Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Mpambano wa FAM na TAL una afya
''Chawa Wanashona Sanda, Wapambe wanachimba kaburi
Kwa wiki, habari zinazotamalaki ni mpambano wa Uenyekitiki wa CHADEMA (CDM) kati ya Mh Mbowe (FAM) na Mh Lissu (TAL). Mvutano kati yao umepandisha joto la siasa nchini kuliko wakati mwingine.
Joto la siasa limezaa kinachojulikana kama (The good, the bad and the ugly) kwa tafsiri isiyo rasmi 'uzuri, ubaya na ubovu' kwa maana katika utatu lipo jema , baya na bovu. Huo ndio msingi wa kusema kuna fursa, makosa na kisha anguko!
CDM wanaita ''minyukano ndani ya chama''. Mwandishi Mark Twain aliwahi kusema '' History never repeats itself, but it does often rhyme'' akimaanisha tukio halitokei tena katika hali ile ile lakini mara nyingi laweza kuwa na ufanano sana unaoleta hisia kama zile za awali
Waziri mkuu wa Uingereza Bw. W.Churchill alisema '' study history, study history. In history lies all the secrets of statecraft'' akimaanisha jifunze historia, ndani yake yapo maarifa ya kiutawala
Sehemu ya I: Historia ya minyukano
Si rahisi kupitia matukio kwa kina au usahihi wake hata hivyo ni muhimu tukapata ufahamu wa nini kilitokea ili tujifunze na tuoanishe na mnyukano uliopo
NCCR , kamati ya kupigania mageuzi ya katiba na mifumo ya nchi, baadaye ikawa chama cha siasa NCCR-Mageuzi. Masumbuko Lamwai (R.I.P) akawa diwani, kisha Mbunge akiwa na Mabere Marando. CCM ikaingia mtafaruku na Mrema aliyehamia NCCR-Mageuzi. Uchaguzi wa 1995 NCCR ilikuwa tishio hadi CCM walipofanya ''maarifa' yao!
Bundi akatua NCCR, mgogoro wa uongozi kati ya ' Wasomi na Mrema'' ukazuka.
Mkutano wa Tanga ukaisha kwa ngumi na mateke. Mrema akatambua hatma si nzuri akatimkia TLP.
NCCR ikabaki na makovu makubwa kwasababu Mrema alikuwa na Wafuasi.
Mh J.Mbatia na S.Mvungi ( R.I.P) wakajitahidi kukirejeshea chama uhai.
Katika Uchaguzi wa Mwenyekiti uliofanyika Diamond na kuonyeshwa na TV, kila Mtanzania alikubali kwamba NCCR-Mageuzi ilifanya uchaguzi bora sana ukiwa na uhindani wa hoja na si matusi.
Mwenyekiti Mbatia akafanikiwa kuirudisha NCCR katika ''ramani'.
Kosa la mbatia ni kufanya ' Maridhiano' na JPM. Kwa ukubwa wa makovu ya siku nyuma , NCCR ikawa '' vulnerable'' ikishambuliwa na CCM kwa msaada wa Ofisi ya vyama! NCCR imebaki katika kabrasha.
Minyukano haikuiacha NCCR salama ingawa ilidhaniwa itatoka salama kwa ukubwa wake.
CUF: Minyukano kati ya Maalimu Seif (R.I.P) and J.Mapalala (R.I.P). Mgogoro ukamhusisha Hamad Rashid, Maalimu alikuwa na Prof Lipumba. Katika hali isiyotarajiwa Lipumba akakacha CUF.
Maalimu akafanya kosa la kifundi, akabaki na chama akiwa yeye ndiye taasisi.
Lipumba akarejea na kutumia hoja za kiufundi akisaidiwa na CCM, Mahakama na Ofisi ya vyama.
Maalimu Seifu hakuwa na pa kutokea, akatimkia ACT Wazalendo. CUF ikabaki na makovu ya minyukanano na haijawahi kutengemaa tena. Minyukano haijaiacha CUF Salama.
