Chadema na dharau kwa amri ya mahakama.

Chadema na dharau kwa amri ya mahakama.

tumewabamba hatujawabamba???tumewa
bamba!!!tena kinooooma."mtataga".

mkuu acha vituko. Asante kwa kuonesha mmetubamba kwa kukahidi agizo la mahakama.
 
Umeeleza vizuri sana, lakini sidhani kama Ruttashobolwa atakubaliana na wewe !

Mwanzoni nilifikiri haelewi nami nikabishana naye kwa posts kadhaa....baadaye nikaconclude kwamba hataki kuelewa kwa makusudi !

Hii kitu iko wazi na very intuitive wala haina haja ya kutafuta mtaalamu wa sheria akutafsirie.
 
Ukiwa na chama kama CHADEMA huweki kiamini ukakipa dola....hawana msimamo
 
Nyie zitto team ni mambumbu
mbu kama yeye.

Dai la zitto kwenye avidati yake aliyowasilisha mahakama ni hofu ya kuvuliwa unachamana na cc hawazi kuwa na dai jipya zaidi ya hapo.
Ambapo kiukweli hakukuwa na hoja ya kujadili juu ya kuvuliwa uwanachama wake au la.

Lakini cc haikuzuiwa kujadili juu ya washiriki wake wakina Mwigamba na Kitila.

katika njia moja au nyingine bila kiadhiri kuvuliwa uwanachama wake ilikuwa lazima ajadiliwe kama mshiriki wa waraka ule uliomuhusu yeye na ndicho alichokisema LISSU na DR. Slaa.
 
Chadema ni chama chenye ndoto za kushika dola na kilitegemewa kiwe chama cha kwanza kuheshimu amri za vyombo vya dola ikiwemo mahakama.

Sote tuna fahamu zitto kabwe aliweka zuio mahakamani dhidi ya kamati kuu ya chadema kujadili uanachama wake na kutokana na mwenendo wa shauri hilo mahakami, mahaka iliagiza chadema kutojadili uanachama wa mh zitto kabwe hadi mwisho wa shauri yani hukumu.

Siku ya ijumaa John Mnyika alionekana kwenye vyombo vya habari akisema hawatojadili uanachama wa zitto kutokana na agizo la mahakama na shauri linalo endelea.

Lakini cha ajabu leo kwenye kikao cha chadema na waandishi wa habari kilicho kuwa na lengo la kutoa na kueleza maazimio ya kamati kuu, wameonesha wazi kuwa wame kahidi agizo la mahakama na kuya dharau na ni wazi walijadili uanachama wa zitto.
Kurugenzi ya Habari imenukuu maneno yaliyo somwa na dr slaa ya kionesha kamati kuu imejadili uanachama wa zitto.
Na nukuu
" chama kina wataka wanachama wote na wapenzi wote kuto shiriki mikutano ,ama shughuli zozote za kisiasa zitakazo andaliwa na zitto kabwe na washirika wake kwa jina la chadema"

kwa hayo maneno hapo juu haihitaji kuwa profesa kuelewa kuwa chadema wamemjadili zitto pamoja na uanachama wake hivyo wame kahidi maagizo ya mahakama na kuyasigina kabisa kama hawatambui uwepo wake.


Hayo maneno yaliyo somwa na dr slaa leo yanaonesha kabisa chadema kuto heshimu mamlaka za nchi.

Wananchi wanatakiwa kujua hawa chadema mambo yanapo kwenda kombo kwa upande wao ndio huwa wa kwanza kusema wanaonewa.

Nimejiuliza kilicho wafanya chadema kuto subiri jumatatu baada ya hukumu ndio wajadili uanachama wa zitto?

Hivi kwanini mh Tundu Lissu unashindwa kuwa mshauri mzuri kwa chama chako?

Chadema kwa hili la leo ni dharau kubwa kwa mahakama.

Karibuni wana jamvi.


Endelea na kunukuu mpaka wataja kunukuu na wewe mwenyewe ila mkae mkijua mtu wenu huyo Zito ndiyo kafyekwa miguu,mkitaka na kama mnampenda kweli mchukue ili tuje kushuhudia mnavyoweza kwenda naye na siasa zake za Usaliti-kama hataishia Kum-Kolimba.
 
Last edited by a moderator:
msome dr slaa umuelewe.

Kama ulivyo sema anasema kama isingekuwa mahakama angeunganishwa na wenzie, lakini tukubaliane kuwa kauli hiyo ina maanisha walisha ujadili uanachama wake, kama sio mahakama na yeye wange mtangaza amefukuzwa kama wenzie.
Ka ame kwenda mbali zaidi kwa kusema wana chama wasi hudhurie mikutano yake aki maanisha hawamtambui kama mwana chama maana walisha ujadili uanachama wake na kumvua uanachama kinyume na agizo la mahakama.

