CHADEMA wanaamini Serikali itawafukuza wabunge 19 na kuwaunga wao kugomea matokeo ya uchaguzi

CHADEMA wanaamini Serikali itawafukuza wabunge 19 na kuwaunga wao kugomea matokeo ya uchaguzi

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
Mimi siwaelewi chadema kabisa na watanzania wanaoshabikia hili

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 CHADEMA walitangaza kutokubali matokeo na kuamua kususia kila kitu kilichotokana na uchaguzi huo kwa kufanya yafuatayo.

1. walitangaza kutomtambua raisi
2. Walimzuia mbunge wa nkasi kwenda bungeni
3. walitangza kususia nafasi za ubunge wa viti maalumu
4. Walitangaza kususia ruzuku.

Baada ya kufanya haya
Chama kiligawanyika katika makundi kulingana na maslahi

1. Mbunge wa nkasi alikataa kutii na kuwaeleza kuwa yeye alichaguliwa na wananchi wa nkasi hivyo alikwenda bungeni kuwawakilisha wananchi wa nkasi.

2. Wanawake waliotegemea nafasi za viti maalumu walikataa hoja za kususa kwa hoja kwamba msiamo wa chama chaguzi zote umekuwa wa kukataa matokeo, kipindi hicho viongozi walipokuwa wakipata nafasi za ubunge hawakuleta hoja za kususia fursa hizo ila baada ya kukosa wanataka kila mtu asuse.

Wanawake waliona kama kuna doble standard katika maamuzi na hivyo kuamua kutosusia nafasi za ubunge wa viti maalumu. Hapa Chadema walianzisha mchakato wa kuwatimua bungeni kwa kwanza kudai hawajawateua, hoja hii ilipogonga ukuta wakawafukuza chama kwa kutegemea watakuwa wamekosa sifa za kuwa wabunge.

3. Viongozi wa juu wa chama, Mwenyekiti pamoja na Makamu mwenyekiti wamekutana na raisi mara kadhaa ikiwemo kwenda ikulu. hii inaonyesha viongozi wa juu nao wametupilia mbali msimamo wa kutotambua matokeo ya uchaguzi.

4. Chama kumwandikia spika wa bunge barua ni sawa na kutambua pia matokeo ya uchaguzi kwa maana kama hutambui matokeo ya uchaguzi na kitu chochote kilichotak kwenye matokeo ya uchaguzi huwezi kumwandikia "official letter" mtu anayeshika wadhifa uliotokana na matokeo ya kura.

Lakini yote bin yote ni hii hatua ya CHADEMA kutafuta serikali / Bunge kuwaunga mkono wao waliosema hatutambui matokeo ya uchaguzi na fursa zitokanazo na matokeo ya uchaguzi kwa kuwafukuza wabunge 19 ambao wao walikaa upande wa serikali na bunge kwa kutambua kila kitu na kuchukua fursa.

Je, inawezekana serikali ikawaunga mkono kwenye kivuli cha katiba inavunjwa?

Je, katiba inawapa ruhusa wanachadema kugoma na inawanyima ruhusa baadhi ya wanachadema kukataa kugoma?

Je, mwenyekiti anavyokwenda ikulu kuzungumza na mama wakati chama kilishatoa msimamo wa kutotambua serikali, je naye anatakiwa kuchukuliwa taratibu za kinidhamu na chama?
 
Mimi siwaelewi chadema kabisa na watanzania wanaoshabikia hili

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 chadema walitangaza kutokubali matokeo na kuamua kususia kila kitu kilichotokana na uchaguzi huo kwa kufanya yafuatayo...
Umejenga hoja vizur sana.
 
Hakuna hoja ya maana uliyojenga hapo zaidi ya kuwaza kwa mazoea, na mazoea yako hayo ndio yamewaponza hao kina Mdee na wenzake.

Wamefukuzwa uanachama.
 
Hakuna hoja ya maana uliyojenga hapo zaidi ya kuwaza kwa mazoea, na mazoea yako hayo ndio yamewaponza hao kina Mdee na wenzake.

Wamefukuzwa uanachama.
Nchi hii tuna wanasheria wasiojua kutafsiri sheria na ndo hao wanaowaponza chadema.

