Chalamila: Dkt. Janabi alisema sukari ni hatari kwa afya, tumieni fursa ya upungufu huu kuachana nayo msipate magonjwa mbeleni

Chalamila: Dkt. Janabi alisema sukari ni hatari kwa afya, tumieni fursa ya upungufu huu kuachana nayo msipate magonjwa mbeleni

Inamaana mkuu wa mkoa bado hajui kama sukari anayoongeleaga Prof ipo hadi kwenye ugali na wali?
 
Kwavile hakuna umeme , Wananchi tumieni fursa hiyo kulala mapema

JokaKuu

..viongozi wetu hawajali.

..na ukweli huo unajidhihirisha ktk kauli kama iliyotolewa na RC Chalamila.

..kodi zetu zinatumika kulipa mishahara ya viongozi wanaotukejeli.
 
na shida umeme inayoendelea tutaambiwa tuachane na matumizi ya vifaa vinavotumia umeme
 
Nje kidogo ya Mada.

Sukari hii ndio ilitufanya tuwe watumwa katika Nchi za watu wa nje. "Wawekezaji"







Kitu ambacho hakiingi akiliini, ni jinsi tulivyoweza kutosheleza mahitaji ya mabeberu, kwa kifedha na (utumiaji) si chini ya miaka 70 iliyopita.

...duh
 
"Kama hakuna mikate, basi wale keki" alisikika akisema Malkia mmoja kwa watu wake ambao walikuwa wakifa kwa njaa kwa kukosa chakula
 
Na watoto wetu wachanga uji tuwapikie na nini? Nao tuwaambie sukari ina madhara?
Upuuzi mwingine bwana.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam hana akili timamu. Huwezi kumtofautisha na yule aliyewahi kusema wasioweza kulipa 200 pale kivukoni wapige mbizi kuvuka.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam hana akili timamu. Huwezi kumtofautisha na yule aliyewahi kusema wasioweza kulipa 200 pale kivukoni wapige mbizi kuvuka.
Professor Janabi ni vizuri ajikite kuendesha semina Kwa wagonjwa ambao maradhi wakiyonayo Wala hayakutokana na utumiaji Sukari,chumvi,Wanga ,nyama au Mafuta Lakini tiba Yao inahitaji waache hivyo vitu

Asihangaike na watu wazima wenye Afya zao

Ajikite Kwa hao wagonjwa ambao moja ya medical prescription ni kutotumia hivyo vitu asifanye ni universal medical rule

Wagonjwa wengi Tanzania magonnjwa Yao hayasababishwi na hivyo vyakula anapiga vita uongo wanaumwa miradhi mingine ambayo ndio huambiwa na madaktari usalama wenu msile hivyo vyakula vya wanga,sukari ,Mafuta na nyama na chumvi kuleni chukuchuku

Professor Janaba ajikite Kwa hao wagonjwa wake wazingatie medical prescription vinginevyo watakufa Kabla ya muda
 
Chalamila asema ukimsikiliza Dr. Janabi anasema ulaji wa sukari nyingi unasababisha maradhi mengi, kwahiyo wakati huu ambako sukari imeadimika tuachane nayo kabisa ili usiweze kupata matatizo ya afya hapo baadaye.


Kwahiyo serikali imeshindwa kabisa kutatua changamoto hii ya upatikaji wa sukari sasa wanatafuta 'justification' ya ukosefu huo?

Bashe ilibidi uwajibike kwa kushindwa kutatua hili hadi hali imekuwa mbaya hivi.

Pamoja na haya yote bado viongozi mnakula kwa kama zenu na hutasikia posho za wabunge zimepungua, ama wamechukua 'initiatives' za kubana matumizi ili kupunguza makali haya kwa wananchi.

Bure kabisa!
Huyu jamaa sometimes sijui huwa anatumia akili za wapi kufikiria!
 
Mwakilishi wa rais kwenye mkoa anaongea mataptap kama haya!we are finished!
 
Wakati Changamoto ya uhaba wa sukari ikizidi kushika Kasi, viongozi wamekuwa wakinukuliwa kusema watu waachane na matumizi ya Sukari Kwa sababu sio salama kiafya kama ambavyo Mkuu wa Mkoa wa Dar Albert Chalamila amenukuliwa.

Hii ni Kauli ya pili ,ya kwanza ilitoka Kwa Prof.Janabi na kuungwa mkono na Waziri wa Afya.

Swali.Je huu ndio msimamo wa Serikali au msimamo binafsi wa Chalamila na wengine?
Sasa kwa muonekano wa huyo Prof je kweli ni mwenye afya? pamoja na kushindia mchicha anaonekana mgonjwa tu.
 
..viongozi wetu hawajali.

..na ukweli huo unajidhihirisha ktk kauli kama iliyotolewa na RC Chalamila.

..kodi zetu zinatumika kulipa mishahara ya viongozi wanaotukejeli.
RC wetu anajua sukari ni kunywa chai tu, hajui kuna dawa zinatengenezwa kwa sukari. Kuna viwanda vya vinywaji n.k
Kama alivyosema SpiderNyoka, sukari inayoongelewa kiafya si ya miwa tu! Ugali una sukari hivi RC ana habari

Tuna tatizo la Viongozi, huyu asingekuwepo madarakani kwa kauli 'lose' namna hii.
Ni mteule wa Rais na anamwakilisha!
 
Back
Top Bottom