LGE2024 CHADEMA yatoa tamko baada ya Freeman Mbowe kukamatwa na Jeshi La Polisi

LGE2024 CHADEMA yatoa tamko baada ya Freeman Mbowe kukamatwa na Jeshi La Polisi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Jeshi la Polisi leo tarehe 22 Novemba, 2024 katika Pori la Halungu lililopo Wilaya ya Mbozi wamevamia Msafara na kumkamata Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na Viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao.

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama Taifa ulikuwa umeshafanya Mikutano ya kampeni katika Kata ya Itaka, Kijiji Cha Itewe na Kata ya Halungu Mjini.

Awali mkutano wa kwanza uliokuwa ufanyike katika mji wa Mlowo uliozuiliwa na Polisi pamoja na wenyeji wetu ambao ni Chama Cha ACT Wazalendo kutualika kushiriki kwenye mkutano wa pamoja ila Polisi walikataa na kutawanya wananchi Kwa mabomu ya machozi.

Kabla ya kuwakamata walifuatwa na gari ya Polisi ambayo ilikutana nao njiani na hivyo iligeuza na baada ya mwendo kidogo walikuwa njia imefungwa na gari za polisi ndipo walipofungua milango Kwa nguvu na kuanza kuwashambulia waliokuwa kwenye Magari hayo na kuwakamata Kwa nguvu.Waliokamatwa ni:

1. Mhe.Freeman Mbowe
2. Mhe. Joseph Mbilinyi - Mwenyekiti Kanda ya Nyassa
3. Mhe. Pascal Haongo- Mbunge wa Mbozi mashariki Mstaafu
4. Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi
5. B Appolinary Boniface - Mkuu wa Digital platform
6. Paul Joseph - Afisa habari Kanda ya Nyassa6. Calvin Ndabila - Afisa habari Kanda ya Nyassa
7. Mdude Nyagali - Mwanaharakati na mwanachama wetu
8. Wasaidizi wa Mwenyekiti wa Chama Taifa Bwire, Adamoo na Lingwenya


Jeshi la Polisi wameondoka na viongozi wetu na hajajasema wanawapeleka wapi na mpaka Sasa hatujui wanashikiliwa wapi na Kwa sababu gani.

CDM.jpg


CDM 2.jpg

Soma Pia:
 

Attachments

  • CDM.jpg
    CDM.jpg
    581.7 KB · Views: 1
  • CDM.jpg
    CDM.jpg
    581.7 KB · Views: 1
Wakuu,

1732284754158.png

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kuwa viongozi wake akiwemo Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe pamoja na Mwenyekiti wa Kanda ya Nyassa Joseph Mbilinyi (SUGU) pamoja na wanachama wengine wamekamatwa na Jeshi la polisi mkoani Songwe.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje John Mrema imeleza kuwa viongozi hao wamekamatwa leo Novemba 22 katika Pori la Halungu lililopo wilayani Mbozi.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa polisi walivamia msafara na kumkamata Mbowe pamoja na viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao. Viongozi waliokamatwa wengine ni pamoja na Pascal Haongo ambaye ni Mbunge wa Mbozi Mashariki mstaafu na Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi Ezekia Zambi.

Wengine waliokamatwa ni Appolinary Boniface Mkuu wa Digital platform, Paul Joseph na Calvin Ndabila ambao ni maafisa habari Kanda ya Nyassa, Mwanaharakati Mdude Nyagali pamoja na wasaidizi wa Mbowe ambao ni Bwire, Adamoo na Lingwenya.

Hata hivyo CHADEMA imelaani kitendo cha kukamatwa kwa viongozi hao huku ikitoa wito kwa jumuiya za kimataifa kushirikiana nao kwa kile walichokiita uvunjifu wa kidemokrasia.

Jambo TV imefanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Agustino Senga hata hivyo kupitia afisa habari wa Jeshi la polisi mkoani humo amesema kuwa watatoa taarifa rasmi baadae.
 
Nimeona hapo wametajwa makomandoo wa chadema...ADAMOO, BWIRE, LINGENYWA.

NIMEMKUMBUKA COMMANDO MARTIN ALIE TUPWA SIJUI WAP..

Aisee kua mpinzani ni ngumu Sanaa nchi hii.
 
Hadi wavunja tofali wastaafu wana enyeshwa
 

Attachments

  • Screenshot_20241122_172440_Instagram.jpg
    Screenshot_20241122_172440_Instagram.jpg
    154.3 KB · Views: 2
CHADEMA ni wapumbavu. Hayo mazungumzo yasiyokuwa na kibali cha polisi ni uvunjifu wa amani. ACT ndo wanatoa vibali vya mikutano siku hizi? Waache utoto.
 
