Huku kwetu kuliko ungua shoka mpini ukabaki; Bukama Batoko tafsiri yake sikwambii leo wala kesho! bali itoshe tu kukushauri kwamba "Jiunge na timu ya washindi" kabla hakujakucha!! Fikra za CDM ndio fikra za wakati uliopo; going forward;
Ukiona kila mtia nia wa CCM anatangaza nia kwa kutaka kuijenga upya Tanzania! salaaale! kwani tumepata uhuru leo?! eti kupambana na rushwa na ufisadi; Aaastagafilulahi! rushwa na ufisadi vimetoka wapi wakati wao ndio wako madarakani? na hao mafisadi, wala rushwa na majangili ni kina nani!? Eti kuimarisha amani na mshikamano, kumbe vimetikisika under their watch?! eti kujenga uchumi wa viwanda; afanaleki! viwanda alivyoacha mwalimu vimekwenda wapi na wao ndio watawala!?; au kuna Tsunami ilipita vikatumbukia kweusi?! Eti kudumisha muungano; kwani hizo nyufa na kero hawazioni au ndio kesi ya "Funika kombe mwanaharamu apite?!!
Hata hivyo; pole sana Bukama Batoko; kwa CV hii hapa chini wewe bado ni wa "Chandimu" kule mchangani; kwa ligu kuu hujapevuka; tulia ukikua utaelewa! au jiunge na ACT; alliance for cowards and traitors watoto wenzio!
Join Date: 27th April 2015
Posts: 157
Rep Power: 338
Likes Received: 22
Likes Given: 14
text color mine and deliberate!!