CHADEMA msipoyakabili/kuyakemea haya magazeti yatawayumbisha wafuasi wenu na kuleta mgawanyiko, yakemeeni

CHADEMA msipoyakabili/kuyakemea haya magazeti yatawayumbisha wafuasi wenu na kuleta mgawanyiko, yakemeeni

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
44,629
Reaction score
83,056
Yakemeeni magazeti haya uchwara msiyape nafasi bila kukanusha upuuzi kama huu.

Content za mikutano yenu yote, Sauti mnazopiza kuhusu Katiba Mpya, wameona hili ndilo la kuwataarifu wananchi? Wakemeeni

Erythrocyte

1684993822901.jpeg

 
Kumbe nyie jamaa nanyi mna vimelea vya kidikteta tu, na ni waoga kama CCM, pia siioni tofauti yenu na CCM kifikra, inaonekana wote mna muelekeo unaofanana, tofauti yenu rangi za vyama tu.

Hayo magazeti hayayumbishi wafuasi, kauli mkingamo za viongozi wa chama ndizo zinayumbisha wafuasi, kama hata adui yako humjui basi huwezi kushinda vita, mnaelekea kushindwa.
 
Yakemeeni magazeti haya uchwara msiyape nafasi bila kukanusha upuuzi kama huu.

Content za mikutano yenu yote, Sauti mnazopiza kuhusu Katiba Mpya, wameona hili ndilo la kuwataarifu wananchi? Wakemeeni Erythrocyte



View attachment 2634029
Hawapaswi kuyakemea, hawatakua na tofauti na CCM, wanachopaswa kufanya ni either kufafanua au kutoa msimamo, badala ya kuruhusu vyombo hivyo vitafsiri msimamo wao.
 
Kumbe nyie jamaa nanyi mna vimelea vya kidikteta tu, siioni tofauti yenu na CCM kifikra, inaonekana wote mna muelekeo unaofanana.

Hayo magazeti hayayumbishi wafuasi, kauli mkingamo za viongozi wa chama ndizo zinayumbisha wafuasi, kama hata adui yako humjui basi huwezi kushinda vita.
nimesema wayakemee, sikusema wayakataze wasiandike, elewa mantiki! Mtu akisema uongo unaukanusha. Silence mens consent
 
Huoni kwamba CDM kuyakemea magazeti ni UDIKTETA?

Sioni kosa lao Mwananchi, maana kutofautiana ndo DEMOKRASIA yenyewe.
 
Huoni kwamba CDM kuyakemea magazeti ni UDIKTETA?
Mtu akisema UONGO unamkemea, ila humkatazi kuandika anachokiamini! Unamkemea asiandike uongo. Unamkemea asitunge uongo akauandika
 
Kwani kutofautiana kumekuwa tabu?

Nani ambaye hajasikia kutoka kwa Lissu kuponda maridhiano na kuyaita ni ujinga?
 
Ni kweli Lisu na Mbowe wana mitazamo na misimamo tofauti kama utakuwa unafuatilia mikutano na hotuba za Lisu utaliona hilo kweupe kabisa,mfano Lisu alivyokuwa kama siyo Morogoro au Dodoma alisema anajua katika maridhiano yaliyofanywa CCM na CHADEMA kuna mpango wa kuachiana majimbo,John Mrema akatoka hadharani akakanusha taarifa hiyo. Inavoonekana Lisu anaamini mwenyekiti kalamba asali ndio maana anafanya usiri wa maridhiano hayo. Ngoja nitafute link niweke hapa.
 
Mbowe na Lissu na CHADEMA kwa ujumla hizo drama/kelele za kujaribu kuwatoa kwenye mstari wanazimudu vizuri sana na hawajawahi kuyumbishwa... KAMA ALISHINDWA JIWE HADI AKAFA BILA KUTUBU SEMBUSE WAKATI HUU..?
 
Mtu akisema UONGO unamkemea, ila humkatazi kuandika anachokiamini! Unamkemea asiandike uongo. Unamkemea asitunge uongo akauandika
Mkuu sipingi angalizo lao, lakini kulingana na uhuru wa vyombo vya habari huwezi kuwazuia kuandika wanachotaka. Ni juu ya CDM kusimamia wanachoamini. Hata hivyo wananchi wengi sio wasomaji wa magazeti. Na wanaosoma wanaweza kuelewa malengo ya kinachosemwa.

Kwangu mimi kama ni kweli Lisu na Mbowe wanapishana tena hadharani, hiyo ndio afya kwa CDM kwani kwanza ndio demokrasia, na ni rahisi sisi Wafuasi kujua yupi ni kiongozi sahihi kwa chama. Haya mambo ya viongozi kukubaliana kila kitu, ndio ilipelekea Lowassa kupokelewa ndani ya CDM bila kupima madhara ya jambo lile.
 
Back
Top Bottom