Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #21
Yatatokananayo CHADEMA
1. Mbowe (FAM) na Huruma
Kampeni zimeendelea kwa kasi kwa kutumia vyombo vya habari. Tumeeleza awali, hata vyombo ''mahasimu' hutoa nafasi (air time) kwa Wagombea wa CDM! kinyume kabisa na taratibu zao!!!
FAM akihojiwa alisema kwa hisia sana kuhusu fadhila zake kwa Wapinzania wake akiwemo Mh G Lema.
Kwa nadra sana, akihojiwa ,FAM alisema akichaguliwa ataweka kipindi cha uchaguzi cha miaka 3 ili kuwiana na chaguzi za Serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu.
Hoja: Tulieleza Team FAM wanatafuta huruma kwa kueleza nini waliwafanyia wapinzania wao na si nini watafanyia Chama. Tulionya Team TAL wakiingia katika malumbano hayo watapoteza.
Katika hali ya kushangaza Team TAL wameingia katika malumbano ya fadhila wakitekeleza hoja zao za nini wanataraji kufanya wakipewa uongozi. Katika hili, Team FAM imewavuta wakaingia 18.
Hoja ya vipindi 3 iliyotolewa na FAM haina mashiko. Miaka 5 ingeweza kupangwa kwa kuangalia kalenda za chaguzi za Kitaifa. Swali, ni kwanini kwa miaka 21 FAM hakuweza kuliona hili au kulifanyia kazi?
Uongozi wa miaka 3 haumpi nafasi kiongozi kutekeleza azma na ahadi au mipango yake Kichama
2. Tundu Lissu (TAL) na Urpokaji
Kuna tuhuma kutoka Team FAM kwamba TAL ni mropokaji, wakiitumia kumdhalilisha au kumdunisha.
Hoja: Kuropoka kwa maana ya kiswahili kunaweza kuwa na maana mbili
Kwanza, kuongea jambo bila ithbati au uhakika. Ni aina ya uzushi unaojengwa bila mantiki
Pili, kuropoka ni kutoa maneno yaliyokuwa siri kwa kudhamiria au kwa bahati kutoka
TAL anapotoa hoja mara zote zinajengwa kwa mantiki na hutoa hadi chanzo.
Mfano, alibanwa aeleze ushahidi wa kuhongwa pesa. TAL alijibu, aliyetoa habari hizo ni Marehemu.
TAL akaendelea kusema ikiwa ni uzushi itolewe video inayoonyesha aliomba radhi.
Kwa tafsri, TAL anakuwa mropokaji kwa hoja ya pili hapo juu, kwamba anatoa habari ambazo zilitakiwa ziwe siri. Inaweza kuwa kweli lakini je wanaomtuhumu huzingatia ukweli kwamba TAL anahitaji kujitetea?
TAL anapojitetea huambiwa ni Mropokaji, anazungumza yasiyotakiwa kuzungumzwa.
Wanaomtuhumu hawafikirii gharama za tuhuma, na wangependa TAL akaekimya.
Kanuni za asili (natural justice) hazipo hivyo.
Ni dhahiri, uropokaji waousema watuhumu wake ni ili kumtaka akae kimya anapotuhumiwa
Wasira na Mkutano Mkuu wa CCM
Mzee Wasira (80) amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara.
Katika hotuba ya kushukuru, Mzee alizungumzia suala la maridhiano akisema CCM itaendelea nayo, na kwamba maridhiano si mtu mmoja, kuna yanayohusu jamii kama viongozi wa dini n.k.
Hoja: Mzee Wasira ameongelea maridhiano makusudi kabisa.
Kwanza, kujibu hoja za wanaosema maridhiano yalikuwa Utapeli na hasa kambi ya TAL.
Pili, Mzee anachomeka maridhiano katika kumtetea muasisi wa Maridhiano Mh FAM.
Mzee Wasira anaposema 'si mtu mmoja' ana maanisha maridhiano si baina ya CCM na TAL ambaye amekuwa mwiba mkali bali CCM na Taasisi
Hoja ya maridhiano imechomekwa makusudi kuonyesha CCM ina dhamira na mtu anayeweza kuwa mshirika ni FAM. Kwa kujua au kutojua Mzee Wasira atakuwa ameshadidia hoja ya TEAM TAL kwamba CCM wanamtaka FAM kwasababu wana mmudu.
Huu ulikuwa mkakati mbaya sana wa Mzee Wasira, hakusoma mazingira.
