CHADEMA yahamishiwa Ubelgiji na Mtandaoni

CHADEMA yahamishiwa Ubelgiji na Mtandaoni

ACT inakuja kwa kasi na mipango thabiti. Wao wamebaki space za Maria kila siku. Hivi mwananchi wa kawaida wa Tandahimba asiyekuwa na pesa ya kula hayo mambo ya space anayajulia wapi? ACT wao wanaenda vijijini wanaibua changamoto za wananchi na kuzipazia sauti.
ACT ni tawi la CCM wanaweza kwenda popote bila bugudha, cdm wakithubutu kwenda kwa watu na kuibua shida zao, watakamatwa na kuambiwa wanaleta uchochezi. Utasikia viongozi wa maeneo husika wakisema cdm waache kuleta siasa kwenye kila jambo, na waache waliochaguliwa wawatumikie wa kwani huu sio muda wa kampeni.
 
JIFANYA ZOMBI TU.. umesahau ANC walitafuta uhuru wa nchi yao wakiwa nnje ya nchi yao na wengi walikuwa hapahapa TZ tukiwasadia kujitoa kwenye makucha ya wakoloni hivo acha kujizombika acha akili za LUMUMBA zisikutawale ubongo wako
Sasa wale walikuwa wanatafuta uhuru ila hawa wanatakakufanya uhuni tu
 
Hata huko kwenye mtandao wa Maria space, wana ccm wamewafuata huko huko na wamevurugana wao kwa wao. Kwenye hiyo mitandao CDM imebakiza watu watatu tu ambao ni Lissu, Lema na Heche tu. Watu kama akina Msigwa na Sugu walishajitoa.

Hiyo ndiyo namna chadema ilivyokufa.
Sindo vizuri,CCM 2025 watapata kura za kutosha, Chadema kimekufa,,,,,furahi Sasa[emoji1]
 
Ndugu Siasa ni akili, hebu rudia ulichoandika. ANC walikuwa hawaruhusiwi hata kuwa wanachama wa chama cha kisiasa, Chadema kina Maofisi yake viongozi wake kila mkoa, Iko tofauti kubwa sana kati ya CDM na ANC. Hata wewe ni mwanaCDM lakini hakuna anyekukatalia kushabikia chama chako.
Akili zako zikirudi utajitambua
 
Ninapenda kwanza kutoa heshima zangu kwa Mheshimiwa Mbowe, aliyekuwa kizuizini, kwa kuonewa na bila kupewa haki yake kama sheria inavyosema.

Nikirudia mada yangu, hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa, kutoka mikoni mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake, na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni haswa kwenye kipindi cha MARIA SPACE.

Hili jambo linazungumzwa sana na limewabughudhi sana wengi wetu, kwani Chadema ni mali ya watanzania na kina manufaa kwa waliomo na wasiokuwemo, inaumiza kuona Chama kimetekwa Nyara.

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa CHADEMA, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyum



Ruhusini mikutano ya hadhara alafu muone kama watu watakwenda kwenye space. Mikutano ya ndani tu mnawaingilia, wamekwenda kwenye space inakuwa nongwa. MNATAKA WAKAE KIMYA?
 
Hili sahihi kbs!
Mkuu Mkirindi, kumbe na wewe uko kundi langu la wazee wa mwaka 47! Dunia sasa imeshift kutoka physical world kwenda cyber world, hivyo kila kitu sasa ni kimehamia mitandaoni, hivyo Chadema are right, ila wanapaswa kuanzisha its own space. Jana nilitembelea web site ya Chadema, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Official Website nilikuta last update ya habari ilifanywa November 2019! sasa kila kitu ni kwa twitter tuu!. This is wrong!

Kwa vile sasa kila kitu kimehamia mitandaoni, na chadema kinajingamba kwa matumizi ya mitandao, then kitu cha kwanza tulitegemea kuona Chadema inafanya ni kuwa na website live interactive, ukiingia tuu unakuta kila kitu!

P
 
Ninapenda kwanza kutoa heshima zangu kwa Mheshimiwa Mbowe, aliyekuwa kizuizini, kwa kuonewa na bila kupewa haki yake kama sheria inavyosema.

Nikirudia mada yangu, hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa, kutoka mikoni mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake, na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni haswa kwenye kipindi cha MARIA SPACE.

Hili jambo linazungumzwa sana na limewabughudhi sana wengi wetu, kwani Chadema ni mali ya watanzania na kina manufaa kwa waliomo na wasiokuwemo, inaumiza kuona Chama kimetekwa Nyara.

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa CHADEMA, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyumbayumba.
You bear eyes but not the sight, as a blind fellow who says: "I see". "Walioko Ubelgigi na mitandaoni siyo wanachama vile?"
 
