Huwa tathimini yangu nilioipiga nimeona nikama mikoa ya mbeya songwe chadema niwengi kuliko mikoa mingine yote
Mwaka huu mtajamba cheche!Hamna ki2 apo
Ka-simu ameanza vituko vya kuteka watu!Yapo majinga mengi yalitia Nia ccm, na Pasco Mayala akiwemo, kwa kudhani kuw a CCM itawabeba kiulaini. lakini shughuli ya October hata kasimu majaliwa huenda asirudi bungeni
ingawa sijaelewa wanachokiimba lakini wamenifurahishaCHADEMA msingi upo imara kabisa ndani ya nyoyo za waTanzania
Hawa ni wapiga diliHivi hawa hawana habari za ndege kununua kwa cash? Hawajui SGR?
Mbona wako hivi hawa? Jee hawana habari za kuunga mkono juhudi kwa kina Nasari, Gekule, Silinde, na madiwani wengi tuu? Hata daraja la mfugale ambalo ni la aina yake barani Afrika?
Kama namuona silinde!!!Na hii ndo itakuwa hali halisi mwaka huu. Hakuna namna CCM itaishinda Chadema mwaka huu si udiwani, si ubunge wala si Uraisi
Ushauri : Mgombea wa ccm Tunduma ajitoe .13 August 2020
Tunduma, Tanzania
UMATI WA WATU WAMPELEKA MWAKAJOKA KUCHUKUA FORM YA KUGOMBEA UBUNGE.
Source: DSS Tunduma
Tuliwaambia CCM Mpya wananchi wanataka sera bora zitakazowafanya wawe watu huru katika kujiletea Maendeleao ya Watu.
Mfano wa Maendeleo ya Watu kwa mtu huru ni serikali kuweka mazingira bora katika kilimo. Siyo wao wanalima Korosho kama watoto yatima halafu siku ya mavuno serikali inakuja kuyanyakuwa kwa mkopo wakati wamefanya kazi kwa bidii na jingi bila msaada wa Mkuu wa wilaya DC, RC, Waziri wa Kilimo, Ofisi ya Waziri Mkuu wala Ofisi ya Rais. Huo ni mfano mmoja wa unyanyasaji.
Wananchi wanaona unyanyasaji wa wazi kwa wabunge wao waliowatuma huko ndani ya Bunge na nje ya Bunge. Chaguzi ndogo kati ya 2015-2019 zilizofanyika kukuta Ofisi ya Mkurugenzi imefungwa! Mwaka 2019 November Uchaguzi wa serikali za Mitaa na Vijiji wagombea wa upinzani kunyimwa fomu au kuenguliwa kihuni wananchi waliona. Vyombo vya habari kutishwa kurusha habari za wapinzani...
Wananchi wanalipa kodi lakini viongozi wanasema wazi na kwa vitendo vya kibaguzi kuwa hawatapata barabara kwa vile wamechagua viongozi bora ambao wametokana na upande mbadala ambao licha ya kuwa unatambulikana kisheria kupitia katiba lakini wanaadhibiwa na CCM Mpya kwa kunyimwa huduma muhimu za Maendeleo ya Watu.
Sasa wananchi wameamua kusema basi!
Tunduma ni wapiga spana waliotukukaUshauri : Mgombea wa ccm Tunduma ajitoe .
Alishawaambia hakuna kuwa neutralNyie chadema kwenye sanduku hatuwawezi, ila inshaalah wakurugenzi wanalipwa na gari zao zinajazwa mafuta kwa hela kutoka mfuko wa mwenyekiti wetu naamini jambo haliwezi haribika!
mkuu kuwa honest kwenye nafsi yako, hebu jiulize inawezekana vp pamoja na mazingira ya upinzani kubanwa sana awamu hii lakini kumbe bado wapo tu kwa wingi hivyo?!. na hapo hakuna cha wasanii wa muziki wala wananchi kusombwa kwa mabasi/malori!!.Hapo unakuta wanaopiga kura ni wachache tu
Hao walipata elimu mapema sana, so wanajua kufanya tafakuriKina mama wa Mbeya huwa nawaelewa sana, hawanaga shobo na mboga mboga wamejitambua kitambo sana.
Hakika CHADEMA imekuwa imara sana.Unaweza kutoka machozi
Magufuli hakushauriwa na yeyote , aliamua mwenyewe binafsi kwa kudhani ana akili kuliko wengine , Sisi wengine tulijua kitakachotokeaKati ya makosa makubwa CCM watajilaumu kumuacha akazuia Shughuli za Vyama vya siasa na kudhulumu uchaguzi wa Serikali za mitaaa mwaka jana ndio matokeo yake tunayaona leo
WANANCHI KOTE NCHINI BARA NA VISIWANI WAMEKUA NA SHAUKU KUBWA SANA YA KUWASIKILIZA WAPINZANI KINYUME KABISA NA MAWAZO KUWA WANGEKATA TAMAA
Kiukweli kupitia hili ccm wajifunze ;ingekua wapinzani wanapata muda wa kusema miaka mitaano hii bila kunyanyaswa leo hawangekua na la kuwaambia watu
Binadamu huna jipya la kuwafanyia au kuwapa ; WAPE KILA KITU ILA USIWANYIME MDOMO KUSEMA NA MASIKIO KUSIKIA ......Dola na Vyama vyenye Nguvu duniani zilifanya Maendeleo makubwa Lakini zilianguka kwa sababu tu waliziba watu midomo ...
Leo CCM haipo kwa watu kabisa zaidi ya kwenye Dola tena kwenye dola sio wote bali wale wenye mamlaka
Wanamikakati wa CCM wamempotosha Sana Mwenyekiti
Mwaka Huu ni maeneo machache Sana ccm inaweza kushinda kihalali Hii ni tofauti kabisa na miaka mitano nyuma Pamoja na kazi nzuri iliyofanywa
SEKRETARIET ya CCM imeuwa Chama kwenye mioyo ya watu !!!!!
Baada ya uchaguzi Huu lazima mabadiliko makubwa yafanyike kwenye sekretariet ya CCM ile ya kina Kinana na Nape was far better kwakua ilikua na approach ya kutumia siasa zaidi kuliko kutegemea kubebwa na Dola nzima .