Uchaguzi 2020 CHADEMA mmekosa fikra chanya za kisiasa na mmekosa mwelekeo thabiti wa kisiasa

Uchaguzi 2020 CHADEMA mmekosa fikra chanya za kisiasa na mmekosa mwelekeo thabiti wa kisiasa

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Kwa siku mbili leo na jana CCM kinaendesha mchakato wa kupata wagombea wa nafasi za ubunge kwenye majimbo ya uchaguzi.

Na taifa zima limeelekeza macho kwenye huu mchakato ili kujua nani ataibuka kidedea ili aingie kwenye tatu bora kisha kamati za siasa za CCM za wilaya, mikoa na kisha halmashauri kuu kuchagua jina moja ambalo linafaa kwa ajili ya kugombea kiti cha ubunge.

Kwa jana watu wengi masikio na macho yao yalikuwa kwenye matokeo ya jimbo la Kigamboni na huko mshindi wa kwanza ni Dk Ndugulile na wa Pili ni Paul Makonda.

Pia watu walifuatilia kwa ukaribu matokeo ya jimbo la Kinondoni na Temeke ambapo waliokuwa wabunge wa majimbo hayo hawakupata hata nafasi ya kutinga tatu bora.

Kinachoshangaza ni kuwa baada ya matokeo ya Kigamboni kutoka na Paul Makonda kushika nafasi ya pili wafuasi na wanachama wa CHADEMA wamefurahi na kucheka mpaka jino la mwisho linaonekana. Na hapo ndipo wameonekana kuwa ni wapuuzi na hawana fikra chanya.

Sababu hizi ni kura za maoni tu na kwa CCM zinatoa mwelekeo namna gani wagombea wanakubalika, lakini mchakato ni mrefu. Sababu majina matatu lazima yajadiliwe na kamati za siasa za wilaya, mkoa na kisha NEC kupitisha jina linalofaa. Na kwa mantiki hiyo mchakato bado na mpaka sasa haijulikani nani atapita.

Wao hao wafuasi wa CHADEMA kama wangekuwa na akili timamu wangeshughulika na ya kwao hasa kujinasua sababu CHADEMA sasa haina mvuto tena kwenye jamii ndio maana hata kura za maoni za CHADEMA hakuna anaefuatilia maana ni hawakubaliki na wananchi.

Kama Chama makini walipaswa kuangalia watajisafisha vipi kwa wananchi na kashfa za ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi zinazokikabili chama chao? Sio kukaa na kufurahia Makonda kushika nafasi ya pili.

Ni upuuzi na kukosa fikra chanya za kisiasa. Mambo ya CCM yanawahusu nini? Wakati wo ni mgonjwa aliyekata kauli.
 
Dont dare to wake up a sleeping lion, kuimba kupokezana.....We subiri Chadema ianze mchakatoo
Mchakato waanze mara ngapi? Chadema haina mvuto, hamna mwananchi anafuatilia hata mchakato wao.
 
Sasa kama mliona mambo yenu ya ccm hayawahusu chadema, mngefanyia chumbani! ..kama mmeamua kuweka mambo hadharani wacha adhira iende na mdundo.
 
Kinachoshangaza ni kuwa baada ya matokeo ya Kigamboni kutoka na Paul Makonda kushika nafasi ya pili wafuasi na wanachama wa CHADEMA wamefurahi na kucheka mpaka jino la mwisho linaonekana. Na hapo ndipo wameonekana kuwa ni wapuuzi na hawana fikra chanya.
Ukiwa na akili mfu/finyu utajua watu walifuatilia kwasababu ccm kinapendeka😂, watu walitamani mpumbuvu mwenzako atupwe jararani afu awe mwepesi ndio aonyeshe hizo Tambo zake kuwa yeye ni mkubwa, ndio anakula Raha Peke ake Dunia. Nyambafu we Bashite
 
Sasa kama mliona mambo yenu ya ccm hayawahusu chadema, mngefanyia chumbani! ..kama mmeamua kuweka mambo hadharani wacha adhira iende na mdundo.
Kwani kura za maoni Chadema mnajifungia chumbani? Hazina mvuto. Mnakomalia masualamadogo, sasa Nec ikimpitisha mtakunywa sumu?
 
Kwa siku mbili leo na jana CCM kinaendesha mchakato wa kupata wagombea wa nafasi za ubunge kwenye majimbo ya uchaguzi.

Na taifa zima limeelekeza macho kwenye huu mchakato ili kujua nani ataibuka kidedea ili aingie kwenye tatu bora kisha kamati za siasa za CCM za wilaya, mikoa na kisha halmashauri kuu kuchagua jina moja ambalo linafaa kwa ajili ya kugombea kiti cha ubunge...
Umasikini wa akili mbaya sana. Hivikuna mtu mwenye akili anashabikia ccm, bila ya kutanguliza maslahi binafsi
 
Umasikini wa akili mbaya Sana
Hivikuna mtu mwenye akili anashabikia ccm, bila ya kutanguliza maslahi binafsi
Maslahi binafsi ni nchi kupata maendeleo. Ndio maana hata wewe unanufaika na maendeleo yanayoletwa na Ccm
 
Back
Top Bottom