UDP: Chama kilichokuwa na nguvu kanda ya ziwa. Mgogoro ukazuka kati ya Mwenyekiti M.Cheyo na Amani Nzugile (Jidulamambambasi). Mh Cheyo akapigiwa pande na CCM.
DP ikabaki mfukoni kwa Cheyo. Minyukano haijaiacha UDP Salama.
ACT Wazalendo: Uchaguzi ukamhusisha Babu Duni na Othman Masoud (OMO).
Duni akionekana mwanafunzi aliyefuzu wa Maalimu. OMO akionekana msomi mwenye misimamo mikali. Busara ikatumika, Duni ''akatema Bungo'' si kwa hiari, ni kwa shari.
Tayari kulikuwa na minyukano iliyotishia kukigawa Chama. Busara zikanusuru madhara
CHADEMA:
Waheshimiwa Mtei na Makani katika uongozi kwa miaka 10. Mh Mbowe akachukua uongozi 2003.
C.Wangwe akaonyesha nia ya kutaka kiti, mtafaruku ukarindima. Bahati akafariki kwa ajali ya gari.
Zitto Kabwe akisaidiwa na K,Mkumbo na Mwigamba wakaanda mpango kimya kimya.
Hoja zao zilikuwa na mashiko, namna waliyotaka kutekeza mpango ilikuwa ni hovyo, hawakuungwa mkono.
Mh F.Sumaye akagombea nafasi ya kanda. Tetesi zikaenee anautaka uenyekiti.
Katika hali ya kushangaza aligaragazwa 'mchangani' katika kanda na ilikuwa 'inside job' ikiongozwa na ' Vijana' watiifu.
Mwaka huu, TAL akijua mbinu nyingi chafu alivuta muda na kushtukiza dakika za mwisho, anautaka uenyekiti. Hili ndilo chimbuko la mnyukano ambao ni mkubwa kuliko misuko suko ya nyuma!
Je, mnyukano huu utaibeba CDM au historia itajidhihiri kwa namna ile ile ingawa si kwa chama kile kile!
Sehemu ya II inafuata
''Chawa Wanashona Sanda, Wapambe wanachimba kaburi
Kwa wiki, habari zinazotamalaki ni mpambano wa Uenyekitiki wa CHADEMA (CDM) kati ya Mh Mbowe (FAM) na Mh Lissu (TAL). Mvutano kati yao umepandisha joto la siasa nchini kuliko wakati mwingine.
Joto la siasa limezaa kinachojulikana kama (The good, the bad and the ugly) kwa tafsiri isiyo rasmi 'uzuri, ubaya na ubovu' kwa maana katika utatu lipo jema , baya na bovu. Huo ndio msingi wa kusema kuna fursa, makosa na kisha anguko!
CDM wanaita ''minyukano ndani ya chama''. Mwandishi Mark Twain aliwahi kusema '' History never repeats itself, but it does often rhyme'' akimaanisha tukio halitokei tena katika hali ile ile lakini mara nyingi laweza kuwa na ufanano sana unaoleta hisia kama zile za awali
Waziri mkuu wa Uingereza Bw. W.Churchill alisema '' study history, study history. In history lies all the secrets of statecraft'' akimaanisha jifunze historia, ndani yake yapo maarifa ya kiutawala
Sehemu ya I: Historia ya minyukano
Si rahisi kupitia matukio kwa kina au usahihi wake hata hivyo ni muhimu tukapata ufahamu wa nini kilitokea ili tujifunze na tuoanishe na mnyukano uliopo
NCCR , kamati ya kupigania mageuzi ya katiba na mifumo ya nchi, baadaye ikawa chama cha siasa NCCR-Mageuzi. Masumbuko Lamwai (R.I.P) akawa diwani, kisha Mbunge akiwa na Mabere Marando. CCM ikaingia mtafaruku na Mrema aliyehamia NCCR-Mageuzi. Uchaguzi wa 1995 NCCR ilikuwa tishio hadi CCM walipofanya ''maarifa' yao!
