengi wenye wazimu kama huyu busara hata itoke wapi haiwezi kusaidie kuwarekebisha!!
 
Hivi wanachama na wanaotaka kugombea hawana simatifoni.. mkasambaza matukio mnayodai yanafanyika?

Ila badala ya kupiga kamupeni nyie mupo tu na kulalamika.. kama kawaida yenu..

Musilie musipopigiwa kura.. munaboa hamuchangamshi siasa nchini kama zamani
 
Aisee !
 

Walichangamsha siasa wakati box la kura lilipokuwa linaheshimiwa kwa wastani na sio sasa. Hakuna mwenye akili timamu atashiriki huo upuuzi uitwao uchaguzi. Kama ccm mlijiandaa muone watu wengi wakipiga kura muibe kisha mjifanye mnakubalika, basi watu watawaonyesha hamkubaliki kwa kuacha kupiga Kura.
 
Uchaguzi upi huo mnauongelea wakati mlikataa kujiandikisha kabisa na mkawa mnahamasishana msijiandikishe?

Tatizo lenu lipo hapo, akili hamna kabisa sijui nani aliwaroga, hizi akili za kiwendawazimu ndio mnataka tuziamini tuwape mitaa yetu muongoze? Never
 
Ndugu mleta uzi huu, umekuwa mkweli kwa chama ukipendacho, lakini naona bado uko gizani kuhusu viongozi na waasisi wa wa chama chako.

Hawa ndugu zetu hii familia ya extended Mtei Family unite with the Mbowes hawana ujasiri huo unaoutaka. Hao ndio wenye asili ya lile kabila lenye usemi eti" NTAKUPIGA KISU NA KIKIVUNJIGA UATAKILIPA" methali hiyo imetafsiriwa na wahenga wajuzi wa lugha kuwa ni usemi wa uoga.

Hizo familia mbili ni majasiri wa kujibambikizia mali kwa njia za utata, na hiyo ni historia inayojulika na hakuna cha haramu kwao.

Watu wanamna hiyo hawawezi kujitia mhanga, isipokuwa kwenye mali au pesa ndio mtauwana.

Mbowe hayuko tayari kurudi jela, na hivi sasa kuna siasa za chini chini kesi yake mahakamani isimrudishe jela, na inashughulikiwa na Lowasa.

Kesho akijitokeza mwanasiasa yoyote kugombeakiti cha mbowe , utamsikia mzee mtei akinguruma kama simba kongwe
 
Ndio mana mange aliwaita waoga na wapumbavu
Yaani we we umejitoa kabisa unawataka chadema wachukue hatua
Chadema ni akina nani hao?
 
 
Mkuu umechanganya mambo mengi yaliyojaa uongo kwa 100% , huna hoja na uko nje ya mada
 
Muda wa kugawana fito umefika huo ndio ukweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…