CHADEMA wakubali yaishe majimbo baada ya serikali tatu kukubalika katiba mpya

CHADEMA wakubali yaishe majimbo baada ya serikali tatu kukubalika katiba mpya

Hivi kati ya maoni haya ya rasimu yepi yalikuwa maoni ya CCM? nahitaji kujua hilo! Maana naona maoni karibia yote ni mwiba kwa CCM!

Ni huu ushabiki wa kisengerema ndio uliotaka kuharibu zoezi hapo awali, tutenganishe kabisa siasa na uandishi wa katiba maana tutaharibu zoezi hili. Kwa taarifa yako muongozo wa kutoa maoni ya katiba kwa wana ccm ni kama umepigwa photocopy tu kwenye hii rasimu.
 
Demokrasia ni pana, busara, uvumilivu na ustahimilivu ni muhimu kwa ajili ya umoja wa kitaifa. Pamoja na kila mmoja kuwa na maoni ya mtazamo binafsi licha ya mtazamo wa vyama vya siasa, taasisi, mashirika nk, hatimaye katiba inayopatikana haiwezi kumridhisha kila mmoja, ikitokea kumridhia kila mtu, kila taasisi, kila chama cha siasa dhahiri itakuwa na mapungufu makubwa maana itakuwa imeudhwa kuridhia kila mtu kitu ambacho kwa mwingine hakiungi mkono nk.

Kuna maoni kadhaa ya Chadema yanaonekana kukubalika katika rasimu ya katiba mpya, ingawa kuna ile ya serikali ya majimbo inaonekana kugonga mwamba. Busara kuwa tayari kupokea ambayo yanaonekana kukubalika na wengi maana muundo wa serikali tatu utaondoa kero kadhaa ambazo zilikuwa zinaielemea serikali mbili ya Muungano na ile ya Zanzibar.

Mimi kwangu kilichonivutia ni pale kwenye Madaraka ya Raisi yanabaki kama yalivyo hapo tu, Mimi binafsi napinga kuvunja vunja Madaraka ya Raisi, sitaki kuishi kwenye Nchi ambayo hakuna mtu mwenye NENO la Mwisho! Hivyo nakubaliana na hii Rasimu!
 
Daah kuna ulaji tena wa kuandaa katiba Tanganyika? Itabidi tufanye mipango nasisi tuwemo humo kama kina Humphrey Harakaharaka.

Mkuu hiyo inakuja!ZNZ wenyewe tayari wanayo hadi katiba kamili!Nahisi tutapiga kura ya maoni kama jina letu la Tanganyika lirudi au tuitwe tu Tanzania Bara!

Ulaji huo lkn nahisi itakuwa ngumu kidogo kupenyezewa ulaji kuwa mjumbe wa Tume hiyo la sivyo uwe na sifa za u-jaji!
 
kwa kuwa hii ni RASIMU YA MAPENDEKEZO sio kwamba ndio imeshakuwa KATIBA RASMI ahhh tutaijadili huko kwenye mabaraza ya katiba kwa nguvu zote hata mimi naweweseka na serikali 3, ni MZIGO kwa Taifa na athari zake ni kubwa kwa Taifa zima.
-pia athari zake MGOMBEA BINAFSI KWA NAFASI YA U-RAIS ni kubwa pia so haya ni mambo mawili nitajadili kwa kina katiba baraza la katiba wilaya. kwa kuwa ni mjumbe sina shaka watanielewa wajumbe wenzangu tutaelewana na kushauri wengine kuliona hili kwa jicho la mbali zaidi...................Mungu ibariki Tanzania......!!!
 
Mkuu hiyo inakuja!ZNZ wenyewe tayari wanayo hadi katiba kamili!Nahisi tutapiga kura ya maoni kama jina letu la Tanganyika lirudi au tuitwe tu Tanzania Bara!

