Uchaguzi 2020 CHADEMA vipi, jiwe la Tume ya Uchaguzi liliwapata gizani

Uchaguzi 2020 CHADEMA vipi, jiwe la Tume ya Uchaguzi liliwapata gizani

Nguruka

Senior Member
Joined
Dec 6, 2006
Posts
189
Reaction score
129
1-1.jpg

MAPEMA Juma hili tumesikia baadhi ya vyama vya siasa nchini vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa 2020 vikitoa maneno makali dhidi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kile ambacho wao wanasema kuwa Tume imekosa meno dhidi ya wanaokiuka Maaduili ya Uchaguzi.
Mgombea Urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lisu alitumia dakika kadhaa jukwaani wakati wa kampeni zake huko mkoani Songwe kujibu mapigo dhidi ya taarifa ya Tume ya kuvionya vyama ambavyo vinakiuka maadili ya uchaguzi wakati wa kampeni zao.
Tume kupitia Mkurugenzi wa Uchaguzi, haikumtaja mtu wala Chama cha Siasa anacho kituhumu kukiuka maadfili ya uchaguzi (Hii vijana tunaita kurusha jiwe gizani, utakaesikia anaguna ujue limempoata).
Hivyo Tume ilitupa jiwe gizani lakini binafsi nadhani liliwapata Chadema maana kitendo cha mgombea wao wa Urais kuijibu Tume ni ishara kuwa jiwe hilo liliwapata na huenda limewaumiza.
Mimi naamini kuwa limewaumiza na ndio maana wamesimama kujibu mapigo. Lakini ni Dhahiri kuiwa Chadema kupitia mgombea wao huyo ndio walianza kukiuka maadili ya uchaguzi ambayo waliyasaini kama ishara ya kuyafuata wakati wa kampeni.
Sehemu ya pili ya Maadili hayo ya Uchaguzi inaeleza wazi yanayotakiwa kufanywa na vyama Siasa na Wagombea Katika Kuendesha Shughuli za Siasa wakati wa Kampeni.
Moja ya wajibu wa Vyama vya Siasa na Wagombea kuheshimu na kufuata Katiba ya Nchi sheria za uchaguzi, kanuni za uchaguzi, maadili ya uchaguzi na maelekezo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi pamoja na sheria nyingine za nchi katika kipindi chote cha uchaguzi.
Sasa kwanini nasema Chadema jiwe la tume limewapata ni kwakua wenyewe wamekua wakifanya baadjhi ya vitu ambavyo hawapasi kufanya kwa m,ujibu wa Maadili ya uchaguzi.
Mambo yasiyotakiwa kufanywa na Vyama vya Siasa kulingana na Kanuni za Maadili ya Uchguzi na ambayo Chadema imekua ikiyafanya ni pamoja na .
Kufanya fujo au kuchochea vurugu ya aina yoyote katika mikutano ya vyama vingine; hili limefanmyika katika mkutano wao wa kwanza walihamasisha watu waandamane.
Kutumia lugha ya matusi, kashfa, kejeli, udhalilishaji na vitisho au lugha inayochochea uvunjifu wa amani au kuashiria ubaguzi wa kijinsia, ulemavu, rangi au maumbile kwenye mikutano na kwenye shughuli zote za kampeni;ya kampeni ya vyama vingine vya siasa na matangazo ya uchaguzi yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi;
Pia kutokubali au kutokuheshimu maamuzi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi yanayofanywa kwa mujibu wa sheria za uchaguzi.
Hivyo Chadema wanatakiwa kutoa boriti katika macho yao ndipo waende kutoa Boriti kwa tume ya taifa ya Uchaguzi ambayo kimsingi inapaswa kutoa ingiliwa na mtu au chama chochote wakati inatekeleza majukumu yake.
 
KAMA HUNA AKILI TIMAMU HUWEZI KUELEWA HII. ASANTE SANA BWANA NGURUKA
 
Sijasoma habari yako, lakini kutokana na kichwa cha uzi, inaonekana kuna unacho kitafuta.

Mmezoea kusema kibaraka wa mabeberu, sasa maheara kasema akawaambie wajomba zake huko ulaya. Je uli ulifikirini nani anayetajwa kama si huyo anaye wanyima usingizi?
 
Nguruka.

Umekaa unaandika ujinga huku unajifanya huoni ?! Huoni vyama vinavyonyanyaswa kwa kuenguliwa wagombea wao ?! Unajifanya kipofu kutoona vyama vingine vinafanya kampeni kwa lugha kisukuma ?! Hujui nini , kwamba uonewe ukae kimya ndiyo nidhamu ?!.
 
