Asante Rev. Kishoka, naamini wenye mapenzi mema na Chadema wamekuelewa, mimi nimeposti post kuhusu Chadema hawajajipanga, nakubali udhaifu wangu nilitaja majina na udhaifu wao, hivyo ikaonekana ni matukano.
Safu ya uongozi uliyoipendekeza ni nzuri, ila kwa maoni yangu, safu hiyo mpya ya uongozi pia ipinge baadhi ya dhana zilizojengwa dhidi ya Chadema, hivyo kwa ushauri wangu, Mwenyekiti akiwa denomination fulani, katibu mkuu awe denomination nyingine na nilitaja jina, halafu Rwakatare awe naibu katibu mkuu.
Kuna mafanatic wa Chadema ambao bado ni waumini kuwa Chadema ni chama cha kina fulani, na hao akina fulani, ndio wamewakabidhi chama kina fulani, hivyo hao waliokabidhiwa, chama ni mali yao. Ndio maana Zitto alipogombea Uenyekiti nilimuuliza amepata wapi manlaka ya kutaka kwenda juu bila ruhusa ya wenye chama?, Zitto na kiburi chake na kujiamini kwake kulikopitiliza, akataa ushauri wa kuomba baraka kwa wenye chama na kutangaza straight atawavaa wenyewe. Kilichofuatia sote tunakijua.
Hivyo ili kuondoa dhana ya Chadema ni chama cha kina fulani na ndio wamepewa kifamilia, hao kina fulani wakubali kupisha uongozi wa kitaifa zaidi ili kuifuta hiyo dhana ya kifamilia hata kama wamechaguliwa katika chaguzi halali ndani ya chama.
Angalizo kwa wapenzi wa Chadema na mashabiki wa chama hiki, Chadema sasa imefika level za juu kabisa, sio chama chenu tena, ni chama cha wote, ni chama cha kitaifa, kama kinavyopendwa Kaskazini, tungependwa kipendwe vivyo hivyo na Kusini. Tunawashukuru na kuwaheshimu waasisi wa chama hiki tangu walipokiasisi na kukitoa hapo kilipoanza mpaka hapa kilipofika, hapa ndio mwisho wao, its about time kuunda more capable team kukiondoa kwenye the running lane na kukipaisha kabisa angani na kuenea Tanzania yote.