Ulaji huo lkn nahisi itakuwa ngumu kidogo kupenyezewa ulaji kuwa mjumbe wa Tume hiyo la sivyo uwe na sifa za u-jaji!

Daa hivi ni lazima kuwaza haya majina mawili tu? Mimi ningependa tutunge jina jipya lisilo na chembe za ukoloni kama hili la Tanganyika.
 
hii katiba mpya utafikiri imeandikwa na chadema. katiba ina mambo yale chadema iliyo yapendekeza sema baadhi yamebadilishwa kimuundo tu. mia
 
Daa hivi ni lazima kuwaza haya majina mawili tu? Mimi ningependa tutunge jina jipya lisilo na chembe za ukoloni kama hili la Tanganyika.

Rasimu ya Katiba Mpya imesisitiza kuhusu kuutambua UTU WETU na HESHIMA;watasema tukileta jina jipya kabisa basi HATUUTAMBUI UTU wetu na TULIPOTOKA ahahahahaha
 
Rasimu ya Katiba Mpya imesisitiza kuhusu kuutambua UTU WETU na HESHIMA;watasema tukileta jina jipya kabisa basi HATUUTAMBUI UTU wetu na TULIPOTOKA ahahahahaha

Nitakubaliana nao kama watanishawishi kuwa hakuna mkono wa mkoloni kwenye jina la Tanganyika, la sivyo jina hili linatudhalilisha sisi na utu wetu.
 
Mwenye hyo draft atupe tuipitie maana warioba kataja machache tu asije ikawa kataja yale yaliyopendwa kusikika na majority ila yale ambayo wananch hawayaki na kuyapinga kwenye maoni hayajasomwa lkn yapo kwenye rasimu.
 
