CHADEMA na Sauti ya Watanzania, msikaribishe tena watu waoga waoga kwenye mikutano yenu

CHADEMA na Sauti ya Watanzania, msikaribishe tena watu waoga waoga kwenye mikutano yenu

Burkinabe

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2023
Posts
2,354
Reaction score
4,024
Jana Jumapili ya tarehe 23/07/2023, CHADEMA na SAUTI YA WATANZANIA, walikuwa na mkutano mkubwa sana juu ya kupinga uuzwaji/ubinafsishaji wa Bandari za Tanzania.

Mimi kama mmoja ya wahudhuriaji wa mkutano huo, nilifurahia sana jinsi mkutano ulivyoratibiwa kwa umakini wa hali ya juu.

Kilichonisikitisha ni baadhi ya waalikwa ambao walipata nafasi ya kuhutubia mkutano huo, kwanza walionekana ni waoga, wasiojiamini na nasikitika kusema walitumia muda wa mkutano vibaya kwa kuongea maneno ya kuwatisha wazungumzaji wengine.

Yule Mzee Luhigo pamoja na Bw. Thomas, binafsi waliniboa sana pamoja na wahudhuriaji wengine, maana walijitanabaisha kujipendekeza kwa Rais na kuwatisha wazungumzaji wengine jasiri kama Wakili Msomi Mwabukusi na wale Maaskofu wote waliokuwepo, ambao tunamshukuru Mungu kwa kuwa hawakuogopa kusema kile walikusudia kusema licha ya maneno ya "vibaraka" hao waliokuwa na nia ovu.

Nimalizie kwa kusema, Maandiko Matakatifu katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 20:8 yanasema; Mwenye HOFU (mwoga) na MNYONGE hakutakiwa kwenda vitani asije akaiyeyusha mioyo ya wenzake! (akawaambukiza woga wengine). Uoga unaambukiza kama ukoma!

Tafadhalini sana Chadema na Sauti ya Watanzania, tunaomba kabla ya kuwaalika watu watakaokuja kutuhamasisha kwenye mikutano yenu ya huko mbeleni, ikiwezekana muwasikilize kwanza au kupitia hotuba zao kabla ya kuwapandisha majukwaani. Na endapo wakileta ujinga na ushenzi jukwaani, msiwaonee aibu kama mlivyofanya kwa sehemu jana. Mabadiliko hayawezi kuja kwa kuoneana aibu kwa wapumbavu wachache wanaoturudisha nyuma.

Vinginevyo, siku ya jana mmefanya jambo kubwa sana litakalokumbukwa na historia pamoja na vizazi vyetu vyote.

Hatutakubali Bandari na Raslimali zingine za Taifa letu, kuhodhiwa kwa manufaa ya watu wa wachache, bali zitumike kwa ajili ya faida ya Watanzania wote.

Aluta continua.
 
Mtu mwenye akili timamu, hawezi kuhudhuria mikutano ya MACHADEMA majinga yaliyosheheni udini mtupu, mkutano umejaa maaskofu, sasa huo ni mkutano au wanajumuia?
 
Jana ndo ilikuwa kifo cha swala la DP world ila ajabu imekuwa tofauti. Serikali iliruhusu mkutano ufanyike kuona watajitokeza wangapi, ishapata picha kuwa wananchi hawana shida na DPW
 
Jana ndo ilikuwa kifo cha swala la DP world ila ajabu imekuwa tofauti. Serikali iliruhusu mkutano ufanyike kuona watajitokeza wangapi, ishapata picha kuwa wananchi hawana shida na DPW
mkutano ulidoda?
 
Usichokielewa ni, hao maaskofu ule ni mkutano wao, waliwakodisha chadema kujificha ndani ya pazia la siasa.

Waliolipia gharama zote za mkutano ni kina bashiru na genge lake. Na haohao ndiyo kwanza sasa hivi wana genge la nshomile, nshomile walikuwa wanafaidika sana na bandari kwa kushirikiana na kanisa.

Usinisemeshe mengi.
 
Mtu mwenye akili timamu, hawezi kuhudhuria mikutano ya MACHADEMA majinga yaliyosheheni udini mtupu, mkutano umejaa maaskofu, sasa huo ni mkutano au wanajumuia!!?
Hahaha jana Chadema na Sauti wameonesha umwamba na ukawa kweli kweli
 
Jana ndo ilikuwa kifo cha swala la DP world ila ajabu imekuwa tofauti. Serikali iliruhusu mkutano ufanyike kuona watajitokeza wangapi, ishapata picha kuwa wananchi hawana shida na DPW
Kumbe nikajuaga wewe ni mpiga maji muda wote lakini kumbe wakati mwingine unakuwa Timamu
 
Mtu mwenye akili timamu, hawezi kuhudhuria mikutano ya MACHADEMA majinga yaliyosheheni udini mtupu, mkutano umejaa maaskofu, sasa huo ni mkutano au wanajumuia!!?
Sasa kama Mashehe walirushiwa nao wakatishika, wangewafanyaje?
Lakini bora wao, hawakufika kabisa, kuliko wangefika halafu watuletee mambo ya hovyo kama ya hao ndugu niliowataja.
 
Usichokielewa ni, hao maaskofu ule ni mkutano wao, waliwakodisha chadema kujificha ndani ya pazia la siasa.

Waliolipia gharama zote za mkutano ni kina bashiru na genge lake. Na haohao ndiyo kwanza sasa hivi wana genge la nshomile, nshomile walikuwa wanafaidika sana na bandari kwa kushirikiana na kanisa.

Usinisemeshe mengi.
Bibi hivi wewe huwezagi kuchangia mada pasipo kuchanganya na udini?!
 
Bora hao walijitokeza. Wengine waliomba kuto kuwepo kabisa.(unafiki na uoga wa kiwango cha juu kabisa)
Halafu wanatuhubiri kutokuwa na hofu na kifo wakati wao wenyewe waoga kupitiliza.
Kiongozi mahili hupatikana wakati wenye changamoto.
 
Back
Top Bottom