Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika tawi la Kemondo, kata ya Igoma, jijini Mwanza, wameeleza wazi msimamo wao wa kumuunga mkono Tundu Lissu kuwa mwenyekiti wa chama hicho. Wanachama hao wamewataka wajumbe wa uchaguzi wa chama hicho kumchagua Lissu kwa madai kuwa ndiye anayefaa kuliongoza CHADEMA katika kipindi hiki.
Wanachama hao wamesema wanatambua juhudi na mchango mkubwa wa Freeman Mbowe katika uongozi wa chama kwa miaka mingi, lakini wanaamini ni wakati muafaka kwa chama kumpa nafasi kiongozi mpya mwenye uwezo wa kuendeleza mafanikio ya chama.
Soma, Pia: CHADEMA Mwanza: Ni vyema Mbowe apumzike kwa heshima, amuachie nafasi Tundu Lissu
Hata hivyo, wanachama hao wameeleza wasiwasi wao juu ya baadhi ya wanachama ambao wanadaiwa kumuunga mkono Mbowe kwa maslahi yao binafsi. Wamedai kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje, ni mmoja wa wafuasi wa Mbowe ambaye wanahisi hana nia ya dhati kwa maslahi ya chama.
Wanachama hao wamesema wanatambua juhudi na mchango mkubwa wa Freeman Mbowe katika uongozi wa chama kwa miaka mingi, lakini wanaamini ni wakati muafaka kwa chama kumpa nafasi kiongozi mpya mwenye uwezo wa kuendeleza mafanikio ya chama.
Soma, Pia: CHADEMA Mwanza: Ni vyema Mbowe apumzike kwa heshima, amuachie nafasi Tundu Lissu
Hata hivyo, wanachama hao wameeleza wasiwasi wao juu ya baadhi ya wanachama ambao wanadaiwa kumuunga mkono Mbowe kwa maslahi yao binafsi. Wamedai kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje, ni mmoja wa wafuasi wa Mbowe ambaye wanahisi hana nia ya dhati kwa maslahi ya chama.