Uchaguzi 2020 CHADEMA kwa sera hii, mtakomba kura zote za wafanyakazi wa nchi hii, na haya ndio maneno tunayotaka kuyasikia yatayomuangusha Magufuli na CCM yake

Sijui ni kwanini Mimi ninaamini kwenye matumizi ya nguvu kuiondoa ccm kuliko hizi sera zenu? Hivi Kati yenu nani anaamini 2015 Magu alishinda uchaguzi? Chadema hawajaanza kuwa na sera nzuri leo, elimu bure pia ilikuwa sera ya chadema
Sasa ukisema matumizi ya nguvu jiulize against who.....?!

CCm kama chama wanatumia mamlaka, tukijua namna ya kubana hizi mamlaka sio kwa kuwategemea chadema bali sisi kama raia mtaona mabadiliko tunayotaka.

Shida wanachi wa Tanzania wanatumia kauli za upinzani na akili za upinzani kukemea serikali na hapo ndipo serikali wanapata sababu ya kuwa na kiburi maana wanajua wanachi hawajui kujisemea na wanajazwa akili na upinzani.
 
Dunia nzma ajira ni tatizo
Acha kupenda kutetea upuuzi. Hivi Tanzania unahisi tunaukosefu wa ajira au tuna viongozi waliofeli kufufua ajira.

Kwa taarifa yako tatizo la ukosefu wa ajira Tanzania ni matokeo ya mifumo na uongozi wa kipuuzi na sio hali halisi.

Zikisimamishwa taasisi chache tu hapa zitachukua wahitimu hadi zitaanza kutafuta wa kuajiri.......
 
Me sitetei me naongea ukweli wapi wew unadhani hawana tatzo la ajira
 
Kuna sehem nimeandika machinga au bado upo usingizin mkuu
 
Me sitetei me naongea ukweli wapi wew unadhani hawana tatzo la ajira
Hivi kabisa unasema Tanzania tuta tatizo la ajira. Hivi mfano kwenu muwe na chakula cha kutosha ila tu mnampishi mzembe ambaye hapiki kwa wakati au anazembea kupika utasema ninyi kwenu mnanjaa?!

Hapo tatizo sio njaa ni kukosa mpishi serious.
 
Ajira pia,ni pigo kubwa kwa serikali iliyopo madarakani,wanasisitiza viwanda,wakati vyuoni hasa vyuo vya kati na vyuo vikuu wanazalisha walimu wa sanaa na sayansi ambao hawaajiriwi viwandani.
uzuri wa mpira usichezeee nje, ingia ndani uone, JPM hii nchi ameitoa kwenye hali mbaya sana, kwa Tanzania bado hatujafikia huko uchumi wetu ndo kwanza tumeingia wa katikati.
Na ndo maana yeye atengeneza vyanzo vya mapato kwanza.
akifanya yote hayo Kwa kukurupuka bado tutamcheka tu, maana hizo ajira atashindwa kulipa mishahara, hiyo mishahara akiongeza kwa kukurupuka atashindwa kulipa kwa wakti, na ndo maana anajenga uchumi ulio imara ili mambo yote yawezekane kwa badae.
kwa Mr JPM, ni Kiongozi mzuri sana, kwanza kwa jinsi alivyoweza kuhandle issue ya COVID19, watanzania tuwe na shukrani hakuna kiongozi wala wataalam wetu hawa tunaowategemea, wangeweza ivi, ndo kwnza wanaishia kununuliwa na mabeberu.
watanzania tungekufa wengi sana, JPM katumwa na MUNGU tumsupport, tumuombee, ivyo mnavyovitaka mtapata tu.
Issue sio Sisiem, hapa nazungumzia JPM, Kama ni sisiem hata membe bado ni sisiem.
tumchague JPM na mimi naamini hakuna wa kumuangusha.
 
Chadema inambidi aje na namna ya kupata hizo pesa za nyongeza kwa watumishi wa umma bila kuadhiri sekta nyingine kama afya,elimu,maji,na miradi inayoendelea kujengwa.
Miradi isiyo na tija inapaswa kupigwa chini.
 
