CHADEMA na Makamanda tujifunze Mbinu za Medani #1


Inatia moyo kuwa hakuna asiyejua umuhimu wa katiba mpya. Bila shaka basi suala ulilomaliza nalo la madaraka ni kujichanganya tu.

Ila bado umekwenda kunilisha maneno lukuki nisiyo husika nayo kabisa. Laiti ungekuwa umenisoma vyema na kutambua kuwa:

"Hayuko adui wala rafiki wa kudumu bali agenda," bila shaka usingefanya hivyo.

Hata hivyo kwa bahati mbaya zaidi hukujibu swali langu la msingi:

"Kwenye harakati hizi, kuna wadai, wadaiwa, maadui, washirika na wasiohusika."

Nakazia: Wewe ni yupi katika hao?
 
Usifananishe mandela na siasa zetu zilivo ni vitu viwili tofauti mandela alikuwa na support na WAnanchi na dunia pia tofauti na huku wananchi hata hawajali

Inafahamika kuwa adui yetu na mdaiwa wetu wana ka-kujidanganya hako.

Kujaribu kumtofautisha Mandela na sisi ila kuyarejea mauaji ya Rwanda kuwahadaa wasioelewa kuwa ndiyo ambayo Chadema wanayotaka kuyaleta ni hulka ya maadui zetu.
 

Habari hii ni mbaya sana kwa wote mdaiwa na pia adui zetu.

Muhimu kujua na kuwa wazi. Haipo katiba mpya bila kuyajaza pomoni magereza yao.

Huo ni uchaguzi wao ambao sisi ni lazima kuwa tayari kuuridhia.
 
Unataka wafanyaje ?

1. Tulipo tunadai katiba mpya ambayo ni haki yetu. Mdaiwa hayuko tayari kuridhia. Mengine yote haya ni longo longo tu.

Your browser is not able to display this video.


2. Mdaiwa na maadui zetu wamedhamiria kwa vitendo kutuzuia kudai haki yetu, yakiwamo matumizi ya nguvu. Hatuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuingia kwenye mpambano huu Mtukufu.
3. Silaha na ngao zetu kuu ni umoja na wingi wetu. Utayari wetu wa kuyajaza magereza yao pomoni ni silaha yetu kuu ya hakika kamili.
4. Ushindi ni dhahiri. Panapo nidhamu thabiti safari itakuwa ni fupi na yenye gharama ndogo zaidi.
5. Tuwaombe marafiki zetu, wasiohusika au wanaodhani hawahusiki kutuelewa. Hizi pilipili wala hazina sababu ya kuwa washa washa.

Tuko kwenye njia sahihi.

Aluta Continua!
 
πŸ‘πŸ‘πŸ‘
 
Haujali wewe, wananchi wangekuwa hawajali, wasingeenda kuwakamata kanisani wakidai wamekusanyika bila kibali. Tulia, time will tell soon
Wanajipa matumaini tu ya muda mfupi hao ccm na vibaraka wao. Waulize nani aliandika maoni ya wananchi nchi nzima chini ya Tume ya Warioba?
 
Ana laana ya kushangilia kifo cha Magufuli huyo ataliwa na kulelewa mpaka mwisho wake.
 
Wanajipa matumaini tu ya muda mfupi hao ccm na vibaraka wao. Waulize nani aliandika maoni ya wananchi nchi nzima chini ya Tume ya Warioba?

Nini tusichokijua katika medani hii? Kwani Tahrir ilikuwaje? Kwani watu wa kukamatwa Medani ya Tahrir, Misri walikuwa wamejificha?

Medani ya Tahrir na yetu, zote baba mmoja mama mmoja.

Magereza yakijaa wakakosa pa kutuweka, mchakato wa katiba mpya utaridhiwa na wote walioshikiliwa kwenye dhuluma zao watawekwa huru:

1. Tunazo sababu zote za kuvipigana vita hivi.
2. Tunayo nia ya kuvipigana vita hivi.
3. Tunao uwezo wa kuvipigana vita hivi.
4. Tunayo haki ya kuvipigana vita hivi.

Yote tisa, kumi ni kuwa hivi ni vita vya amani na kwa mujibu wa sheria.

God bless.
 
Ana laana ya kushangilia kifo cha Magufuli huyo ataliwa na kulelewa mpaka mwisho wake.

Kifo cha Magufuli kilishangiliwa na watu wengi sana. Katika hao wamo ndugu jamaa na marafiki wa Ben Sanane, Mawazo, Azory, Lissu, wa waliopotea ikiwamo wa kwenye viroba na wengi wengine waliokumbana na dhuluma za kishetani za shujaa wako huyu:



Sina hakika ni nani unayemwongelea wewe kamili aliyeshangilia katika hao.

Hudhani hao walikuwa na haki ya kushangilia kama waliokuwa wamekwazwa na kina Iddi Amini, Hitler, Osama bin Laden, Tony Blair na hata George Bush katika maeneo yao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…