CHADEMA na Udikteta Makao Makuu

CHADEMA na Udikteta Makao Makuu

Mimi nilifikiri kuna madai mapya ? Haya ya ukabila mbona yamesha ongelewa sana hapa .Matumizi ya mchine kila siku yanasemwa .Kwa ni ni wabunge wametoka upande mmoja ni sababu ya wazi kabisa na zimesha semwa .Labda kw auchache kama pesa kutofika mikaoni hili laweza kuwa jambo lakini mengine mwandishi yuko katika kampeni ambazo zilisha feli kabla ya kuanza .Ukabila Chadema wala mie siuoni labda kwa kuwa mimi si mwenzao .
asante kwa kwa ufafanuzi huu mkuu...yote yalishasemwa mengine ni marudio tu na siasa za maji taka.
 
Yusuphu Halimoja alikuwa anatumiwa na watu walio karibu na mafisadi ili kuibomoea CHADEMA lakini tutasimama Daima kusema ukweli hadi pale uhuru wa kweli na mabadiliko ya kweli yatakapopatina na tazama pia hata miendo ya vyombo vya habari vya hivi karibu vilikuja kubadilika kuwa na kuwasakama Makamanda wa CHADEMa walikuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi
 
Mzee Halimoja alikuwa recruit wa Chacha Wangwe aliyetaka uwenyekiti taifa kwa mbinu. Ajali ya gari ilimpata Chacha Wangwe (Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi) kabla ya kukivuruga mno Chadema.

Hakuna udikteta Chadema, Makao Makuu. Waulize wachapa kazi wa Makao Makuu kama Suzan Lyimo, John Mnyika, Suzan Kiwanga na Halima Mdee wathibitishe.
 
Ama Kweli CHADEMA ni Chama Cha KIKRISTO, hakina viongozi kabisa wa Kiislamu hii ni hatari sana Chama Cha Siasa Kuendeshwa namna hii ni Ubaguzi Uliokithiri na Usiokuwa na Maana yeyote na ndio Maana CHADEMA inawapa Vigumu Kuunga Mkono Hoja ya KADHI Kwa sababu sio Mtazamo wao.
 
Ni ngumu sana maana suala hilo sio agenda yetu sisi Chadema Itakuwa ngumu sana kuwa ajili ya kusemea mambo ya watu binafsi kama haya, tutakuja kusema mambo ya taifa na uozo wa Taifa hili sio masuala ya watu binafsi kama haya bwana mzee
 
Ama Kweli CHADEMA ni Chama Cha KIKRISTO, hakina viongozi kabisa wa Kiislamu hii ni hatari sana Chama Cha Siasa Kuendeshwa namna hii ni Ubaguzi Uliokithiri na Usiokuwa na Maana yeyote na ndio Maana CHADEMA inawapa Vigumu Kuunga Mkono Hoja ya KADHI Kwa sababu sio Mtazamo wao.

CCM pia chama cha waislamu viongozi wote wa juu ni waislamu,madiwani wengi na wenyeviti wa serikali za mitaa na viongozi wa nyumba kumi, pia viongozi wote wa jumuiya zake,vijana,wanawake,wazazi/wazee wote waislamu lakini ukweli sasa hivi wananchi wameamka hawadanganywi na propaganda tena za udini wanajua nia yenu ,mumechelewa sana wanajali zaidi utaifa Tanzania kwanza propaganda peleka china sio nchi hii hamtaturudisha nyuma kamwe nia yenu kutaka kuvuruga nchi,nchi inaenda ovyoovyo kwa sababu ya watu kama nyie
 
Ama Kweli CHADEMA ni Chama Cha KIKRISTO, hakina viongozi kabisa wa Kiislamu hii ni hatari sana Chama Cha Siasa Kuendeshwa namna hii ni Ubaguzi Uliokithiri na Usiokuwa na Maana yeyote na ndio Maana CHADEMA inawapa Vigumu Kuunga Mkono Hoja ya KADHI Kwa sababu sio Mtazamo wao.

Acha Umbeya Mkuu! Kwani CHADEMA ni lazima iunge mkono hoja ya Kadhi? Ni vyama gani vingine vilivyounga Mkono hiyo hoja!

