CHADEMA: Tanzania itakombolewa na wenye Moyo

CHADEMA: Tanzania itakombolewa na wenye Moyo

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Siyo siri kuwa hii nchi ni ngumu sana. Uwekezaji uliopo dhidi ya haki na usawa ni mkubwa sana.

Kwa makusudi demokrasia na uhuru wa watu vimeminywa vilivyo ili kufanikisha hayo.

Hali hii haitaondoka yenyewe bila ya makabiliano. Ni muhimu kufahamu watesi wetu hujipanga upya kwa kila hatua tunazochukua.

Iwe wanapanga kusuka au kunyoa hiyo na ikawe shauri yao.

Muhimu kwetu ni kujua wazi wazi tunakwama wapi na hali iwe hivi hadi lini:

1. Harakati za kudai katiba mpya kupoa baada ya Aboubakar kukamatwa.
2. Kuweka matumaini yoyote chanya kutokea kwenye kesi za ngedere hakimu akiwa nyani.
3. Kutokuwa na mikakati ya wazi kuhusiana na kuwahami wahanga wetu katika mapambano.
4. Kutokuhakikisha chaguzi zinakoma kama hakuna tume huru. Kususia peke yake hakutoshi.
5. Kutokuiangazia nguvu yetu ya kuyajaza magereza yao kama sera halali na mbadala dhidi ya matumizi yao batili ya nguvu.

Makamanda uelekeo uwe zaidi kutoka mitandaoni. Lissu, Lema, na makamanda wote tukutane Tahrir tuna hisani ya kuifanyia nchi hii.

Tanzania itakombolewa na wenye moyo.
 
Bongo mambo mengi
heart_beating_0.gif
 
Kama hutaki kutembea na tumaini basi ni vigumu kupiga hatua yoyote chanya sio kwenye siasa zetu pekee, bali kwenye maisha kwa ujumla.

Suala la jaji kwenye kesi ya Mbowe kwa mfano, hilo halihitaji hofu sababu wao ndio wateuzi, kilichopo muhimu sheria ifuatwe, na hicho ndicho kinachopiganiwa. Lakini ukianza kumuogopa jaji na kesi ndio tayari iko mahakamani utakimbilia wapi kwingine?

Rilaxx bro, mapambano yoyote lazima yawe na turning point, na kwako nimeona umeiweka mitandaoni, lakini lazima ijulikane njia ya kuihamisha toka mitandaoni kuyaleta field, vinginevyo yakibaki mitandaoni yatakuwa ni sawa na kelele tu.

Kusema kweli polisi kwa kushirikiana na CCM wamejipanga kuipoteza Chadema, hawataki kabisa viongozi na wanachama wake wafanye chochote, tunapoelekea hata wakicheka watakamatwa, muhimu ni kuendelea na mapambano huku ikitafutwa njia mbadala.

Mfano, ile jogging ya Bawacha iwepo, waache kuvaa zile t-shirt zinazowakera CCM ( nasema CCM makusudi coz polisi ni tawi lao).

Naamini uwepo wao kwa pamoja utaamsha hari kati yao, utawaamsha watanzania wengine kujiunga nao, na utaamsha hisia za Katiba Mpya, hivyo wakati utakapofika wa kuyaunganisha makundi mengine, kazi itakuwa rahisi lengo litafikiwa kwasababu wote watakuwa na mawazo yanayofanana.

- Mikakati ya kuwahami wahanga ipo, tatizo naloliona ni upatikanaji wa resources, mpaka michango ipitishwe ndio lengo litimie, hapa siwezi kuwalaumu Chadema coz tangu utawala uliopita walibanwa kiuchumi, hakuna ruzuku, binafsi naona wanajitahidi sana.
 
Kama hutaki kutembea na tumaini basi ni vigumu kupiga hatua yoyote chanya sio kwenye siasa zetu pekee, bali kwenye maisha kwa ujumla.

Suala la jaji kwenye kesi ya Mbowe kwa mfano, hilo halihitaji hofu sababu wao ndio wateuzi, kilichopo muhimu sheria ifuatwe, na hicho ndicho kinachopiganiwa. Lakini ukianza kumuogopa jaji na kesi ndio tayari iko mahakamani utakimbilia wapi kwingine?