Jeshi la Polisi leo tarehe 22 Novemba, 2024 katika Pori la Halungu lililopo Wilaya ya Mbozi wamevamia Msafara na kumkamata Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na Viongozi mbalimbali aliokuw...
Hadi wavunja tofali wastaafu wana enyeshwa
Ccm wana hofu na CHADEMA bila sababu za maana
Watatuletea shida kubwa sana mwakani hawa watu
Hayo mnayataka nyinyi wenyewe Watu wa Chadema.
Chadema tambueni kwamba mpo vitani, kulalamika tu kwa maneno matupu haitwasaidia kitu. Chukueni hatua madhubuti ili kukomesha udhalimu huo mnaofanyiwa, tumechoka kusikia malalamiko yenu ya maneno matupu miaka yote.
Ikiwa Kama Ccm inatumia majeshi yake ya Polisi na Tiss, Je, na nyinyi nao mnashindwa Nini kutumia ya kwenu???


"The right cannot be given as a gift by the oppressor, it must be demanded by the oppressed."

Dr. Martin Luther King Jr.
 
Ipo siku hii mchi inaweza kushuhudia mauaji ya halaiki kwa upumbavu wa watu wachache.

Nawaza tu kama chadema na wafuasi wake wangeamua kupambana na polisi ingekuwaje.

Tutumie busara sana kbla hata ya sheria. Utu na utaifa wetu ni muhimu kuliko maslahi ya kisiasa mnayopigania.
 
Jeshi la Polisi leo tarehe 22 Novemba, 2024 katika Pori la Halungu lililopo Wilaya ya Mbozi wamevamia Msafara na kumkamata Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na Viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao.

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama Taifa ulikuwa umeshafanya Mikutano ya kampeni katika Kata ya Itaka, Kijiji Cha Itewe na Kata ya Halungu Mjini.

Awali mkutano wa kwanza uliokuwa ufanyike katika mji wa Mlowo uliozuiliwa na Polisi pamoja na wenyeji wetu ambao ni Chama Cha ACT Wazalendo kutualika kushiriki kwenye mkutano wa pamoja ila Polisi walikataa na kutawanya wananchi Kwa mabomu ya machozi.

Kabla ya kuwakamata walifuatwa na gari ya Polisi ambayo ilikutana nao njiani na hivyo iligeuza na baada ya mwendo kidogo walikuwa njia imefungwa na gari za polisi ndipo walipofungua milango Kwa nguvu na kuanza kuwashambulia waliokuwa kwenye Magari hayo na kuwakamata Kwa nguvu.Waliokamatwa ni:

1. Mhe.Freeman Mbowe
2. Mhe. Joseph Mbilinyi - Mwenyekiti Kanda ya Nyassa
3. Mhe. Pascal Haongo- Mbunge wa Mbozi mashariki Mstaafu
4. Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi
5. B Appolinary Boniface - Mkuu wa Digital platform
6. Paul Joseph - Afisa habari Kanda ya Nyassa6. Calvin Ndabila - Afisa habari Kanda ya Nyassa
7. Mdude Nyagali - Mwanaharakati na mwanachama wetu
8. Wasaidizi wa Mwenyekiti wa Chama Taifa Bwire, Adamoo na Lingwenya


Jeshi la Polisi wameondoka na viongozi wetu na hajajasema wanawapeleka wapi na mpaka Sasa hatujui wanashikiliwa wapi na Kwa sababu gani.

Soma Pia:
hata watoe maelezo marefu na yenye hisia kali namna gani, hawataruhusiwa kuleta fujo na kuvuruga ratiba ya mikutano ya kisiasa ambayo tayari jeshi la polisi nchini wanayo na ndiyo wanayoisimamia na kujipanga kuilinda.

Kinyume na hivyo itatambulika kama uchochezi na uvunjifu wa amani kitu ambacho kama Taifa, tutailinda amani ya Tanzania kwa nguvu na gharama yoyote ile.

Fuateni utaratibu wa kampeni ambao upo bila kuathiri shughuli na ratiba za watu wengine.

ikiwa kuna mabadiliko ya mikutano au makubaliano na chama kingine cha siasa, bas jeshi la polisi nchini, linafaa kuarifiwa siku tatu kabla.🐒

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Mimi misingewakamata

Kuwakamata ni sawa na kuwasaidia kupiga kampeni tena nchi nzima Bure Kwenye TV na mitandao yote ya kijamii

Siasa ni sayansi 🐼
 
Back
Top Bottom