Haya ni maandalizi ya kukusanya sadaka.
Soon mtashangaa Mbowe aliwezaje kuongoza Chama kisichokuwa na pesa.
These are the thoughts indicted with ignorance of high degrees....!
Lakini ajabu nyingine ni kuwa wewe unajiita ni
Dr Matola PhD tena mwenye PhD. Labda hii yako bila shaka ni PhD ya ujinga na ujinga wako uko justified na hoja na fikra zako hizi...!!
Kwanini udhani kuwa vyama vya siasa vya siasa vinaweza kujiendesha na kugharamiwa na fedha za tajiri mmoja au matajiri wachache wenye nia ya kuhodhi mamlaka ya maamuzi ya chama kwa nguvu na kwa sbb ya pesa zao wanazotoa..? Kwanini unadharau sadaka ya kila mwanachama?
Kumbe wewe
Dr Matola PhD mwenye fikra na dhana hii iliyobeba ujinga ndani yake ikitokea ukapewa chama kama CHADEMA, basi haina shaka yoyote kuwa, unaweza kukiuza kwa matajiri mapema asubuhi tu....
Kama ulikuwa hujui ni kuwa, ndiko ilikokuwa inaelekea CHADEMA kama kusingefanyika intervention ya haraka kama ilivyofanyika sasa....
Ni bahati mbaya tu kuwa, hata hizo fedha alizokuwa anazitoa Freeman Mbowe kugharamia baadhi ya shughuli za chama wala hazikuwa zake, bali naye alikuwa anapewa na matajiri wa CCM wenye mapesa ya wizi na ufisadi serikalini...
Na wewe unafikiri nini juu ya CCM? Kwamba ni chama cha wanachama wote wa kawaida? Thubutu...!
CCM ni chama cha matajiri. Wao ndio huamua nani awe nani na kamwe sio maamuzi na utashi wa wanachama. Tukio la juzi Dodoma kwa Bi Samia kujiteua kuwa mgombea u - Rais ni uthibitisho wa hili. Na unajua kilitokea nini wanachama wa kawaida walipojaribu kuhoji..?
Kama hujui, nenda Moshi Kilimanjaro kamuulize Mch Malisa au kamuulize Kibajaji yule mbunge wa Dodoma (sikumbuki jimbo lake)..
Na umeshawahi kujiuliza swali hili kuwa, iwapo CCM ikipoteza dola leo, kitaishi vipi? Unadhani kitaendelea kuwepo au ndio itakuwa mwisho wake? Unajua KANU iko wapi sasa? Unajua ZANU ya Zambia ya Kennedy Kaunda iko wapi sasa? Au unadhani hatujui kuwa maisha ya CCM ni kwa sababu inatumia fedha na rasrimali za serikali na siku ikitoka tu ktk mkondo huo ndo itakuwa mwisho wake..?
Dr Matola PhD chama cha siasa ni watu (wanachama) na kwa nguvu zao kwa umoja wao, watakiendesha chama kwa michango kidogo kidogo ambayo wewe unaiita "sadaka". Hii ndiyo sifa ya chama cha siasa halisi...!
Kama unafikiri CHADEMA itakufa kwa sababu matajiri wanaotaka kukinunua chama wamefungiwa milango, basi utabaki kuota hivyo hivyo, mara pa mwana si wako....
Kwa heri, usiku mwema...πΆπ»πΆπ»πΆπ»πΆπ»πΆπ»