Uanachama wa Zitto ulishajadiliwa kitambo yeye alitakiwa ajieleleze kwa nini asifukuzwe kutokana na ule waraka. Zuio la mahakama ni kama lilikuwa obsolete kutokana na makosa ya kiufundi kwani kimsingi uanachama wake ulishajadiliwa ilikuwa imebaki hukumu baada ya utetezi wa Zitto.
Kuzuia wanachadema kuhudhuria mikutano ya Zitto kutokana na tuhuma alizonazo si kosa chama lazima kichukue hatua za kujilinda na kulinda wanachama wake wasipotoshwe nje au ndani ya chama.
 
inawezekanaje mtu awekewe kikwazo hichi na aendelee kuwa mwana chama?

Hivi baba akisema hakuna kuongea kwa niaba ya familia kutokana na tabia ya kuropoka bila nidhamu... ina maana umekoma kuwa mtoto wa familia...?? Hasa ukizingatia mtoto mwenyewe sio first born; ni mtoto kama wa tatu au wa nne hivi...

Labda wataalamu wa sheria na maswala ya utawala wa siasa watusaidie..
 
Jaribu kufikiri vizuri, Zitto alitakiwa ajitetee mbele ya kamati kuu kwa nini asifukuzwe kutokana na ule wa waraka, lakini yeye akakimbilia mahakamani uanachama wake usijadiliwe, lakini zuio la mahakama halifuti intention ya CC ya kumfukuza Zitto chamani kama angepatikana na hatia. Najua mapenzi yako kwa Zitto yanaweza kukufanya usione ukweli kwani kila mwanadamu ni victim wa mapenzi.
Lissu hakuna alichokosea alichozungumzia ni kuwa Zitto bado ni mwanachama wa CHADEMA kwa sababu za kimahakama lakini kama zisingekuwepo angeungana na wale wenzie wawili waliofukuzwa leo na shitaka lao lilikuwa moja.

Achana na hili gamba sugu,linamboyoyoka tu na mboyoyo ziso mashiko kwa uelewa finyu kipimo cha kichwa cha samaki."NI HIVI VICHWA VYA SAMAKI ALIVYOVISEMA Mh.Karume ndivyo vilivyokuwa vinalishadadia suala la wasaliti ndani ya chadema,hawawezi katu kujadili juu ya lichama lao la kijani lililozidiwa na majanga hadi kutuangamizia TAIFA.Pilipili usiyoila yawawashiani???Kati ya swaga hili walishadadialo na majanga ya ccm ni kipi kiteketeshacho taifa na watu wake?"Haya sasa tunaelekea tamati mliyekuwa mnamdanganya na kumshobokea ndo hayo yashamkuta ya kujitakia nanyi mwaweweseka.@"MABADILIKO NI LAZIMA".
 
endelea na kunukuu mpaka wataja kunukuu na wewe mwenyewe ila mkae mkijua mtu wenu huyo zito ndiyo kafyekwa miguu,mkitaka na kama mnampenda kweli mchukue ili tuje kushuhudia mnavyoweza kwenda naye na siasa zake za usaliti-kama hataishia kum-kolimba.

mkuu asante kwa kuonesha na wewe umeungana nami kukubali kuwa chadema wameidharau mahakama.
 
threat imedhihirisha mwandishi ni div 5 hoja ya mhe Tundu lissu haiwezi akitafakari ataishia kuchora zombi chezea u div 5 kajizua angeendelea kutafakari hoja ya Mwanasheria angemchora zombi chezea mulugo type
 
Ukiwa na chama kama CHADEMA huweki kiamini ukakipa dola....hawana msimamo

Unachekesha!!!Kisa nyie mmeshindwa kuvuana magamba sasa mwaona wiiiivu."KINACHOSTAHILI KUPEWA DOLA NI KILE KINACHOSEMA TUKISHIKA WAIZI NCHI ITAYUMBA".majanga.
 