Bundi akatua NCCR, mgogoro wa uongozi kati ya ' Wasomi na Mrema'' ukazuka.
Mkutano wa Tanga ukaisha kwa ngumi na mateke. Mrema akatambua hatma si nzuri akatimkia TLP.
NCCR ikabaki na makovu makubwa kwasababu Mrema alikuwa na Wafuasi.
Mh J.Mbatia na S.Mvungi ( R.I.P) wakajitahidi kukirejeshea chama uhai.
Katika Uchaguzi wa Mwenyekiti uliofanyika Diamond na kuonyeshwa na TV, kila Mtanzania alikubali kwamba NCCR-Mageuzi ilifanya uchaguzi bora sana ukiwa na uhindani wa hoja na si matusi.
Mwenyekiti Mbatia akafanikiwa kuirudisha NCCR katika ''ramani'.
Kosa la mbatia ni kufanya ' Maridhiano' na JPM. Kwa ukubwa wa makovu ya siku nyuma , NCCR ikawa '' vulnerable'' ikishambuliwa na CCM kwa msaada wa Ofisi ya vyama! NCCR imebaki katika kabrasha.
Minyukano haikuiacha NCCR salama ingawa ilidhaniwa itatoka salama kwa ukubwa wake.
CUF: Minyukano kati ya Maalimu Seif (R.I.P) and J.Mapalala (R.I.P). Mgogoro ukamhusisha Hamad Rashid, Maalimu alikuwa na Prof Lipumba. Katika hali isiyotarajiwa Lipumba akakacha CUF.
Maalimu akafanya kosa la kifundi, akabaki na chama akiwa yeye ndiye taasisi.
Lipumba akarejea na kutumia hoja za kiufundi akisaidiwa na CCM, Mahakama na Ofisi ya vyama.
Maalimu Seifu hakuwa na pa kutokea, akatimkia ACT Wazalendo. CUF ikabaki na makovu ya minyukanano na haijawahi kutengemaa tena. Minyukano haijaiacha CUF Salama.
UDP: Chama kilichokuwa na nguvu kanda ya ziwa. Mgogoro ukazuka kati ya Mwenyekiti M.Cheyo na Amani Nzugile (Jidulamambambasi). Mh Cheyo akapigiwa pande na CCM.
DP ikabaki mfukoni kwa Cheyo. Minyukano haijaiacha UDP Salama.
ACT Wazalendo: Uchaguzi ukamhusisha Babu Duni na Othman Masoud (OMO).
Duni akionekana mwanafunzi aliyefuzu wa Maalimu. OMO akionekana msomi mwenye misimamo mikali. Busara ikatumika, Duni ''akatema Bungo'' si kwa hiari, ni kwa shari.
Tayari kulikuwa na minyukano iliyotishia kukigawa Chama. Busara zikanusuru madhara
CHADEMA:
Waheshimiwa Mtei na Makani katika uongozi kwa miaka 10. Mh Mbowe akachukua uongozi 2003.
C.Wangwe akaonyesha nia ya kutaka kiti, mtafaruku ukarindima. Bahati akafariki kwa ajali ya gari.
Zitto Kabwe akisaidiwa na K,Mkumbo na Mwigamba wakaanda mpango kimya kimya.
Hoja zao zilikuwa na mashiko, namna waliyotaka kutekeza mpango ilikuwa ni hovyo, hawakuungwa mkono.
Mh F.Sumaye akagombea nafasi ya kanda. Tetesi zikaenee anautaka uenyekiti.
Katika hali ya kushangaza aligaragazwa 'mchangani' katika kanda na ilikuwa 'inside job' ikiongozwa na ' Vijana' watiifu.
Mwaka huu, TAL akijua mbinu nyingi chafu alivuta muda na kushtukiza dakika za mwisho, anautaka uenyekiti. Hili ndilo chimbuko la mnyukano ambao ni mkubwa kuliko misuko suko ya nyuma!
Je, mnyukano huu utaibeba CDM au historia itajidhihiri kwa namna ile ile ingawa si kwa chama kile kile!
Sehemu ya II inafuata