Uchaguzi 2020 CHADEMA na Tundu Lissu wamekuja na mwarobaini wa tatizo la mfumo wetu wa elimu

Uchaguzi 2020 CHADEMA na Tundu Lissu wamekuja na mwarobaini wa tatizo la mfumo wetu wa elimu

Mangisandy

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
2,652
Reaction score
2,273
Nimepokea kwa mikono miwili sera ya CHADEMA, hasa kuhusu mfumo elimu.

Sera yetu ya elimu na mfumo huu wa elimu siyo mzuri. Tuna mfumo wa elimu ambao umejikita kwenye kukariri ili kujiandaa na mitiani ya mwisho. Lengo ni kupata cheti cha ufaulu wa mitiani, na hatimaye kuajiriwa.

Kuna matatizo kadha yanayo tengenezwa na mfumo huu wa elimu:

Kwanza, mfumo huu haumpi mwanafunzi uwezo wa ubunifu, kujenga hoja binafsi, zaidi ya kukariri alicho elekezwa na mwalimu!

Pili, mwanafunzi hapati maarifa yalikusudiwa.

Tatu, mfumo huu unajenga mianya ya rushwa, siyo tu kufaulu mitiani yenyewe, lakini ndiko tabia za rushwa na ufisadi zinakozaliwa.

Mfumo huu wa elimu siyo shirikishi, kwa sababu mwanafunzi hapati nafasi za kushiriki darasa kwa kuchangia au kuuliza maswali. Ni mfumo wa “ndiyo mzee”, ambapo mwalimu ni ‘I know it all, na wanafunzi ni ‘you know nothing’! Hapa ukijumlisha na dhana ya ‘mkubwa hakoseagi’, unapata taifa la watu wasikosowa na kutopenda kukosolewa hata kama unakosea.

Matatizo hayo ya mfumo wetu wa elimu na pia uelewa mdogo wa lugha za kimataifa, ni kikwazo kikubwa cha soko la ajira ndani na nje ya nchi, hasa wakati huu wa utandawazi.

Asante sana Tundu Lissu na CHADEMA kwa utayari na uthubutu wenu wa ku-challenge mfumo wetu wa elimu. Nategemea kwamba sera yenu hii itakuja kutekelezwa kwa kuufumia kabisa mfumo wetu wa elimu, ili kujenga taifa lenye elimu bora, katika kutekeleleza kaulimbiu yenu ya Uhuru, Haki na Maendeleo ya watu.

Mungu ibariki Tanzania , Mungu ibariki CHADEMA, Mungu mmbariki Tundu Lissu!
 
Kaka na mwarobaini kwahiyo tujiandae kupiga nyungu? Alete na mishana na shuntama tupige nyungu sawasawa, mkuu elimu sio korona
 
Kwa hili namuunga mkono kwa asilimia zote!!

Mfumo wa elimu tunaouhitaji ni wa kuwawezesha watu kuwa na practical skills kwa kiasi kikubwa!

Hatuhitaji elimu za mkwawa alifia bwawa gani, sijui mzungu wa kwanza anaitwa nani!! Elimu ya kipumbavu sana!

Fumua kabisa huu ugonjwa wote wa akina ndalichako!
 
Hii mifumo ya elimu iko kidunia, huo mfumo yeye anautoa wapi? Umefanikiwa majaribio wapi? Nani kamwambia majirani wako vizuri kuliko wabongo?

Lissu hebu nenda Congo Mali Bulgaria uone mining experts wakitanzania wanavyoheshimika, one of the best pilots wa emirates Ni miraj kikwete, nenda world bank utamkuta Miriam Salim, nenda who utakutana na Dr Mwale, wote Hawa wameanza shule humuhumu, hao mbumbu Ni wapi?
 
Akifumua anaweka nini?
Mifumo huwa haifumuliwi bali huboreshwa taratibu ili kuzuia kukwamisha mifumo mingine.
Mfano, ukifumua 7,4,2,4 ziwe na mchefuo wa kujitegemea , utakosa walimu.
Itakubidi ufundishe miongo kadhaa kupata walimu.
Ndio, ni kweli kabisa, lazima uje na mfumo mbadala, ambao ni shirikishi unaolenga kujenga ubunifu na ujuzi! Na pia siyo kazi ya siku moja, wala ya mtu mmoja! Tunacho[SUP] shukuru ni kwamba tayari kuna wazo na baada ya October 28, mchakato wa kulitekeleza utaanza.[/SUP]
 
Kwa hili namuunga mkono kwa asilimia zote!!

Mfumo wa elimu tunaouhitaji ni wa kuwawezesha watu kuwa na practical skills kwa kiasi kikubwa!

Hatuhitaji elimu za mkwawa alifia bwawa gani, sijui mzungu wa kwanza anaitwa nani!! Elimu ya kipumbavu sana!

