Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Mungu Ibariki Chadema
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwamba wanayosema siyo kweli?Hizo kiki zao zilishapitwa na wakati!
Wakiacha mbinu gani unashauri watumie mbadala wa hii?Ni ama acheni au badilisheni mbinu.
Barabaran ataingia Mbowe tu akamatwe lkn sio kenge ww!!Hakuna uchaguzi hapa ningeshauri kesho watu tuingie barabarani kwenye maandamano
Hii ni dalili mbaya kwa uchaguzi wa 2025. Wahusika wajirekebishe haraka vinginevyo hali itakuwa tete 2025.TAARIFA KWA UMMA
Matukio mbalimbali ambayo yametolewa taarifa mpaka muda huu wa saa nne kamili asubuhi, leo tarehe 27 Novemba, 2024 siku ya kupiga kura, uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Mauaji
Tumepokea taarifa za viongozi wetu kuuwawa usiku wa kuamkia leo kama ifuatavyo:
1. Jimbo la Manyoni Mashariki
Katika Kata ya Mkwese ,Kitongoji Cha Stand, Jana usiku mgombea wetu wa nafasi ya Uenyekiti Kitongoji Cha Stand alivamiwa nyumbani kwake na watu waliofahamika kuwa makada wa CCM ndipo ukatokea mzozo mkubwa, Polisi walifika nyumbani kwake na kumpiga risasi ndugu George Juma Mohamed na kufariki Dunia.
2. Jimbo la Tunduma
Usiku wa kuamkia leo Kiongozi wetu Steven Chalamila, alivamiwa nyumbani kwake usiku na kukatwakatwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na umauti kumkuta.
Karatasi za kura kukamatwa
1. Chato
Karatasi za kupigia kura zimekamatwa Kata ya Nyaruntembo, Kijiji cha Nyantimba, kituo Cha kupigia kura Nyantimba maboksi 6 yenye kura ambazo zimeshapigwa tayari Kwa wagombea wa CCM zimekamatwa kituoni hapo na wananchi. Polisi wamefika na kuwakamata Viongozi wetu na wameondoka na maboksi hayo yenye kura ambazo zilishapigwa tayari.
2. Bariadi Mjini
Kata ya Malambo,Mtaa wa Nyashanda, zimekamatwa kura ambazo tayari zilishapigwa kwa mgombea wa CCM wa mtaa huo.
3. Msalala
Kata ya Bugarama, Kijiji Cha Igudija, mpaka saa nne asubuhi hawajaanza. Kupiga kura kwani hakuna karatasi za kura za nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji na kwenye vitongoji karatasi zimechanganywa za kitongoji A kupelekewa kitongoji B, mfano Kitongoji Cha Isaka zimepelekwa za kitongoji Cha Igudija.
4. Jimbo la Kilosa
Kata ya Dumila, Kijiji cha Dumila zoezi la kupiga kura halijaanza mpaka saa nne asubuhi sababu hakuna karatasi za kura nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji.
5. Jimbo la Kibaha Mjini
Kata za Tangini, Pangani na Msangani mitaa yote mawakala wametolewa na Polisi na kura zilizopigwa kuingizwa na zikajazwa kwenye boksi la kura. Mtaa wa Machinjioni Msimamizi wa Uchaguzi alifika na kura zilizopigwa na zikajazwa kwenye boksi na wakala wetu amekamatwa na Polisi. Mtaa wa Kwa Mathiasi masanduku yenye kura zilizopigwa yamekamatwa na mawakala wetu, Polisi (OCD) na Mkurugenzi wa Halimashauri wamefika na kuyachukua na kusema mawakala wetu wameharibu uchaguzi na hivyo wamewakamata.
Mwenyekiti wa chadema Mkoa wa Pwani Bumija Senkondo amekamatwa yupo ndani Polisi mamlaka ya Mji Kibaha baada ya kukamata masanduku ambayo tayari yamepigwa kura Kata ya Mkuza -Kibaha
6. Jimbo la Igunga
Mawakala wetu wamekamata kura zilizopigwa tayari zaidi ya 200
6. Jimbo la Segerea
Kata ya Kisukuru, Mtaa wa Kuhanga karatasi za kupigia kura zimepelekwa Mtaa wa Chanika, Jimbo la Ukonga. Daftari la wakaazi lililopo kituoni hapo ni la mtaa wa Mianzini badala ya Luhanga. Polisi wameitwa na wapo kwenye kituo hicho.
Mosi, Tunalaani matukio ya mauaji yaliyotokea na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua mara moja za kuwakamata na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wote.
Pili, tunaitaka TAMISEMI itoe maelezo kwa umma kuhusu kura ambazo tayari zimeshapigwa kwa wagombea wa CCM maeneo mbalimbali ya nchi na itachukua hatua zipi dhidi ya wasimamizi wa uchaguzi kwenye maeneo hayo.
Tatu, kwenye maeneo ambayo karatasi za kura hazijafikishwa, tunaitaka TAMISEMI ipeleke karatasi hizo na kuongeza muda wa kupiga kura ili wananchi waweze kutimiza haki yao ya kupiga kura.
Nne, vituo vyote ambavyo mawakala wetu wamekamatwa na Polisi, zoezi la kupiga kura lisimame ili tuweze kuwa na mawakala wetu.
John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje
View attachment 3163015View attachment 3163016