Mzizi wa kosa kamwe hauwezi kuachwa katika maamuzi ambayo yanatolewa baadae juu ya mambo yanayofuata.

mfano
Kumzurumu mtu pesa yake ni kosa kisheria na mtu akikufikisha mahakami utahukumiwa. Lakini mahakama haiwezi kutazama kudhulumiana pesa tu bila kuangalia kama madai hayo ya pesa yalikuwa halali (hapa tunatazama mzizi wa tendo la kudhulumiana ni nini?) kwamba ukimuuzia mtu bangi na huyo mtu akashindwa kukulipa pesa yako huwezi kumpeleka mahakamani kwa kuwa mzizi wa tendo unaloliona lina uhalali kisheria haukupi haki ya kudai haki mahakamani.

au mtu akikuahidi rushwa ili umuhudumie na ukatoa huduma lakini akashindwa kukupatia fedha basi huwezi kuwa na haki mahakamani kwa kuwa fedha siyo halali.

Turudi kwenye mada yetu.
Kosa la hawa wabunge 19 ni kwenda kuapishwa bungeni na hili siyo kosa katika jamhuhuri ya muungano wa tanzania. Hivyo kuwafukuza uanachama pekee haitoshi kuwakosesha ubunge lakini kama kosa lao ni kwenda kuapishwa basi ni vigumu kwa mahakama kusema wabunge walikosea kwenda kuapishwa na ni halali kufukuzwa kwa kitendo hicho. Kama chama kisingekuwa kimegawanyika makundi mawili labda lakini kama ni hawa waligomea kwa nini wote wasigome,

ngoja tusubiri mahakama itasemaje
 
Nchi hii tuna wanasheria wasiojua kutafsiri sheria na ndo hao wanaowaponza chadema.

Mzizi wa kosa kamwe hauwezi kuachwa katika maamuzi ambayo yanatolewa baadae juu ya mambo yanayofuata...
Tangu lini mtu kuapishwa bungeni ikawa kosa?

Kosa la hao wanawake ni kutofuata taratibu za chama chao kwenye uteuaji na hatimaye uwasilishwaji wa majina bungeni.

Kuna forgery na mambo mengine mengi, inshort huu uhuni umesimamiwa na CCM na kuratibiwa na taasisi zake, kosa halipo Chadema hata sekunde moja.
 
Tangu lini mtu kuapishwa bungeni ikawa kosa?

Kosa la hao wanawake ni kutofuata taratibu za chama chao kwenye uteuaji na hatimaye uwasilishwaji wa majina bungeni.

Kuna forgery na mambo mengine mengi, inshort huu uhuni umesimamiwa na CCM na kuratibiwa na taasisi zake, kosa halipo Chadema hata sekunde moja.
Kumbuka wakati huo chama kilikuwa kimegawanyika makundi mawili.

Kuna kundi lilikuwa linapinga hawa kwenda bungeni na hawa ndiyo wanajaribu kufanya ujanja wa kutazama utaratibu na mchakato wa chama wakati walikuwa wamepinga.

Labda kama katiba chama imeweka utaratibu wa kunapotokea mgawanyiko kama huo, mwenyekiti, katibu au mtu yeyote ambaye alitakiwa kukuwekea saini amesusa

na wewe mwanachama ukaamua kutosusa je, mchakato uweje?

kama hilo halimo kwenye katiba basi tukio kama hili linakuwa fundisho linalopelekea maboresho ya katiba.
 
Mimi siwaelewi chadema kabisa na watanzania wanaoshabikia hili

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 chadema walitangaza kutokubali matokeo na kuamua kususia kila kitu kilichotokana na uchaguzi huo kwa kufanya yafuatayo...
Tufafanulie kwanza kura bandia kwenye mabegi zilikuwa za Nini? Tufafanulie kabla ya kupiga kura, tayari CCM Wana wabunge 80 wa kupita bila kupingwa maana yake nini? Fafanua kwanza kurudisha fomu za wagombea ni CCM tu walijua kujaza wapinzani tu ndio hawakujua.
 