Rilaxx bro, mapambano yoyote lazima yawe na turning point, na kwako nimeona umeiweka mitandaoni, lakini lazima ijulikane njia ya kuihamisha toka mtandaoni kuyaleta field, vinginevyo yakibaki mitandaoni yatakuwa ni sawa na kelele tu.
Hahahaaaa........ Chadema ilishirikiana na Kigogo wa mitandaoni asiyejulikana!
 
6. Kuidai katibaa na ufuataji wa katiba hiyo na kuhubiri demokrasia huku sisi wenyewe tukiwa vyote hivyo hatuvitekelezi. Katiba ndogo tu ya chama inasiginwa na kubadilishwa kabisa kwa ajili ya faida ya mwenyekiti; demokrasia ndani ya kakichama kamoja tu hakuna.....ukitoa mawazo mbadala dhidi ya mwenyekiti unatukanwa, unakashifiwa na kufukuzwa kabisa chamani. Hakuna kupinga wala kuhoji lolote aliqletalo mwenyekiti (ref. ujio wa lowassa)!
 
6. Kuidai katibaa na ufuataji wa katiba hiyo na kuhubiri demokrasia huku sisi wenyewe tukiwa vyote hivyo hatuvitekelezi. Katiba ndogo tu ya chama inasiginwa na kubadilishwa kabisa kwa ajili ya faida ya mwenyekiti; demokrasia ndani ya kakichama kamoja tu hakuna.....ukitoa mawazo mbadala dhidi ya mwenyekiti unatukanwa, unakashifiwa na kufukuzwa kabisa chamani. Hakuna kupinga wala kuhoji lolote aliqletalo mwenyekiti (ref. ujio wa lowassa)!
Kama Katiba ya Chadema inasiginwa kwanini msajili asikifungie hicho chama kwa mamlaka aliyopewa na sheria mpya kandamizi ya vyama?

Tatizo lenu huwa mnaimba mapambio bila kujipa muda wa kuyatafakari. Kutoa mawazo sio hoja, muhimu mawazo yako ni concrete? au unataka kila utachosema kikubaliwe? na hao wanaokutukana ni wakina nani, viongozi? au mashabiki? wajibu watulie, kama hutaki challenges huwezi succeed kwenye maisha.
 
Mkuu umeandika kwa kiasi chake, ukijaribu kuangalia vizuri namna mfumo wa kiuongozi/kiutawala wa nchi hii utagundua yafuatayo;
1. Hii nchi ina mfumo wa hovyo na wa kimakusudi wa kuwalinda watawala na kukandamiza wananchi.
2. Huu mfumo siyo wa jana wala juzi. Ni wa miaka zaidi ya 40 iliyopita, ni kama mti uliopandwa mwaka 1970 na sasa ndio umekomaa na kuzaa.
3. Waanzilishi wa mfumo huu wa hovyo ndio wanaoitwa mashujaa leo hii, na majina kedekede na taswira mpaka kwenye fedha.
4. Kwa mfumo huu ni ngumu kujiita watu huru.
5. Mfumo ulisukwa kwa lengo mahsusi kunufaisha familia/ kundi la watu wachache.
6. Utamu wa matunda ya mfumo huu wa kale ukiyaonja lazima unogewe na kuupalilia mti huo milele.
7. Uchungu wa matunda ya mfumo huu wanaujua wale tuu walio/ watakaojaribu kuyashika na kupeleka mdomoni, haijalishi ni kiongozi wa dini, mwanasiasa, mtawala au raia wa kawaida.
8. Kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo mti unazidi kumea na kutoa matunda kwa wingi na harufu yake inafika mbali zaidi.
9. Asilimia kubwa ya waathirika wa mfumo huu wameamua/ tumeamua kukabidhi hii VITA ipiganwe kwa niaba yetu.
10. Kwa mpaka sasa bado haijaonekana hata chembe ya dalili ya kutoka hapa tulipo, kazi kubwa bado haijaanza kufanyika.
 
