Otorong'ong'o
JF-Expert Member
- Aug 17, 2011
- 37,957
- 26,414
Hapa tunacho jadili ni kauli za viongozi wa chadema na wameyaongea na wewe umesikia kabisa na ni wazi wame ujadili uanachama wa zitto.
amri ya mahakama ilikuwa uanachama wa zitto usijadiliwe ...sio kila kitu kuhusu zito kisijadiliwe..
hata kama unavyodai chadema imekiuka amri ya mahakama, hivi nikuulize kwa akili yako fupi mahakama inaweza ikarejesha uanachama wa zitto...?
Unajisumbua..
Ujielewi wewe!Je mtu anapokua na nyumba au shamba,ambayo ameipangisha,alafu anaamua kuuza kesho kutwa,na mpangaji akaenda kuzuia mahakani sababu yeye kama mpangaji haki zake zimekiukwa!mahakama ikazuia,je wewe utauza nyumba tu sababu hatujui ulipataje?Jitambue,kuna taasis isiyo na katiba?chadema kama chama katiba yao inawapa mamlaka ya kumpiga maruufuku mtu yeyote kujifanya shughuli za chama that has nothing to do with judicial proceeding. pili uanachama wake haujajadiliwa ungejadiliwa asingekuwa mwanachama leo hii angekuwa kama mkumbo na mwenzake mwigamba
Mkuu kama hii thread unahisi haifai, bonyeza kitufe cha 'report abuse' hapo juu ya hiiyo thread then mods watapima.Hii thread ifungwe haina mashiko....Ni mipasho ya misukule ya Zitto..
mahakama iliizuia kamati kuu kujadili uanachama zitto na wamezingatia hilo ndo maana zitto bado ni mwanachadema. Tamko lile limetolewa kwenye mkutano na wanahabari. Subiri baada ya kesho km utamsikia tena huyo kibaraka wa ccm.Soma maneno ya dr slaa ndio utaelewa nasema nini. kwa maneno ya dr slaa ni wazi wameujadili uanachama wa zitto.
shauri uanachama wa zitto ndani ya chadema kutojadiliwa na kamati kuu.
Agizo la mahakama lina wataka chadema kutojadili uanachama wa zitto hadi mahakama itakapo toa hukumu.
Kuna tofauti kati ya kumjadili zitto na kujadili uanachama wa zitto. Shughulisheni bongo zenu, msilete mihemko isiyo na msingi.
Haya ndio aliyosema Zitto kuhusu fisadi Mbowe."Lissu anasema nimepewa magari
2 na Mzee Mkono. Anasema
kaambiwa na Mkono. Naamini
Mkono alimwambia pia mwaka
2005 alimpa Freeman Aikaeli
Mbowe tshs 40m ili Mbowe
asifanye kampeni Musoma vijijini.
Nadhani alimwambia pia mwaka
2008 (baada ya orodha ya
mafisadi kutangazwa 2007) Mkono
alimpa Freeman tshs 20m za
uchaguzi wa Tarime na Freeman
akasema kwenye chama ametoa
mkopo na akalipwa. Nadhani
alimwambia pia kuwa Mwaka 2010
Mkono alimpa Mbowe tshs 200m
za kampeni ya Slaa. Pia
hakusahau kumwambia kuwa
Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs
100m za kampeni. Lissu anajua
kuwa gazeti la Tanzania Daima
limeanzishwa na fedha za chama
kutoka Conservative party?
Nimefanya internship yangu kwa
Mkono and Company Advocates
kuhusu masuala ya mikataba.
Mzee Mkono ni Mzee wangu na
alisaini petition ya kumtoa Waziri
Mkuu Pinda.
Lissu awaambie waliyemtuma
wamwambie ukweli wote. Lissu
ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi
namtaka mama wa kifaranga
ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani
na Kinana na Sumaye mwaka 2005
kufuatia deni lake NSSF. Aweke
wazi mkataba kati yake na NHC
kuhusu nyumba ya Umma ilipo
Club Bilicanas.
They must know I am not a push
over. Chacha died, I won't.
Mtu ambaye hawezi kuheshimu
mke wake aliyemzalia watoto
hawezi kunyooshea mtu kidole
kuhusu maadili
Mkuu hawa Visebengo wa Lumumba huwa wamekremishwa lines za kuja kuchafua hewa hapa jukwani... Darasa ulilompatia kama haja kuelewa tena baaaaasi... Kinacho ni kera kuliko ni jinsi ambavyo hawana uwezo wa kupambanua mambo kwa mapana! Hawaoni hawasikii hawapimi athari za kupanda kwa bei ya umeme na gesi kwa mapana na marefu! Hawaoni athari za kutoa eneo lote la bahari kwa wawekezaji! Hawani athari za kuwaua wananchi badala ya majangili.... nahisi humu ndani wanaoandika pengine ni robot...Lumumba CCM yote ni Janga kwetu Watanzania, Nshindwa kuelewa alie format brains zao kiasi cha wao kushabikia ngono 24/7 badala ya kujadili mambo yenye maslahi mapana kwa nchi yetu ...
