CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015

Kuna nyuzi ukizipitia na kuangalia watu walisema nini na nini kinatokea, utakubaliana na mimi Chadema bado sana!.

Pasco

ha ha

unajua mageuzi yanaanza na akili kwanza

ukiwa ndani ya chama chochote kiwe chadema, ccm au ACT

kama mwanachama hana uwezo wa kushauri, kukosoa, kuonya na kusikilizwa, wanachama wa chama hicho hawana tofauti na mbuzi, ng'ombe, nyumbu, au mabata unawasukuma tu na kuwapa moyo

kisha unawajaza molari ya kuwa mwaka huu urais ni wetu, unarudia kauli mara nyingi mpaka wanaamini kabisa kuwa lazima washinde mwaka huo, bila kuangalia chochote kile...na hivi washazoea kuamini kutoka kwenye dini zao za uislamu na ukristo basi kuwaaminisha huku kwenye siasa ni kazi ndogo sana

kisha unawaaminisha kuwa 2020 urais ni wetu, miezi 11 tu baada ya kuwa ulishindwa ulichowaaminisha majuzi

maisha yanaendelea, ruzuku inaongezeka, watoto wao wanatembelea vogue, jeep na VX.....huku akina salary slip, mshana na mchambuzi na nguruvi wanapanda bajaji roho nyeupeeee.


kupenda raha bana
 
Hakika siasa zimewashinda kabisa. Isitoshe, ACT haistahili kuitwa chama cha siasa, ni kagenge tu kalichowezeshwa na utawala uliopita, ameondoka, na sasa mmekosa dira kabisa. Tulitabiri haya.

Kama vile kuvuruga chadema haitoshi, sasa yupo busy kuvuruga CUF. Its such a pitty kwamba Zitto aliyekuwa inspirational figure for many of us amegeuka kuwa mtu wa mipasho na vijembe kwenye mitandao ya kijamii na kujiacha utupu huku nyinyi wafuasi wake mkishangilia mfalme anazidi kunawiri na mavazi yanamkaa haswa.

Ama kweli kuishi ni kuona mengi.
 
Du! .
Pasco.
 
Tanzania hakuna chama cha siasa.Tanzania tunatawaliwa na Dola tu,chama cha siasa kinaongozwa na itikadi lakini kwa tz itikadi zipo kwenye katiba ya Magenge yaao.Iwe CDM,CCM,CUF,ACT haya yote ni magenge yaliyoamua kujivika majina ya vyama vya siasa ili wanachama wake waweze pata chakula cha familia zao.

Genge la chadema lipo kwa ajili ya kunufaisha watu wachache kama Mbowe,Mtei na sasa Lowasa.Chama cha siasa lazima kinadi itikadi yake katika jamii,Lakini itikadi ya chadema imegeuka kuwa matamko.

CCM nao ni kitengo alichokiacha Mwalimu ila kwa kukivika jina la chama cha siasa.CCM(Dola) ingekuwa ni chama cha siasa kingeruhusu na magenge mengine kama Chadema,ACT wafanye mikutano ya siasa lakini wote tunaona yanayoendelea.

ACT nao nigenge tu analopitia Zitto ili aweze kunufaika na Maisha ya kila siku.

Wanavyama wa magenge yote wapo kwenye magenge yao ili kujitafutia fulsa za kuendesha maisha yao ya kila siku.Hakuna mwanachama wa genge lolote aliepo kwa ajili yakumkomboa mtanzania.Wote wapo kwenye magenge yao ili kusaka fulsa za kuendesha matumbo yao.
 

ha ha ha, nacheka kwa dharau

huu mchezo hauhitaji hasira
 
Imani ni Kuishi Unachokijua. Na kila mtu hujisaliti mwenyewe kwanza kabla ya kusalitiwa na mwingine. Ole ukakwepa kuamini na kuishi kile kile unachokijua. Hii ni Afrika, nchi ya mtu mweusi. Afrika.
 
Angalia nondo hizi.
Huyu jamaa ni political scientist. Vyama vingine, ushauri kama huu huwa unalipiwa consultancy.
Hapa Chadema wamepewa bure!. Sasa angalia hoja hizi kama zilifanyiwa kazi.

P
 
Mkuu Mshana Jr, kwanza heshima mbele, hakuna mtu yoyote anayeiombea Chadema ife, kosa langu ni kuwa mkweli too much.

Humu jf tuna members wa aina 3, tuna
  1. Simple minds, discuss people, wao badala ya kujadili hoja iliyo mezani, hawa watamjadili mtoa hoja.
  2. Ordinary minds, discuss events, hawa watadili matukio, nini kimetokea etc
  3. Great minds discuss ideas, hawa watajadili hoja iliyo mezani.
Hivyo naomba keep on being free, kujadili watu, matukio na hoja, katika mabandiko yangu, ukiweza kujibu hoja, nitashukuru, ila hata ukinijadili, sikulaumu na likes nakutwangia.
Ukipata muda karibu ujibu hoja za bandiko hili.

Asante
P
 
Hakika siasa zimewashinda kabisa. Isitoshe, ACT haistahili kuitwa chama cha siasa, ni kagenge tu kalichowezeshwa na utawala uliopita, ameondoka, na sasa mmekosa dira kabisa. Tulitabiri haya.
Aisee...Post hii niliikosa ama ndiyo usahaulifu.
 
Siku hizi mtazamo wako umebadilika. Sijajua sababu ni nini!
===
Ningependa kuja mabadiliko yako yametokana na vyama ulivyovisuta kipindi kile kuamua kubadilika na kuwa vyama vya siasa haswa na siyo magenge tena?
 
Siku hizi mtazamo wako umebadilika. Sijajua sababu ni nini!
===
Ningependa kuja mabadiliko yako yametokana na vyama ulivyovisuta kipindi kile kuamua kubadilika na kuwa vyama vya siasa haswa na siyo magenge tena?
Niling'amua nivigumu kufanya mabadiliko ukiwa nje ya vyama vya siasa kwa mfumo wanchi yetu namna ulivyo. Pia sikudhani kama kuna mtanzania anaweza agiza mtanzania mwenzake amiminiwe mvua ya risasi kisa kupishana namna kutafakari na kufanya mambo. Baada yahapo nahitaji nifanye mabadiliko nikiwa ndani ya mfumo ambao naamini mbeleni unaweza kubadilika, na sehem sahihi kwangu ni upinzani.
 
Chadema wametangaza rasmi kuiunga mkono ACT Zanzibar. Na wao Chadema wanaomba ACT iwaunge mkono kwenye Muungano.
ACT has evolved beyond expectations of many...
 
Tatizo ulikuwa na chuki sana na Zitto ukashindwa kuweka akiba ya maneno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…