Mimi siwaelewi chadema kabisa na watanzania wanaoshabikia hili

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 chadema walitangaza kutokubali matokeo na kuamua kususia kila kitu kilichotokana na uchaguzi huo kwa kufanya yafuatayo...
Tufafanulie kwanza kura bandia kwenye mabegi zilikuwa za Nini? Tufafanulie kabla ya kupiga kura, tayari CCM Wana wabunge 80 wa kupita bila kupingwa maana yake nini? Fafanua kwanza kurudisha fomu za wagombea ni CCM tu walijua kujaza wapinzani tu ndio hawakujua.
 
Mimi siwaelewi chadema kabisa na watanzania wanaoshabikia hili

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 CHADEMA walitangaza kutokubali matokeo na kuamua kususia kila kitu kilichotokana na uchaguzi huo kwa kufanya yafuatayo.

1. walitangaza kutomtambua raisi
2. Walimzuia mbunge wa nkasi kwenda bungeni
3. walitangza kususia nafasi za ubunge wa viti maalumu
4. Walitangaza kususia ruzuku.

Baada ya kufanya haya
Chama kiligawanyika katika makundi kulingana na maslahi

1. Mbunge wa nkasi alikataa kutii na kuwaeleza kuwa yeye alichaguliwa na wananchi wa nkasi hivyo alikwenda bungeni kuwawakilisha wananchi wa nkasi.

2. Wanawake waliotegemea nafasi za viti maalumu walikataa hoja za kususa kwa hoja kwamba msiamo wa chama chaguzi zote umekuwa wa kukataa matokeo, kipindi hicho viongozi walipokuwa wakipata nafasi za ubunge hawakuleta hoja za kususia fursa hizo ila baada ya kukosa wanataka kila mtu asuse.

Wanawake waliona kama kuna doble standard katika maamuzi na hivyo kuamua kutosusia nafasi za ubunge wa viti maalumu. Hapa Chadema walianzisha mchakato wa kuwatimua bungeni kwa kwanza kudai hawajawateua, hoja hii ilipogonga ukuta wakawafukuza chama kwa kutegemea watakuwa wamekosa sifa za kuwa wabunge.

3. Viongozi wa juu wa chama, Mwenyekiti pamoja na Makamu mwenyekiti wamekutana na raisi mara kadhaa ikiwemo kwenda ikulu. hii inaonyesha viongozi wa juu nao wametupilia mbali msimamo wa kutotambua matokeo ya uchaguzi.

4. Chama kumwandikia spika wa bunge barua ni sawa na kutambua pia matokeo ya uchaguzi kwa maana kama hutambui matokeo ya uchaguzi na kitu chochote kilichotak kwenye matokeo ya uchaguzi huwezi kumwandikia "official letter" mtu anayeshika wadhifa uliotokana na matokeo ya kura.

Lakini yote bin yote ni hii hatua ya CHADEMA kutafuta serikali / Bunge kuwaunga mkono wao waliosema hatutambui matokeo ya uchaguzi na fursa zitokanazo na matokeo ya uchaguzi kwa kuwafukuza wabunge 19 ambao wao walikaa upande wa serikali na bunge kwa kutambua kila kitu na kuchukua fursa.

Je, inawezekana serikali ikawaunga mkono kwenye kivuli cha katiba inavunjwa?

Je, katiba inawapa ruhusa wanachadema kugoma na inawanyima ruhusa baadhi ya wanachadema kukataa kugoma?

Je, mwenyekiti anavyokwenda ikulu kuzungumza na mama wakati chama kilishatoa msimamo wa kutotambua serikali, je naye anatakiwa kuchukuliwa taratibu za kinidhamu na chama?
1655972422838.png
 
Naona mna amplify kutotambua matokeo kama issue kuubwa wakati kikatiba sii chochote inabaki kuwa dhana tu ya kuonyesha kutokuridhishwa na kilichotokea. Katiba inasema matokeo ya Rais hayapingwi mahakamani, kitendo cha chama cha upinzani kupinga matokea hayana mashiko yoyote wala hayazuii Rais kuwa Rais sasa leo mnasema CDM akubali matokeo kwani yanaongeza au kupunguza nini? Tafakari na tuache siasa zisizo na mashiko.
 
Back
Top Bottom