1. Mbowe (FAM) na Huruma
Kampeni zimeendelea kwa kasi kwa kutumia vyombo vya habari. Tumeeleza awali, hata vyombo ''mahasimu' hutoa nafasi (air time) kwa Wagombea wa CDM! kinyume kabisa na taratibu zao!!!
FAM akihojiwa alisema kwa hisia sana kuhusu fadhila zake kwa Wapinzania wake akiwemo Mh G Lema.
Kwa nadra sana, akihojiwa ,FAM alisema akichaguliwa ataweka kipindi cha uchaguzi cha miaka 3 ili kuwiana na chaguzi za Serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu.
Hoja: Tulieleza Team FAM wanatafuta huruma kwa kueleza nini waliwafanyia wapinzania wao na si nini watafanyia Chama. Tulionya Team TAL wakiingia katika malumbano hayo watapoteza.
Katika hali ya kushangaza Team TAL wameingia katika malumbano ya fadhila wakitekeleza hoja zao za nini wanataraji kufanya wakipewa uongozi. Katika hili, Team FAM imewavuta wakaingia 18.
Hoja ya vipindi 3 iliyotolewa na FAM haina mashiko. Miaka 5 ingeweza kupangwa kwa kuangalia kalenda za chaguzi za Kitaifa. Swali, ni kwanini kwa miaka 21 FAM hakuweza kuliona hili au kulifanyia kazi?
Uongozi wa miaka 3 haumpi nafasi kiongozi kutekeleza azma na ahadi au mipango yake Kichama
2. Tundu Lissu (TAL) na Urpokaji
Kuna tuhuma kutoka Team FAM kwamba TAL ni mropokaji, wakiitumia kumdhalilisha au kumdunisha.
Hoja: Kuropoka kwa maana ya kiswahili kunaweza kuwa na maana mbili
Kwanza, kuongea jambo bila ithbati au uhakika. Ni aina ya uzushi unaojengwa bila mantiki
Pili, kuropoka ni kutoa maneno yaliyokuwa siri kwa kudhamiria au kwa bahati kutoka
TAL anapotoa hoja mara zote zinajengwa kwa mantiki na hutoa hadi chanzo.
Mfano, alibanwa aeleze ushahidi wa kuhongwa pesa. TAL alijibu, aliyetoa habari hizo ni Marehemu.
TAL akaendelea kusema ikiwa ni uzushi itolewe video inayoonyesha aliomba radhi.
Kwa tafsri, TAL anakuwa mropokaji kwa hoja ya pili hapo juu, kwamba anatoa habari ambazo zilitakiwa ziwe siri. Inaweza kuwa kweli lakini je wanaomtuhumu huzingatia ukweli kwamba TAL anahitaji kujitetea?
TAL anapojitetea huambiwa ni Mropokaji, anazungumza yasiyotakiwa kuzungumzwa.
Wanaomtuhumu hawafikirii gharama za tuhuma, na wangependa TAL akaekimya.
Kanuni za asili (natural justice) hazipo hivyo.
Ni dhahiri, uropokaji waousema watuhumu wake ni ili kumtaka akae kimya anapotuhumiwa
Wasira na Mkutano Mkuu wa CCM
Mzee Wasira (80) amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara.
Katika hotuba ya kushukuru, Mzee alizungumzia suala la maridhiano akisema CCM itaendelea nayo, na kwamba maridhiano si mtu mmoja, kuna yanayohusu jamii kama viongozi wa dini n.k.
Hoja: Mzee Wasira ameongelea maridhiano makusudi kabisa.
Kwanza, kujibu hoja za wanaosema maridhiano yalikuwa Utapeli na hasa kambi ya TAL.
Pili, Mzee anachomeka maridhiano katika kumtetea muasisi wa Maridhiano Mh FAM.
Mzee Wasira anaposema 'si mtu mmoja' ana maanisha maridhiano si baina ya CCM na TAL ambaye amekuwa mwiba mkali bali CCM na Taasisi
Hoja ya maridhiano imechomekwa makusudi kuonyesha CCM ina dhamira na mtu anayeweza kuwa mshirika ni FAM. Kwa kujua au kutojua Mzee Wasira atakuwa ameshadidia hoja ya TEAM TAL kwamba CCM wanamtaka FAM kwasababu wana mmudu.
Huu ulikuwa mkakati mbaya sana wa Mzee Wasira, hakusoma mazingira.