CHADEMA ni Moja, Wanaotaka kufukuza wenzao wadhibitiwe haraka

Nani wa kumzuia Mrema kuingea wewe? Mrema akiongea ataishia kujibiwa na Msigwa, hakuna kiongozi wa CHADEMA mwenye huo muda wa kumzuia huyo
 
Naunga mkono hoja!
Lissu akumbuke ameshinda kwa ushindi mwembamba sana!
Litakuwa ni kosa kubwa kuwapuuza waliokuwa wafuasi wa Mbowe.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA @ChademaTz wa Kata ya Segerea mkoani Dar es Salaam, Kitomary Steven, amekanusha vikali madai yaliyoenezwa mtandaoni kwamba amepanga kumvua uanachama John Mrema @JonMrema , Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA.


Akizungumza na Jambo TV, Kitomary ameeleza kuwa taarifa hizo ni za uongo na hazina msingi wowote.


“Ninaomba nikanushe taarifa hizo, taarifa hizo ni ghushi. Kwanza kabisa, mimi ni Mwenyekiti wa CHADEMA wa Kata ya Segerea, huku Mrema akiwa ni mkazi wa Kata ya Bonyokwa na Mkurugenzi wetu wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, ambaye tunamheshimu sana,” amesema Kitomary.


Ameendelea kueleza kuwa haikubaliki kisheria wala kimantiki kwa ngazi ya tawi kufikia maamuzi ya kumvua uanachama Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, ambaye pia ni sehemu ya Sekretarieti ya Makao Makuu.


Awali, John Mrema alitoa madai kupitia ukurasa wake wa X kwamba viongozi wa CHADEMA, akiwemo Kitomary, walikuwa wakipanga kumvua uanachama kabla ya mkutano wake na waandishi wa habari uliotarajiwa kufanyika hivi karibuni.


Katika ujumbe wake, Mrema aliandika: "Nimejulishwa na mwenyekiti wa tawi langu, ameagizwa anifute uanachama kabla ya kesho ili kama nitaendelea na nia yangu ya kuzungumza na vyombo vya habari basi niwe sio mwanachama!”,


Mrema aliongeza kuwa juhudi za kumvua uanachama ni sehemu ya juhudi za kuzima maoni huru na uhuru wa kujieleza ndani ya chama.


Kitomary amefafanua kuwa Mrema alichapisha ujumbe wa kuashiria kuwa angefanya mkutano na waandishi wa habari, ambapo Kitomary alijibu ‘tweet’ hiyo kwa kumweleza kuwa mkutano huo utafuatiliwa kwa ukaribu.
 
Kwa mara ya kwanza umeongea lugha ya ukali sana Toka nimekujua humu jf, umejificha ficha hatimae umejaa kwenye mfumo😂 kumbe wewe "ulikua timu mwamba"

Mimi naamini chadema ya uongozi mpya haitakuwa ya namna hiyo, nadhani pengine Kuna namna mrema anataka kutengeneza mazingira ionekane kwamba viongozi walioingia madarakani ni watu wa kubana uhuru wa kuongea ndani ya chama.
Hakuna atakae mfuta uanachama mrema kwa sababu ya kupishana misimamo na viongozi wapya hiyo ni hofu yake tu. Chadema ni ya wote uongozi mpya sidhani kama utaruhusu uhuni wa namna hiyo(kama upo kweli)
 
Tathimini ili iweje kwa vyombo vya habari na itamsaidia nani, tathimini kwa vyombo vya habari ? nadhani itakuwa ya kujisafisha?

Nahiyo tathimini kama ni ya kujenga chama kwanini hakuiwakilishwa kwenye kamati kuu
 
waliofiji sahihi ya mnyika na kuingia covid 19 watafute chama chama chao na sivinginevyo

Sawa Mrs mbowe
 
Usiwaze kamanda hizo ni figisu plan F Za chama chawala.. Baada ya plan A,B, C, D kufeli 😂
 
Mkuu
Kwa upande wako bado upo kwenye kampeni za uchaguzi?

Hofu ya John Mrema ni kubwa? Mmewasiliana na Kitomari kabla ya kuja mtandaoni?
 
Huyu ni John mwenyewe amekasirika hadi amepitiliza na ku blow cover yake mwenyewe.
 
Ushindi wa kura tatu kama tofauti si ushindi kwa mantiki ipi, hata ingekuwa robo kiduchu ni ushindi tu
 
Hujui lolote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…