Kuna tofauti kati ya kumjadili zitto na kujadili uanachama wa zitto. Shughulisheni bongo zenu, msilete mihemko isiyo na msingi.
Mimi simwelewi kabisa! Na kwa kweli nimejitahidi sana kutaka kumwelewa lakini wapi bana...kila nikijaribu naishia patupu!
Anachokitaka yeye katika kwenda kwake mahakamani ni nini? Maana tuseme hata akishinda huko mahakamani (na sijui hata atashinda kitu au jambo gani) na akaendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA, tayari mahusiano yake na uongozi wa CHADEMA pamoja na sehemu kubwa tu ya wanachama yameshaharibika.
Ataendeleaje kuwa mwanachama wa CHADEMA katika mazingira kama hayo? Kaazi kweli kweli!
Zitto kasema hayo maneno lini na wapi ?
Aliyeleta huu upuzi kwa mara ya kwanza alidai ameuota kwenye facebook page ya Zitto.....
Kwenye face book ya Zitto hakuna kitu kama hiki........
Sasa nyie maCCM mlivyoishiwa maneno ya propaganda (manake propaganda zote zimeshindwa kulipa), mmeamua kumwekea kipenzi chenu maneno mdomoni....poleni sana !
Na hivi karibuni tunampiga chini !
USilete mambo ya hisia hapa, lete vielelezo, bush lawyer.wakati Tundu Lissu anasema hayo kuwadanganya watu, we soma maneno ya dr slaa aliyo nukuliwa na kurugenzi ya habari na yanaonesha wazi uanachama wa zitto umejadiliwa.
HEBU NIAMBIE HAYO MANENO YA DR SLAA YANA MAANA GANI? KAMA LISSU ANASEMA ZITTO BADO NI MWANA CHAMA NA HAYO MANENO YANATOKA WAPI NA YANA MAANISHA NINI?
Chadema ni chama chenye ndoto za kushika dola na kilitegemewa kiwe chama cha kwanza kuheshimu amri za vyombo vya dola ikiwemo mahakama.
Sote tuna fahamu zitto kabwe aliweka zuio mahakamani dhidi ya kamati kuu ya chadema kujadili uanachama wake na kutokana na mwenendo wa shauri hilo mahakami, mahaka iliagiza chadema kutojadili uanachama wa mh zitto kabwe hadi mwisho wa shauri yani hukumu.
Siku ya ijumaa John Mnyika alionekana kwenye vyombo vya habari akisema hawatojadili uanachama wa zitto kutokana na agizo la mahakama na shauri linalo endelea.
Lakini cha ajabu leo kwenye kikao cha chadema na waandishi wa habari kilicho kuwa na lengo la kutoa na kueleza maazimio ya kamati kuu, wameonesha wazi kuwa wame kahidi agizo la mahakama na kuya dharau na ni wazi walijadili uanachama wa zitto.
Kurugenzi ya Habari imenukuu maneno yaliyo somwa na dr slaa ya kionesha kamati kuu imejadili uanachama wa zitto.
Na nukuu
" chama kina wataka wanachama wote na wapenzi wote kuto shiriki mikutano ,ama shughuli zozote za kisiasa zitakazo andaliwa na zitto kabwe na washirika wake kwa jina la chadema"
kwa hayo maneno hapo juu haihitaji kuwa profesa kuelewa kuwa chadema wamemjadili zitto pamoja na uanachama wake hivyo wame kahidi maagizo ya mahakama na kuyasigina kabisa kama hawatambui uwepo wake.
Hayo maneno yaliyo somwa na dr slaa leo yanaonesha kabisa chadema kuto heshimu mamlaka za nchi.
Wananchi wanatakiwa kujua hawa chadema mambo yanapo kwenda kombo kwa upande wao ndio huwa wa kwanza kusema wanaonewa.
Nimejiuliza kilicho wafanya chadema kuto subiri jumatatu baada ya hukumu ndio wajadili uanachama wa zitto?
Hivi kwanini mh Tundu Lissu unashindwa kuwa mshauri mzuri kwa chama chako?
Chadema kwa hili la leo ni dharau kubwa kwa mahakama.
Karibuni wana jamvi.