CHAI Day 5 Feb 2011 Dar: Kujadili fursa katika Kilimo na ufugaji

Mkuu Kanyagio
Nimekutumia mchango wangu around 4.30Pm . nasikitika kusema kuwa wale wageni 2 hawatoweza kuja kwa sababu zilizo nje ya uwezo
 
Asante kwa wazo zuri sana. Mimi pia nitakuwepo.
 
Mkuu kanyagio unaweza kututumia nukuu za kikao cha mwaka jana?
 
Mkuu Kanyagio
Nimekutumia mchango wangu around 4.30Pm . nasikitika kusema kuwa wale wageni 2 hawatoweza kuja kwa sababu zilizo nje ya uwezo

NEW MZALENDO aisee mbona haijaingia? the same applies to ELNINO.. naombeni tusaidiane ku-track hizo hela mlipotumia
 
Mkuu Kanyagio, nathibitisha kuwa nitakuwepo na nitatoa mchango wangu mlangoni. Asante sana kwa juhudi zako.
 
Wakuu,ktk hii chai Day itawezekana kuchukua kumbukumbu kwa video na still pictures?
protokali za kikao kilichopita zilikuwaje?
kama unamaterials za kushare na wenzako tutatumia njia ipi?projector presentation au?
nimeangalia picha ya lunchitme hotel tutakaa mkao wa confrence room au mkao wa kwenye lounge?
 
Mkuu KAMUZU; nimeona umeanzisha thread ukitutaarifu juu ya mkutano wa MEGAWEALTH ambao utaanza saa nane mchana, Je utaweza kuhudhuria mikutano yote kwa wakati mmoja au ile ilikuwa ni taarifa kwa watakao kuwa interested.


Thread sikuanzisha mimi, isipokuwa nilicomment tu mkuu labda hukunisoma vvizuri.


Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
Wakuu this is off topic na chai day,ila inahamasisha ile vision yetu ya kuwa na jamii farm with members owning and managing a farm of 500 acres and above.nimeona hili shamba natamani Jamii Farm tufike hapa na kuzidi hapa hili shamba lipo kilombero linamilikiwa na watanzania na raia wa Canada .wanalima mpunga na mazao mengine,inaonyesha kuna ubia na wakulima wa canada.click ktk maandishi mekundu utaona full details za shamba lao.
kilombero farm
 

kwa kweli Projector tulikuwa hatujaifikiria kwa sababu hatujaandaa specific presentations.. bali watakuwa wanatoa mawazo kwa kila topic zao. ila kutakuwa na facilitator kwa kila mada atakayetoa overview!!

sisi hatujaandaa mtu wa kupiga ila kama unajitolea utaruhusiwa!!

kuhusu ukaaji nitakujibu later!
 
Mkuu Kanyagio, nathibitisha kuwa nitakuwepo na nitatoa mchango wangu mlangoni. Asante sana kwa juhudi zako.

karibu sana LEN

na wengine ambao hawajalipa kwa MPESA mtalipia mlangoni..
 
Baada ya kuangalia ratiba yangu na kujiridhisha kwa kuulizia menejimenti ya Lunch Time Hotel..Nitakuwepo na nitatoa Mchango mlangoni wakuu...!Kumradhi kwa usumbufu utakaotokea!
 
Baada ya kuangalia ratiba yangu na kujiridhisha kwa kuulizia menejimenti ya Lunch Time Hotel..Nitakuwepo na nitatoa Mchango mlangoni wakuu...!Kumradhi kwa usumbufu utakaotokea!

karibu sana mkesha hoi. hapo penye nyekundu umenifurahisha!!! Good
 
wanandugu, katika mkutano wa kesho wa kilimo kuna mada zifuatazo ambazo tunahitaji watakaosimamia majadiliano:

  • Masoko ya mazao ambayo tunahitaji kujadili upatikanaji wa soko la ndani na lile la nje. na pia kujadili kwa ufupi kuhusu kuuzia shambani au kuleta sokoni na madalali.
  • Uanzishaji umoja/kampuni/taasisi- ambayo itajikita zaidi katika kujadili uwezekano wa kuazisha umoja/kampuni yenye tija na faida; Dira, madhumuni, Muundo, Mchakato na mpango kazi wa uanzishaji wa umoja/kampuni
ninaomba sana kama ninaweza kupata volunteer nitashukuru.. mgombezi/mzalendo/mkeshahoi na wengineo tafadhali naombeni mawazo
 
Nitamtuma partner wangu wa biashara niko nje ya nchi, naunga mkono na miguu! Big up kwa idea nzuri!
 
sina uzoefu na sekta hii kwa undani.. Ila baada ya kikombe cha chai hapo kesho nitakuwa nimepata mwanga wa kujua wapi kwa kuanzia ili kusonga mbele kwa manufaa yetu wote.. Tusihofu... There is always a first time for everything mkuu..!!
 
Finally JF imepatikana ,Duh!!
nasubiria chai day kwa hamu kubwa 🙂
 

Mkuu Kanyagio; nakupongeza kwa utayari wako katika kufanikisha CHAI DAY - 2011, sasa yamebaki masaa. Kuhusu mada ambazo tunahitaji wasimamizi wake katika mjadala, naweza kusimamia hili la uanzishaji umoja/kampuni/taasisi.

Wadua wote nawatakia kila la kheri mnapojiandaa kuhudhuria CHAI DAY - 2011, nimeanza safari ya kuelekea huko.
 

mkuu... naomba uwe mwakilishi wangu kwenye CHAI DAY 2011..... ninatuma TZS 10,000 ...sitaweza kuhudhuria kwa ajili ya majukumu mengine nitachangia hoja baada ya kupata muhtasari ..ahsante
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…