img2383.JPG
​
  • IDADI YA MAWAZIRI
Inapendekezwa Rais aunde Serikali ndogo iliyo na Mawaziri wasiozidi kumi na tano na mawaziri hao wasiwe wabunge. Mawaziri hawatahudhuria vikao vya Bunge isipokuwa kama watahitajika kutoa ufafanuzi kwenye kamati za Bunge.
  • BAADHI YA MAMBO AMBAYO HAYAMO KWENYE RASIMU YA KATIBA
    • Serikali ya Majimbo
Ndugu Wananchi, Tume ilipokea maoni kuhusu mambo mengine muhimu ambayo hayamo katika rasimu hii. Moja ya mambo hayo niSerikali za Majimbo. Tume ilichambua maoni na sababu za wananchi kupendekeza Serikali za Majimbo lakini Tume ilibaini changamoto nyingi na ikaamua kutopendekeza muundo huu. Kwanza, baada ya kuamua kupendekeza Muundo wa Muungano wa Serikali Tatu, ilionekana ni dhahiri kuongeza ngazi nyingine ya Serikali ingeleta gharama kubwa. Serikali nyingine kumi zingekuwa na Wakuu wa Majimbo, Mabaraza ya Mawaziri na Mabunge na gharama yake ingekuwa kubwa. Pili, katika kutembelea nchi Tume ilishuhudia dalili za wazi za mivutano ya Udini, ukanda,malalamiko ya upendeleo wa baadhi ya maeneo na ukabila. Dalili zilikuwa wazi kwamba utawala wa majimbo ungeirudisha nchi kwenye utawala utakaoigawa nchi kwa misingi ya ukabila, udini na ukanda na kuzigawa rasilimali za taifa kikanda na hivyo kuleta tofauti kubwa ya kimaendeleo katika nchi.
  • TUME YA UCHAGUZI
Tume imefanya uchambuzi wa maoni ya wananchi kuhusu Tume ya Uchaguzi. Tume inapendekeza jina la tume liwe Tume Huru ya Uchaguzi. Tume pia inapendekeza sifa za wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ziwekwe kwenye Katiba. Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi watapatikana kutoka miongoni mwa watu wenye sifa zilizoainishwa ndani ya Katiba kwa kuomba. Majina ya waombaji yatachambuliwa na Kamati ya Uteuzi ambayo Mwenyekiti wake atakuwa Jaji Mkuu na wajumbe wengine sita ambao ni Majaji Wakuu wa nchi Washirika, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Maspika wa Mabunge wa nchi Washirika na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu. Kamati ya uteuzi itapendekeza majina ya watu wanaofaa kwa Rais ambaye atateua Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine. Bunge litathibitisha uteuzi wao. Wabunge na viongozi wa aina hiyo hawatakuwa na sifa za kuwa wajumbe wa tume ya uchaguzi.
  • MUUNDO WA MUUNGANO
Wananchi waliopendekeza muundo wa Serikali tatu walikuwa wengi kuliko makundi yote. Sababu zao zilikuwa nzito lakini pia kulikuwa na changamoto nyingi na nzito. Pamoja na maoni ya wananchi Tume ilirejea sababu za kupendekeza muundo huu zilizotolewa na Tume zilizopita na Tafiti zilizofanywa na Tume kuhusu aina mbalimbali za Muungano. Baada ya yote hayo Tume ilifikia uamuzi wa kupendekeza mfumo wa Serikali tatu. Yaani Serikali ya Shirikisho, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
  • ORODHA YA MAMBO YA MUUNGANO
Ndugu Wananchi, Tume imependekeza katika Rasimu ya Katiba kuwa orodha ya Mambo ya Muungano yawe 7 badala ya 22 yaliyopo sasa. Mambo ya muungano yanayopendekwa ni:
  1. Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  3. Uraia na Uhamiaji
  4. Sarafu na Benki Kuu
  5. Mambo ya Nje
  6. Usajili wa Vyama vya Siasa
  7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya Kodi yatokanayo na Mambo ya Muungano.
sikubaliani na hoja kwamba ukanda utaleta ukabila na udini,huu ni ufinyu wa kuangalia, kjiona kwamba sisi ni wakanda fulani hilo na kubaliana nalo kama ilivyo tunapojiona kwamba sisi ni wa mkoa fulani au wilwya fulani,lakini ukabila utakuwa hauna nafasi kwa sababu ukanda unachanganya makabila mengi na dini nyingi, kama ni ukabila ungeletwa na mikoa au wilaya maana hii ndio inaweza kukuta wilaya ina kabila moja au mkoa una kabila chache sana, sasa kama hatukuweza kuwa na ukabila kwenye umikoa wenye kabila chache tutawezaje kuwa na ukabila kwenye ukanda wenye kukusanya makabila mengi?. suala la ukanda ndio suluisho la ufisadi
 
  • IDADI YA MAWAZIRI
Inapendekezwa Rais aunde Serikali ndogo iliyo na Mawaziri wasiozidi kumi na tano na mawaziri hao wasiwe wabunge. Mawaziri hawatahudhuria vikao vya Bunge isipokuwa kama watahitajika kutoa ufafanuzi kwenye kamati za Bunge.


Mambo ya muungano yanayopendekwa ni:


  1. Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  3. Uraia na Uhamiaji
  4. Sarafu na Benki Kuu
  5. Mambo ya Nje
  6. Usajili wa Vyama vya Siasa
  7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya Kodi yatokanayo na Mambo ya Muungano.


Kwa nini Mawaziri 15 wakati mambo ya Mungano ni 7 tu?
na hata ukiangalia hapo mambo ya muungano yatakayo itaji Mawaziri haya Zidi 5, kwavyovyte ilitakiwa Mawaziri wasizidi 10 na sio 15.
 
serikari ya majimbo wanaikwepa tu kwa kisingizio na hoja nyepesi lakini Utawala wa Majimbo ni wa Gharama nafuu zaidi ya serikari tatu endapo watazingatia Majimbo mawili

Magamba wamebanwa kila mahali. Hii tume inakua kama kiini macho
 
Back
Top Bottom