Fumua kabisa huu ugonjwa wote wa akina ndalichako!
Kwetu Kuna elimu inaitwa kuhanwa na kuhembekwa, kuhanwa unafundishwa kuroga watu na kuhembekwa unafundishwa kupiga ramli, hapa Ni practical mwanzo mwisho
 
Kwetu Kuna elimu inaitwa kuhanwa na kuhembekwa, kuhanwa unafundishwa kuroga watu na kuhembekwa unafundishwa kupiga ramli, hapa Ni practical mwanzo mwisho
Hiyo baki nayo wewe na mama ako mrogane huko chumbani mpeane na uroda.

Nazungumza kuhusu mustakabali wa elimu ya nchi na kizazi tunachokizaa.
 
Hii mifumo ya elimu iko kidunia, huo mfumo yeye anautoa wapi? Umefanikiwa majaribio wapi? Nani kamwambia majirani wako vizuri kuliko wabongo?

Lissu hebu nenda Congo Mali Bulgaria uone mining experts wakitanzania wanavyoheshimika, one of the best pilots wa emirates Ni miraj kikwete, nenda world bank utamkuta Miriam Salim, nenda who utakutana na Dr Mwale, wote Hawa wameanza shule humuhumu, hao mbumbu Ni wapi?
Na unakuta wote hao wamesomea nnjeya nchi,ndo maana chadema wanasema badala ya sisi kwenda kutafuta elimu nnje basi hii yetu iboreshwe ifikie viwangi kama hivyo vya nnje. Au wewe bado mzito hujaelewa?
 
Nimepokea kwa mikono miwili sera ya CHADEMA, hasa kuhusu mfumo elimu.


Sera yetu ya elimu na mfumo huu wa elimu siyo mzuri. Tuna mfumo wa elimu ambao umejikita kwenye kukariri ili kujiandaa na mitiani ya mwisho. Lengo ni kupata cheti cha ufaulu wa mitiani, na hatimaye kuajiriwa.


Kuna matatizo kadha yanayo tengenezwa na mfumo huu wa elimu:


Kwanza, mfumo huu haumpi mwanafunzi uwezo wa ubunifu, kujenga hoja binafsi, zaidi ya kukariri alicho elekezwa na mwalimu!


Pili, mwanafunzi hapati maarifa yalikusudiwa.


Tatu, mfumo huu unajenga mianya ya rushwa, siyo tu kufaulu mitiani yenyewe, lakini ndiko tabia za rushwa na ufisadi zinakozaliwa.


Mfumo huu wa elimu siyo shirikishi, kwa sababu mwanafunzi hapati nafasi za kushiriki darasa kwa kuchangia au kuuliza maswali. Ni mfumo wa “ndiyo mzee”, ambapo mwalimu ni ‘I know it all, na wanafunzi ni ‘you know nothing’! Hapa ukijumlisha na dhana ya ‘mkubwa hakoseagi’, unapata taifa la watu wasikosowa na kutopenda kukosolewa hata kama unakosea.


Matatizo hayo ya mfumo wetu wa elimu na pia uelewa mdogo wa lugha za kimataifa, ni kikwazo kikubwa cha soko la ajira ndani na nje ya nchi, hasa wakati huu wa utandawazi.


Asante sana Tundu Lissu na CHADEMA kwa utayari na uthubutu wenu wa ku-challenge mfumo wetu wa elimu. Nategemea kwamba sera yenu hii itakuja kutekelezwa kwa kuufumia kabisa mfumo wetu wa elimu, ili kujenga taifa lenye elimu bora, katika kutekeleleza kaulimbiu yenu ya Uhuru, Haki na Maendeleo ya watu.


Mungu ibariki Tanzania , Mungu ibariki CHADEMA, Mungu mmbariki Tundu Lisu!
Naunga mkono hoja . Elimu yetu inahitaji kufumuliwa upya kabisa.Tumezalisha watu ambao hawawezi ku compete hata kwenye jumuiya ya Africa Mashariki tu!!

Hongereni Chadema kwa kuleta hili.
 
Akifumua anaweka nini?
Mifumo huwa haifumuliwi bali huboreshwa taratibu ili kuzuia kukwamisha mifumo mingine.
Mfano, ukifumua 7,4,2,4 ziwe na mchefuo wa kujitegemea , utakosa walimu.
Itakubidi ufundishe miongo kadhaa kupata walimu.
ni kufumua tu mengine yatajikoki mbele tutaadjust kwenda na mazingira mbele ya kwa mbele mambo ya kuzeekea shule ni upumbafu hakuna unachotoka na nacho kuna sababu gan ya kusoma miaka zaidi ya 20
 
Back
Top Bottom