Hivi kabisa unasema Tanzania tuta tatizo la ajira. Hivi mfano kwenu muwe na chakula cha kutosha ila tu mnampishi mzembe ambaye hapiki kwa wakati au anazembea kupika utasema ninyi kwenu mnanjaa?!

Hapo tatizo sio njaa ni kukosa mpishi serious.
Sasa si ndo serikar inafanyia kaz we kua mvumilivu we huon inaongeza viwanda ,vituo vya afya nk kua mvumilivu ipende nchi yako hata usipopat ajira wew atakuj kupat mjukuu wako
 
Ujinga mtupu,wastaafu mafao yao wanazinguliwa miaka ya kutosha wewe unakuja kuharishia hapa JF.
 
Hii mikakati wakiweza kuinadi kiukweli basi vumbi litatimuka ktk uchaguz ujao. Japo ccm ipo vyema Sana
 
Kama sera ameshindwa kutekeleza si kuna mbadala tuchague watekelezaji!!
Kwanza hizo sera zilukuwa za CDM kadandia kapotea ramani maana hajui pa kutokea!!
Ilani unadandia sera za wenzako sasa wakulima, wafanyakazi na wafanya biashara wote ni mkwamo umebaki na maflyover!!
 
Mkono mtupu haulambwi. Kama wameshindwa kujenga tu makao makuu ya chama chao watawezaje kushawishi hao wafanyakazi? Kumbuka kujenga jengo ni gharama mara moja na Mishahara ni kitu endelevu. Kama ukuongeza mshahara leo maana yake huwezi punguza na hivyo kupunguza uwezo wa kufanya miradi ya kukuza uchumi. Ukiongeza mishahara mfano B 200 kwa mwezi hapo ni maisha yote. Acha tujenge nchi mishahara tutaongezewa tu ili mradi haziliwi na wajanja kama zamani.
 
N Ndoto za mchana hizi.
 
Mimi si support dhuruma,lakini sikubali upumbavu wa kuchukua 99.9 % ya mali asili zetu kama migodi,mafuta,ardhi n.k.kuwakabidhi mabeberu kwa kigezo cha private enterprise za mabeberu. Nenda kwao uone kama utapewa bure mali zao kama kwetu.
Hapa hatuongei theory ndg nakupa facts yanayotojea, Dangote simsikii tena, Cos zimefungwa wenyewe wamekimbia mazingira na taxs sio rafiki!!
Mtaani vijana hawana ajira sera za kurun nchi kiuchumi ni mbovu, unakusanya kodi unauwa tax base, nielewe ndg, hali ni ngumu mbaya!!
 
Hello Mr.lord denning unadhani tunawezaje kuimarisha sekta binafsi kama nchi ili vijana tupate ajira? Nipate maoni yako tafadhali, your positive reply will be highly appreciated sir.
 
CHADEMA!? Ha ha ha ha! Labda huko Kaskazini na kwa wavivu wa kufikiri wa huko Dar na Mara; kwingineko Wananchi walikwishakishtukia hiki Chama, wanakitambua kama ni cha kihuni na wahuni. NCCR Mageuzi ndiyo "wangekaza buti"; angalau kidoogo! Lakini nacho shida ni kuwa Wananchi wanamgroup Mwenyekiti wake pamoja na Freeman. Wanaogopa kabila. Mh, sijui!
 
Hahahaha wenzenu CCM wanawasikiliza tu


Nyie ropokeni..hamjui wenzenu wanaandaa Nini...mtashangaa....sisi wengine tupo pembeni tunaangalia movie...mtashangaa....waulizeni Kinana, Membe, Makamba Snr, Makamba Jnr na Nape...they didn't know what hit them...nyie ongeeni tu...sisi wengine angalau tuna uelewa Fulani kuhusu politics za nchi hii...yataibuliwa Mambo hapa mtaachwa midomo wazi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…