Kesho wameisha, hawawezi kuendelea kudharau Katiba ya Nchi na amri ya mahakama

Nyinyi ndio wale ambao ukisikia mtu anacheka bila kuliza kulikoni na wewe unaanza kucheka tena kumshinda aliyeaza kucheka na hujui kwanini acheke, nafikiri pia na uvivu wakusoma habari unakusumbua, zzk bado ni mbunge na mwanachama wa chadema soma vizuri uelewe kilichoandikwa usikurupuke tu kama alshabab
 
Haya ndio aliyosema Zitto kuhusu fisadi Mbowe."Lissu anasema nimepewa magari
2 na Mzee Mkono. Anasema
kaambiwa na Mkono. Naamini
Mkono alimwambia pia mwaka
2005 alimpa Freeman Aikaeli
Mbowe tshs 40m ili Mbowe
asifanye kampeni Musoma vijijini.
Nadhani alimwambia pia mwaka
2008 (baada ya orodha ya
mafisadi kutangazwa 2007) Mkono
alimpa Freeman tshs 20m za
uchaguzi wa Tarime na Freeman
akasema kwenye chama ametoa
mkopo na akalipwa. Nadhani
alimwambia pia kuwa Mwaka 2010
Mkono alimpa Mbowe tshs 200m
za kampeni ya Slaa. Pia
hakusahau kumwambia kuwa
Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs
100m za kampeni. Lissu anajua
kuwa gazeti la Tanzania Daima
limeanzishwa na fedha za chama
kutoka Conservative party?
Nimefanya internship yangu kwa
Mkono and Company Advocates
kuhusu masuala ya mikataba.
Mzee Mkono ni Mzee wangu na
alisaini petition ya kumtoa Waziri
Mkuu Pinda.
Lissu awaambie waliyemtuma
wamwambie ukweli wote. Lissu
ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi
namtaka mama wa kifaranga
ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani
na Kinana na Sumaye mwaka 2005
kufuatia deni lake NSSF. Aweke
wazi mkataba kati yake na NHC
kuhusu nyumba ya Umma ilipo
Club Bilicanas.
They must know I am not a push
over. Chacha died, I won't.
Mtu ambaye hawezi kuheshimu
mke wake aliyemzalia watoto
hawezi kunyooshea mtu kidole
kuhusu maadili

Teh,teh,teh!!!Hii ndiyo mizinga aliyokuwa amejiandaa nayo???Ama kweki msaliti ni msaliti tu.
 
mkuu asante kwa kuonesha na wewe umeungana nami kukubali kuwa chadema wameidharau mahakama.

Hata nynyi ssm najua mnampigia debe zito tu, ila mkiambiwa aje kwenu hata nyinyi hamtamtaka watu wenye upeo wa mbali hawawezi kumchukua mtu ambaye anauchu wa madaraka kila kukicha, huyo siasa ndio inaelekea mwisho sasa.
 
Jaribu kufikiri vizuri, Zitto alitakiwa ajitetee mbele ya kamati kuu kwa nini asifukuzwe kutokana na ule wa waraka, lakini yeye akakimbilia mahakamani uanachama wake usijadiliwe, lakini zuio la mahakama halifuti intention ya CC ya kumfukuza Zitto chamani kama angepatikana na hatia. Najua mapenzi yako kwa Zitto yanaweza kukufanya usione ukweli kwani kila mwanadamu ni victim wa mapenzi.
Lissu hakuna alichokosea alichozungumzia ni kuwa Zitto bado ni mwanachama wa CHADEMA kwa sababu za kimahakama lakini kama zisingekuwepo angeungana na wale wenzie wawili waliofukuzwa leo na shitaka lao lilikuwa moja.

Achana na hili gamba sugu,linamboyoyoka tu na mboyoyo ziso mashiko kwa uelewa finyu kipimo cha kichwa cha samaki."NI HIVI VICHWA VYA SAMAKI ALIVYOVISEMA Mh.Karume ndivyo vilivyokuwa vinalishadadia suala la wasaliti ndani ya chadema,hawawezi katu kujadili juu ya lichama lao la kijani lililozidiwa na majanga hadi kutuangamizia TAIFA.Pilipili usiyoila yawawashiani???Kati ya swaga hili walishadadialo na majanga ya ccm ni kipi kiteketeshacho taifa na watu wake?"Haya sasa tunaelekea tamati mliyekuwa mnamdanganya na kumshobokea ndo hayo yashamkuta ya kujitakia nanyi mwaweweseka.@"MABADILIKO NI LAZIMA".
 
mkuu acha vituko. Asante kwa kuonesha mmetubamba kwa kukahidi agizo la mahakama.

Kukahidi ndio nini???Hebu niondokee na umburula wako 'kichwa samaki' mkubwa weye,tafuta kazi acha kuishi maisha ya ujanjaujanja na kuungaunga kwa upambe.
 
Kama hauna cha kuandika bora ukalala maana kila siku naona maneno ya namna hii yanajirudiarudia,sasa buku saba inahusiana nini na topic hii au ndo mawazo finyu

Acha hasira magamba tulieni mmeze vidonge vya kutibu ukichaa wenu.
 
Sasa nini kimekuchanganya? Zitto si kaenda pinga uanachama na si kuvuliwa uongozi.Sasa aandae mikutano ya chama km nani?Duh wenge limewazidi...
 
Back
Top Bottom