CHADEMA ina viongozi waislamu mfano ni ZITTO
 
siku Bob ameamka na jinamizi lenye hasira utamjua tu!
Tutasimama Imara kupinga uozo wa taifa hili Daima japo hata watu wabaya nao wanaongezeka, hivyo na hata huyu naye ni miongoni nao, wakati huu tutaona mengi hata zile makala zake kwenye gazeti la Jumapili kuhusu CHADEMa tunajua kuwa hawezi fika mbali, sisi kama wanachama na wajumbe waaminifu kwa CHadema tutasimama Imara ili taifa letu likombolewe tuka mikononi wa watu wabaya hata kuna baadhi ya magazeti mapya yanakuja na utamaduni huu. Tupo Imara na watu wapo imara daima
 
Tutasimama Imara kupinga uozo wa taifa hili Daima japo hata watu wabaya nao wanaongezeka, hivyo na hata huyu naye ni miongoni nao, wakati huu tutaona mengi hata zile makala zake kwenye gazeti la Jumapili kuhusu CHADEMa tunajua kuwa hawezi fika mbali, sisi kama wanachama na wajumbe waaminifu kwa CHadema tutasimama Imara ili taifa letu likombolewe tuka mikononi wa watu wabaya hata kuna baadhi ya magazeti mapya yanakuja na utamaduni huu. Tupo Imara na watu wapo imara daima
Hapana. Nitakupinga vikali hapo. Bob si mtu mbaya, la hasha. He's one of the few true patriotic troupers JF has ever had!! Naomba utumie muda kusoma michango yake mingine mingi hapa jamvini.


SteveD.
 
Hapana. Nitakupinga vikali hapo. Bob si mtu mbaya, la hasha. He's one of a few true patriotic troupers JF has ever had!! Naomba utumie muda kusoma michango yake mingine mingi hapa jamvini.


SteveD.

Malalamiko ya ubabe na wizi wa ccm kutoka kwa mashabiki wale ,huwa siyaamini kwa sababu niyingiiiii sana tena sanaaa
 
Unayesema Chadema haina Waislamu hukijui chama hicho. Wako wengi.

Zitto Kabwe Zubeiri ambaye ni Naibu Katibu Mkuu ni Muislamu. Bob Nyanga Makani aliyekuwa Mwenyekiti (Taifa) kabla ya Freeman Mbowe ni Muislamu. Mhe. Arfi (Mbunge wa Mpanda Magharibi), Mhe. Halima Mdee, Mhe Mhonga Said (Wabunge Viti Maalum) ni Waislamu. Aliyekuwa Katibu Mkuu kabla ya Mhe. Slaa, WAlid Kaburou na former Naibu Katibu Mkuu Akwilombe ambao wametoka Chadema ni Waislamu.

Wajumbe wengi wa Kamati Kuu ya Chadema k.m. Mzee Kasisiko wa Kigoma, Chiku Abwao wa Iringa ni Waislamu. Wajumbe wote wa Kamati Kuu toka Zanzibar ni Waislamu. Huo Ukristo mtupu Chadema uko wapi????????

Kuhusu msimamo wa Chadema re. suala la Mahakama ya Kadhi, hili ni jambo linalohusu Ibada. Hata Mufti amefafanua hivyo. CCM ilikurupuka mwaka 2005 ikaliweka kwenye Ilani ya Uchaguzi kinyume na Sheria ya Vyama vya Siasa na Katiba ya Tanzania, Ibara Na. 19(2). Hii ilikuwa ni janja janja ya CCM ya kuvutia kura za waumini ambao hawafahamu Katiba kwa kina.

Chadema hawawezi kudai kuweka sheria za dini ktk Sheria za Nchi. Zikiwekwa za Kiislamu, Wakristo nao watadai Canon Law iingizwe, wenye kuamini dini ya Kiyahudi watataka Torat na sijui sisi Wapagani tutaingiza sheria gani.

Endapo viongozi wa Kiislamu Tz. watafuata ushauri wa wanazuoni wengi kwamba waunde Mahakama ya Kadhi kama chombo chao chini ya Sheria ya Taasisi Zisizo za Kiserikali (Non-Governmental Organizations), na wakakigharimia kwa fedha za zaka na michango ya wafadhili wengine wa ndani na nje, naamini uongozi wa Chadema hautapinga. Huo ndio utatuzi wa suala ambalo linaweza kuleta mgawanyiko wa kidini Tanzania ambao si lazima.
 
Mkuu Kilasara umetoa maelezo mazuri hasa kwa wenye wasiwasi wa kidini. Ushauri wangu kwa chadema ni ufanyike uchaguzi wa viongozi wa chama mapema kabla 2010. Chaguzi zinachangamoto zake, ni vema kupata viongozi mapema ili wajipange lakini pia, kuponya madonda yatakayo tokea wakati wa uchaguzi.
 
Wanaendesha chama chao bila kufuata misingi ya katiba ya chama chao.

Hawana utaratibu mzuri wa kuonyesha kuwa chama chao ni mali ya umma hivyo kitatoka mikononi mwa familia ya Mbowe.

Kwa udikteta walionao kama wakipewa nchi yatatokea mambo mabaya sana hapa Tanzania.
 
Njaa alikosa uteuzi kwa msukuma mwenzake ajabu ni kwamba Sasa anatafuta uteuzi kwa mkojani. Mpeni pole.
 
Mbona na yule hayati wako naye hakuwa dikteta tu! Alikuwa ni dikteta uchwara! Ilikuwaje akapewa nchi?
 
Back
Top Bottom