Chagua Kimoja unachohisi ndicho 'Kimemgharimu' Mtani wangu wa Kihaya Balozi Mulamula na Kutumbuliwa

Chagua Kimoja unachohisi ndicho 'Kimemgharimu' Mtani wangu wa Kihaya Balozi Mulamula na Kutumbuliwa

Naona number tatu na number nne kuna Lojik hapo kwa kauli ya Mh Rais mwenyewe leo wakati akiwaapisha Mawaziri
 
Na Wewe Mtani wangu wa Kihaya Balozi Mulamula yaani umepata access ya kupiga Picha na hawa Viongozi Wakubwa wa Dunia wakati 'Boss' wako alitoswa na access ya Kiurahisi aliyoipata ni Kudandia tu 'Dala Dala' London akiwa na Kondakta wake Hustler wa Jirani...!!!!

Kwa Picha yako hii hata Mimi Mpanda 'Dala Dala' la London na Kuwahi Dirishani GENTAMYCINE ningekutumbua tu.

Huna Adabu kabisa.......
Kweli mkuu, ile picha na Biden na Kamara
lazima Mama amaindi kinoma,
Hustler wa jirani hata angeambiwa awe konda wa basi poa tu, ndio maana alikuwa anacheka,
 
1. Exposure yake Kubwa Kimataifa

2. Kiburi cha Elimu na Akili Kubwa kutoka kwa Kabila lake

3. Kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu

4. Kutopenda Unafiki na Kujipendekeza kama walio wengi

5. Kutokuwa Muumini wa Uswahili Uswahili ( Uenyeji Uenyeji ) wetu Watu wa Pwani ya Bahari ya Hindi

6. Kuchoshwa na Majungu

7. Kukemea Mambo ya Kiitifaki ambayo mengine yatamuaibisha Mtu na hata Watanzania wengine wote

Nawaamini Great Thinkers wa JamiiForums na naamini hapa mtatiririka na kuserereka vyema juu ya hili na Kuchagua Jibu lako moja tu unaloliona ni sahihi Kwako.
Mwenye picha ya Mama na Baiden tunaomba tafadhali
 
nadhani moja kubwa ni ile kissing ya Msumbiji (alileta uswahili mwingi sana) kiitifaki haikuwa sawa so nadhani mama baada ya kuambiwa ukweli kuwa alikiuka protocali akachukulia personal. Lakini pia na wivu kwa maana kwa hiyo picha ya balozi na Biden ni wazi balozi amemu outshine bishosti kinamna fulani hivi na ni kama ameisema kwenye uapisho wa wateuluwa leo. Ila pamoja na yote the outstanding CV ya waziri ilikuwa inamfanya bishosti kuwa inferior to some extent, yaani ni kama hakuwa na chakumueleza kuhusu diplomasia n international relationship
 
Kwahiyo Stergomena ndiyo anaandaliwa kuja kuwa Rais wa Tanzania hii ambayo GENTAMYCINE naiishi?

Mwisho wa Tanzania Kuongozwa na Mwanamke ni ana mwaka 2025 au mwaka 2030 tu na si vinginevyo halafu msithubutu kutaka Kulazimisha vinginevyo Wanaume tutaamka na patachimbika.
2025 tu Wanaume halisi tutaliamsha labda tusalitiwe na chawa.
 
1. Exposure yake Kubwa Kimataifa

2. Kiburi cha Elimu na Akili Kubwa kutoka kwa Kabila lake

3. Kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu

4. Kutopenda Unafiki na Kujipendekeza kama walio wengi

5. Kutokuwa Muumini wa Uswahili Uswahili ( Uenyeji Uenyeji ) wetu Watu wa Pwani ya Bahari ya Hindi

6. Kuchoshwa na Majungu

7. Kukemea Mambo ya Kiitifaki ambayo mengine yatamuaibisha Mtu na hata Watanzania wengine wote

Nawaamini Great Thinkers wa JamiiForums na naamini hapa mtatiririka na kuserereka vyema juu ya hili na Kuchagua Jibu lako moja tu unaloliona ni sahihi Kwako.
Kwahiyo ktk majibu hayo lipo lilithibitika ni sahihi?Je kama najuwa zaidi ya hayo?
 
Tutasea mengi ila hakuna anayejua kilicho chini ya sufuria au whatever mimi sifui.
Samia amekaa na Libe na amemwona kazi yake. There are two types of persons those who can talk and the dos ones. Mimi siwezi kumweka popote sababu amekuwa nje ya nchi ambayo mimi nipo. Pia namfahamu personally.
Nchi inahitaji mtu agressive kwenye mambo ya kimataifa. Haya mambo ya juzi it is only ignorant and lack of exposure persons can think of that. Wakati rais magufuli anaapishwa viongozi wa UN na mashirika mengine na mabalozi wa Tz walipelekwa kwenye mabasi je kwanini ilikuwa vyema huku na vibaya uingereza???
Libe amefanya kazi na mashirika ya EA na mengine hivyo anahitajika mtu ambaye ataongeza chumvi zaidi. Sikupendezwa na jibu alilotoa wakati vita a Ukrane ilipoanza. To be non aligned doesn't mean isolation.

Kukaa kimya ni aina ya utumwa. Tanzania hatukukaa kimya wakati Southafrica wanaonewa, Namimbia, Mozambique tulipiga kelele but we still were non aligned. Kukaa kimya ina maana sisi ni watumwa wa warusi. wakikohoa tunasema ndiyo bwana tamka ndiyo bwana itika ndiyiyo bwana nenda kwao.
Libe alitereza.
 
Alikataa mother kupanda bus la Majinja kule UK kwamba lingeshusha hadhi yake na Taifa kwa ujumla, ndomana hukumuona Kagame akipanda bus kule.
Haaahaha hio si kweli Kagame mwenyewe alipanda basi sema hakupigwa picha tu. Akina Macron na Trudeu walipanda basi hadi wafalme wa nchi za ulaya walipanda mabasi pia. Ni Joe Biden tu ndio aliruhusiwa kwenda na gari.Toa kabisa hio sio sababu, sema vitu vingine ila sio hilo la kupanda basi..NEver!!!
 
Kagame (Rwanda) hayumo kwenye Commonwealth contries
Kagame - Rwanda yumo kwenye Commonwealth na mkutano mkuu wa Commonwealth wa 2022, ulifanyikia Kigali, Rwanda. Na Mfalme wa sasa King Charles alihudhuria huo mkutano, na bongo iliwakilishwa na VP Mpango. Rwanda walijiunga na Commonwealth ingawa walikua Francophone. Na Kagame alipanda basi pia sema hakupigwa picha tu.
 
Kuna Mtu kanidokeza kuwa hili lilimkera zaidi Balozi Mulamula na hakutaka Watu wa Itifaki waliruhusu kwani alishalipima kuwa lingeleta Picha mbaya kwa Boss wake, Taifa na Watanzania ila akapuuzwa.

Sijajua na kama Busu la Msumbiji lilimkera pia huyu Mtani wangu wa Kihaya ambaye ni Zao la Mfumo na pia She's very Intelligent halafu anajiamini vile vile.
Ivi ubunge wake atasalia nao au ndio zindegi mirenaheeee
 
Back
Top Bottom