Sindo vizuri,CCM 2025 watapata kura za kutosha, Chadema kimekufa,,,,,furahi Sasa[emoji1]
Kila kipindi kina zama yake. Hivi vyama vyote huja na baadaye hupita/hufa. Kulikuwa na zama za NCCR miaka ya 1990s chini ya Mrema, ilitikisa sana kama chama kikuu cha upinzani. Zama zake zikapita. Ikaja zama za CUF miaka ya 2000s ikajizolea wabunge wengi sana hadi kuunda kambi yake rasmu ya upinzani. Zama zake zikapita. Zikaja zama za CHADEMA miaka ya 2010s nayo ikawa kambi rasmu ya upinzani baada ya kujizolea wabunge wengi kwa jotihada za Padri Dr Silaa. Nayo zama zake zimeshapita. Sasa hivi hakuna kambi rasimu ya upinzani ila ACT angalao ina wabunge takribani 10 wakati CDM wana zero. Matarajio ACT itakuwa kambi rasmu ya upinzani ifikapo 2025 au 2030.

Hiyo ndiyo nature ya vyama vya siasa. Hakuna kinachoishi milele. Hata CCM zama zake zitapita. Inatarajiwa miaka ya2050s zama za CCM nazo zitafika mwisho. Hayo ndiyo maisha. Hakuna haja ya kuendelea kulilia kitu kilichopita/ kichokufa. Maisha lazima yaendelee. Wahenga walisema yaliyopita si ndwele tugange yajayo.
 
Mkuu Mkirindi, kumbe na wewe uko kundi langu la wazee wa mwaka 47! Dunia sasa imeshift kutoka physical world kwenda cyber world, hivyo kila kitu sasa ni kimehamia mitandaoni, hivyo Chadema are right, ila wanapaswa kuanzisha its own space. Jana nilitembelea web site ya Chadema, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo- Official Website nilikuta last update ya habari ilifanywa November 2019! sasa kila kitu ni kwa twitter tuu!. This is wrong!

Kwa vile sasa kila kitu kimehamia mitandaoni, na chadema kinajingamba kwa matumizi ya mitandao, then kitu cha kwanza tulitegemea kuona Chadema inafanya ni kuwa na website live interactive, ukiingia tuu unakuta kila kitu!

P
Absolutely true mkuu Paskali.
 
Ninapenda kwanza kutoa heshima zangu kwa Mheshimiwa Mbowe, aliyekuwa kizuizini, kwa kuonewa na bila kupewa haki yake kama sheria inavyosema.

Nikirudia mada yangu, hivi karibuni tumeona kuwa shughuli zote za hiki chama kikubwa cha upinzani zikihamishwa, kutoka mikoni mwa Ofisi zake za kisheria na mikononi mwa Viongozi wake, na kuhamishiwa kwa wale viongozi waliokimbia nchi kwa usalama wao, na pia kuweka makao makuu ya chama mitandaoni haswa kwenye kipindi cha MARIA SPACE.

Hili jambo linazungumzwa sana na limewabughudhi sana wengi wetu, kwani Chadema ni mali ya watanzania na kina manufaa kwa waliomo na wasiokuwemo, inaumiza kuona Chama kimetekwa Nyara.

Inashangaza sana kuona wale wazee muhimu na wenye busara wa CHADEMA, wamekaa kimya huku wakiona Chama kikiyumbayumba.
Makao makuu ya ANC ya Afrika Kusini yalikuwa Tanzania, makao makuu ya FRELIMO yalikuwa Tanzania na Uhuru ulipatikana.
 
Sasa CCM mpewe nini mridhike? Hamna pema kabisa. Mliiona chadema tishio, mkatumia dola kujaribu kuwanyamazisha. Wamekaa pembeni, wakawaacha mfanye mnavyotaka, viongozi wake kede kede mkawatengenezea kesi za uongo, na wengine mkawapa kesi za ugaidi ili wasiwepo uraiani wakiwabughudhi. Bado mnachonga tu. Aisee, MaCCM hadi ibilisi atawashangaa!
 
Pamoja na hayo yote, bana wanakunyima raha, wanakupa hofu.
 
Makao makuu ya ANC ya Afrika Kusini yalikuwa Tanzania, makao makuu ya FRELIMO yalikuwa Tanzania na Uhuru ulipatikana.
Uliowataja makao makuu yao yalikuwa Tanzania kwakuwa hawakuruhusiwa kuwa na ofisi huko kwao.

Inawezekana wakati wa Magufuli maisha ya Lema yalikuwa hatarini akiwa Tanzania. Don't tell me that Lema akiamua kurudi nyumbani leo maisha yake yatakuwa hatarini.

These fellows are riding on the backs of fools like you.
 
ACT ni tawi la CCM wanaweza kwenda popote bila bugudha, cdm wakithubutu kwenda kwa watu na kuibua shida zao, watakamatwa na kuambiwa wanaleta uchochezi. Utasikia viongozi wa maeneo husika wakisema cdm waache kuleta siasa kwenye kila jambo, na waache waliochaguliwa wawatumikie wa kwani huu sio muda wa kampeni.
Mtabakia kusema hive wensen wanafanya siasa za masuala nyie mnafanya siasa za face book.
 
Back
Top Bottom