Sijasoma habari yako, lakini kutokana na kichwa cha uzi, inaonekana kuna unacho kitafuta.
Mmezoea kusema kibaraka wa mabeberu, sasa maheara kasema akawaambie wajomba zake huko ulaya. Je uli ulifikirini nani anayetajwa kama si huyo anaye wanyima usingizi?
Tatizo jingine hilo, Hujasoma Uzi lakini umejua kilichowasilishwa daaaaah
 
Nguruka.
Umekaa unaandika ujinga huku unajifanya huoni ?! Huoni vyama vinavyonyanyaswa kwa kuenguliwa wagombea wao ?! Unajifanya kipofu kutoona vyama vingine vinafanya kampeni kwa lugha kisukuma ?! Hujui nini , kwamba uonewe ukae kimya ndiyo nidhamu ?!.
Mbona povu sana braza kama umewekewa pilipili puani?

Miongoni mwa vyama vilivyowekea wengine pingamizi ni pamoja na hiki chako, usijitoe ufahamu!

hujazuiwa na wewe kwenda kuongea kingoni songea, au kihaya bukoba. kuto kujua lugha za kwenu isiwe sababu ya kulalamika bwana mdogo
 
Nguruka.
Umekaa unaandika ujinga huku unajifanya huoni ?! Huoni vyama vinavyonyanyaswa kwa kuenguliwa wagombea wao ?! Unajifanya kipofu kutoona vyama vingine vinafanya kampeni kwa lugha kisukuma ?! Hujui nini , kwamba uonewe ukae kimya ndiyo nidhamu ?!.
Pole sana na wewe kusoma huo unaoaita Ujinga lakini umekujaza povu la kilo 100.
 
Namba bado haziongopi, takwimu za uhakika bado zinaonyesha ya kwamba, endapo uchaguzi kama ungalifanyika mwishoni mwa juma hili l, matokeo yangekuwa kama ifuatavyo;
TAL kwa upande wa CDM 69%
JPM kwa upande wa CCM 21%
Vyama vingine 10%

Prediction bado inaonyesha TAL anaweza kuchukua 3% kutoka kila upande ifikapo mwisho wa mwezi huu na kufikisha 75% huku akimuacha mgombea wa CCM kwa mbali akijikongoja kwa 19% na vyama vingine kwa 7%

Mfalme Sauli aliua kwa mamia lkn Daudi mtumishi wa Mungu aliua kwa mealfu. Hii ndizo sauti zisikikazo kutoka kwa wapigakura.
 
Sijasoma habari yako, lakini kutokana na kichwa cha uzi, inaonekana kuna unacho kitafuta.
Mmezoea kusema kibaraka wa mabeberu, sasa maheara kasema akawaambie wajomba zake huko ulaya. Je uli ulifikirini nani anayetajwa kama si huyo anaye wanyima usingizi?
Usiogope kusema umesoma maana hakuna mtihani hapo baade. Chamsingi tufahamishane tu. Je Umesoma vyema Maadili ya Uchaguzi? Kama hayo haujayasoma hapo sawa. Maana hata Mgombea wa Chadema alipokua akiijibu Tume aliruka Sehemu ya 2.2 ambayo inaainisha mambo 13 ambayo Vyama vya Siasa havitakiwi kuyafanya.
 
Mbona povu sana braza kama umewekewa pilipili puani??,
Miongoni mwa vyama vilivyowekea wengine pingamizi ni pamoja na hiki chako, usijitoe ufahamu!!
hujazuiwa na wewe kwenda kuongea kingoni songea, au kihaya bukoba. kuto kujua lugha za kwenu isiwe sababu ya kulalamika bwana mdogo
Sheria zinasemaje kuhusu lugha ya campaign ?! Na unadhani ni kwanini mgombea hata mmoja wa udiwani hakuenguliwa kwa sababu za pingamizi za wapinzani ?!.

Usijifanye kipofu dogo
 
Namba bado haziongopi, takwimu za uhakika bado zinaonyesha ya kwamba, endapo uchaguzi kama ungalifanyika mwishoni mwa juma hili l, matokeo yangekuwa kama ifuatavyo...
NEC wametangaza Uchaguzi Mkuu ni tarehe 28/10/2020 siku ya Jumatano. Sio hii ya kwako za "kwamba" , "endapo" na "mwishoni mwa juma hili"
TAFITI ZA KUBUMBA NA KUFIKIRIKA TUPA KULEEE!! Subiri Sanduku la kula liamue, hatutaki uganga wa jadi hapa
 
Ukiona umeweka bandiko, saa moja ikapita unayo like moja, ujue umeharisha. Waombe mods wakusaidie kufuta. Hata maccm wenzako wamekususa, ujue leo hupati hata jero.
 
Back
Top Bottom