Kama hutaki kutembea na tumaini basi ni vigumu kupiga hatua yoyote chanya sio kwenye siasa zetu pekee, bali kwenye maisha kwa ujumla.

Suala la jaji kwenye kesi ya Mbowe kwa mfano, hilo halihitaji hofu sababu wao ndio wateuzi, kilichopo muhimu sheria ifuatwe, na hicho ndicho kinachopiganiwa. Lakini ukianza kumuogopa jaji na kesi ndio tayari iko mahakamani utakimbilia wapi kwingine?

Rilaxx bro, mapambano yoyote lazima yawe na turning point, na kwako nimeona umeiweka mitandaoni, lakini lazima ijulikane njia ya kuihamisha toka mitandaoni kuyaleta field, vinginevyo yakibaki mitandaoni yatakuwa ni sawa na kelele tu.

Kusema kweli polisi kwa kushirikiana na CCM wamejipanga kuipoteza Chadema, hawataki kabisa viongozi na wanachama wake wafanye chochote, tunapoelekea hata wakicheka watakamatwa, muhimu ni kuendelea na mapambano huku ikitafutwa njia mbadala.

Mfano, ile jogging ya Bawacha iwepo, waache kuvaa zile t-shirt zinazowakera CCM ( nasema CCM makusudi coz polisi ni tawi lao).

Naamini uwepo wao kwa pamoja utaamsha hari kati yao, utawaamsha watanzania wengine kujiunga nao, na utaamsha hisia za Katiba Mpya, hivyo wakati utakapofika wa kuyaunganisha makundi mengine, kazi itakuwa rahisi lengo litafikiwa kwasababu wote watakuwa na mawazo yanayofanana.

Ni in relaxation na matumaini kama yote kuyaandika haya na bila kujali hali:

1. Kwa lolote walilopanga na hata watakalopanga kwetu sisi haituhusu tena. Wao waendelee kivyao nasi tutaendelea kivyetu vyeru.

-- Wanasuka au wananyoa hiyo ni shauri yao.

2. Aboubakar kukamatwa hakupaswi kuwa mwisho wa uhunzi.

-- Harakati hazipaswi kupoa.

3. Mpambanaji mikononi mwao hajachuma janga la kula na wa kwao. Bali kila mpambanaji mikononi mwao anayetekeleza sera halali ya mapambano dhidi ya matumizi yao batili ya nguvu.

-- Tuuangazie utayari wetu kuyajaza magereza yao.

4. Mahakamani hatuna cha kujivunia bali kuweka wazi tu sehemu yetu ya hadithi kwa kila Tom na Harry kuweza kuona.

-- Kuwekeza kwenye matokeo chanya yanayoweza kupatikana kwenye mahakama zao ni kuwekeza kwenye kesi za ngedere hakimu nyani.

5. Sehemu tu ya 8m+ iliyopo inatosha sana kukionyesha kijinga chetu cha moto ya kwamba "we mean business."

-- Kuhamisha uwanja tokea mitandaoni kuelekea Tahrir ndiyo unaopaswa kuwa mwelekeo wenye tija zaidi.
 
Mkuu umeandika kwa kiasi chake, ukijaribu kuangalia vizuri namna mfumo wa kiuongozi/kiutawala wa nchi hii utagundua yafuatayo;
1. Hii nchi ina mfumo wa hovyo na wa kimakusudi wa kuwalinda watawala na kukandamiza wananchi.
2. Huu mfumo siyo wa jana wala juzi. Ni wa miaka zaidi ya 40 iliyopita, ni kama mti uliopandwa mwaka 1970 na sasa ndio umekomaa na kuzaa.
3. Waanzilishi wa mfumo huu wa hovyo ndio wanaoitwa mashujaa leo hii, na majina kedekede na taswira mpaka kwenye fedha.
4. Kwa mfumo huu ni ngumu kujiita watu huru.
5. Mfumo ulisukwa kwa lengo mahsusi kunufaisha familia/ kundi la watu wachache.
6. Utamu wa matunda ya mfumo huu wa kale ukiyaonja lazima unogewe na kuupalilia mti huo milele.
7. Uchungu wa matunda ya mfumo huu wanaujua wale tuu walio/ watakaojaribu kuyashika na kupeleka mdomoni, haijalishi ni kiongozi wa dini, mwanasiasa, mtawala au raia wa kawaida.
8. Kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo mti unazidi kumea na kutoa matunda kwa wingi na harufu yake inafika mbali zaidi.
9. Asilimia kubwa ya waathirika wa mfumo huu wameamua/ tumeamua kukabidhi hii VITA ipiganwe kwa niaba yetu.
10. Kwa mpaka sasa bado haijaonekana hata chembe ya dalili ya kutoka hapa tulipo, kazi kubwa bado haijaanza kufanyika.

Mkuu, ninakubaliana na yote uliyoandika. Hakuna linalotokea kutoka CCM ati kuwa ni accident:

IMG_20211004_150742_609.jpg


Uzuri ni kuwa tulipo tunajua tunakwama wapi na pia hatua za kuchukua ni zipi:

1. Kukamatwa mwenzetu yeyote hakutakiwi kupoza harakati zetu.
2. Hatupaswi kutegemea kupewa haki kwenye mfumo huu usiokuwa na usawa.
3. Chaguzi bila tume huru zinapaswa kusimama sasa.
4. Hatuna wachuma majanga kwenye harakati hizi bali tuna wapambanaji.
5. Utayari wetu wa kuyajaza magereza yao kutaendeleza mapambano bila ya kuwapa nafasi ya kulitumia neno ugaidi.
6. Focus yetu kwenye sehemu ya more than 8m+ available strong force, inatosha sana.
7. Tunapaswa sasa kuhamia medani ya Tahrir. Ya mitandaoni imetosha.
8. Sote kokote tulipo muda wa kuifanyia hisani nchi hii umewadia.
 
6. Kuidai katibaa na ufuataji wa katiba hiyo na kuhubiri demokrasia huku sisi wenyewe tukiwa vyote hivyo hatuvitekelezi. Katiba ndogo tu ya chama inasiginwa na kubadilishwa kabisa kwa ajili ya faida ya mwenyekiti; demokrasia ndani ya kakichama kamoja tu hakuna.....ukitoa mawazo mbadala dhidi ya mwenyekiti unatukanwa, unakashifiwa na kufukuzwa kabisa chamani. Hakuna kupinga wala kuhoji lolote aliqletalo mwenyekiti (ref. ujio wa lowassa)!

Uko nje ya mada mkuu.

-- Inataka wenye moyo kuikomboa nchi hii. Kwa vile huna, mengine ni kelele za mlango tu.
 
Mkuu, ninakubaliana na yote uliyoandika. Hakuna linalotokea kutoka CCM ati kuwa ni accident:

View attachment 1970075

Uzuri ni kuwa tulipo tunajua tunakwama wapi na pia hatua za kuchukua ni zipi:

1. Kukamatwa mwenzetu yeyote hakutakiwi kupoza harakati zetu.
2. Hatupaswi kutegemea kupewa haki kwenye mfumo huu usiokuwa na usawa.
3. Chaguzi bila tume huru zinapaswa kusimama sasa.
4. Hatuna wachuma majanga kwenye harakati hizi bali tuna wapambanaji.
5. Utayari wetu wa kuyajaza magereza yao kutaendeleza mapambano bila ya kuwapa nafasi ya kulitumia neno ugaidi.
6. Focus yetu kwenye sehemu ya more than 8m+ available strong force, inatosha sana.
7. Tunapaswa sasa kuhamia medani ya Tahrir. Ya mitandaoni imetosha.
8. Sote kokote tulipo muda wa kuifanyia hisani nchi hii umewadia.
Namba 7 & 8 zikifanyiwa kazi ipasavyo hakika nguvu ya umma itadhihirika na utawala wa kiimla utabaki historia TZ.
 
Mkinyoa, mkisuka ni shauri yenu
Hakuna kitu we endelea kupambana na corona, hili dude jingine ni gumu kweli kweli kwenu na kwako binafsi.

Jaribu kucheck afya ya akili yako ndo siku yenyewe hii, kabla mambo hayajawa mabaya zaidi kwako, Hauko sawa.

Sent from my HUAWEI MLA-L11 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom