Chama cha Demokrasia na Maendeleo kinaendeshwa kwa fujo na vitisho baridi

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kinaendeshwa kwa fujo na vitisho baridi

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wanabodi,

Mnamo jana, naibu katibu mkuu wa Chama cha demokrasia na maendeleo Bw Benson Kigaila aliongea na vyombo vya habari ambapo aliezea mambo ambayo lazima yatekelezwe ili kama wana CHADEMA, waweze kushiriki vikao ambavyo msajili wa vyama vya siasa amepanga kufanya. Katika mambo ambayo Benson Kigaila aligusia na kusema kwamba lazima yafanyike ni pamoja na



1. Zuio la vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara liondolewe
2. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe aachiliwe
3. Wana CHADEMA wengine ambao wapo mahabusu tofauti nchini waachiwe

Kwanza kabisa, nina amini kwamba haki ya kujieleza ipo kwenye katiba yetu ila jambo ambalo sielewi ni sababu ya vyombo vya usalama kuhusika kwenye kuwa kamata na kuzuia mikutano ya hadhara au mikusanyiko ya aina yoyote inayofanywa na wana CHADEMA. Vile vile bado kesi za Freeman Mbowe na wana CHADEMA wengine walio kamatwa nchini hazija sikilizwa. Kwasababu hizo sidhani kama matakwa ya wana CHADEMA yanatekelezeka haswa katika muda wanaotaka haya yote kufanyika.

Inawezekana kabisa kwa msajili wa vyama vya siasa kuwa na nia nzuri kwa kuchukua hatua hii ya kuzungumza na wahusika wote wakiwemo polisi na wana CHADEMA lakini maswali mengine ya kujiuliza ni kama kweli wana CHADEMA wanataka kufanya maridhiano, kama kweli wanafahamu kwamba matakwa yao hayatekelezeki.

Siasa safi, ambazo kila chama kina wafuasi wake na kila chama kina heshimu maamuzi ya chama kingine ni kitu ambacho kinawezekana na jitihada kama hizi za kujenga mahusiano chanya kati ya washika dau wote ni mwanzo wa hatua njema.

Kama "Chama cha Demokrasia na maendeleo", huwezi kupungukiwa chochote kwa kukaa chini kwa muda usiozidi masaa mawili au matatu kusikiliza maoni ya mtanzania mwenzako aliye upande wa pili.

Inawezekana kwamba wana CHADEMA hawaelewi kuwa maandamano yote na hasira waliyonayo vinaweza kuelekezwa kwa IGP Sirro mezani wakiwa wanaongea naye ana kwa ana na sio kwenye mitandao. Ladba ni kweli, Uanaharakati hauna tofauti sana na ushabiki wa mpira, Chama cha Demokrasia na maendeleo kinaendeshwa kwa fujo na bila mantiki.
 
Nccr mageuzi yaliwakuta haya,Cuf waliyapata mazila haya na sasa Chadema ndio inayopata haya mazila. Inaonesha ccm wanaongopa sana chama kikuu cha upinzani ndio maana hutumia nguvu zote ili kufifisha upinzani. Katiba iliopo sasahivi ni ya ccm sisi tunataka katiba mpya tu. Mbona ccm wana ogopa kuna nini kwani hata waogope katiba mpya?



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Kwanza kabisa acha kusema kwamba CCM wanawa ogopa CHADEMA. Tukili jadili hilo bila upendeleo utagundua kwamba CHADEMA wanahitaji kufanya mengi sana na kwa muda mrefu ili kuweza kupindua meza. Kama chombo kikuu kinacho pigania katiba mpya, mkutano na msajili wa vyama pamoja na polisi labda ungeweza kuwa wa manufaa
 
Yaani Badala ya Rais kuwa ndye host wa mkutano na wapinzani eti Msajiri ? Ofisi ya msajiri imekua ndye chombo cha kutishia upinzani kufanya siasa kikatiba wakishirikiana na POLICE.

Kama kweli Serikali inataka mardhiano kwanini Kikao cha wazi kati ya Rais na wapinzani kisifanyike?

Kwanini nchi hii Upinzani umekua Dhambi Badala ya kuwa chombo cha kuimarsha mshikamano na unyoshaji wa mapungufu ya yafanywayo na wenye Mamlaka ?
 
Nyuki wa mashineni hao, hawana madhara yeyote! Maneno na mikwara miingiiiii, field zero! Chama kikuu cha upinzani makungururu zaidi ya vyote Afrika!
 
Yaani Badala ya Rais kuwa ndye host wa mkutano na wapinzani eti Msajiri ? Ofisi ya msajiri imekua ndye chombo cha kutishia upinzani kufanya siasa kikatiba wakishirikiana na POLICE. Kama kweli Serikali inataka mardhiano kwanini Kikao cha wazi kati ya Rais na wapinzani kisifanyike?Kwanini nchi hii Upinzani umekua Dhambi Badala ya kuwa chombo cha kuimarsha mshikamano na unyoshaji wa mapungufu ya yafanywayo na wenye Mamlaka ?
Jifunze kuandika nawe, "Msajiri" ni mdudu gani?
 
Yaani Badala ya Rais kuwa ndye host wa mkutano na wapinzani eti Msajiri ? Ofisi ya msajiri imekua ndye chombo cha kutishia upinzani kufanya siasa kikatiba wakishirikiana na POLICE. Kama kweli Serikali inataka mardhiano kwanini Kikao cha wazi kati ya Rais na wapinzani kisifanyike?Kwanini nchi hii Upinzani umekua Dhambi Badala ya kuwa chombo cha kuimarsha mshikamano na unyoshaji wa mapungufu ya yafanywayo na wenye Mamlaka ?
Una maanisha rais wa chama cha mpira au wanasheria? Kama ni Rais huyuhuyu wa nchi bas wewe ni mzigo kwa nchi yetu.
 
Nccr mageuzi yaliwakuta haya,Cuf waliyapata mazila haya na sasa Chadema ndio inayopata haya mazila. Inaonesha ccm wanaongopa sana chama kikuu cha upinzani ndio maana hutumia nguvu zote ili kufifisha upinzani. Katiba iliopo sasahivi ni ya ccm sisi tunataka katiba mpya tu. Mbona ccm wana ogopa kuna nini kwani hata waogope katiba mpya?



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
Unaweka Post bila kujua tatizo liko wapi, angalau ungejua hata sheria na kanuni zinazoruhusu vyama vya siasa kufanya siasa nchini, hata hilo haulijui ila unajua kulaumu usilolijua! Fanya utafiti kabla ya kuweka Post ili watu wajadili hoja zako.
 


Unaweka Post bila kujua tatizo liko wapi, angalau ungejua hata sheria na kanuni zinazoruhusu vyama vya siasa kufanya siasa nchini, hata hilo haulijui ila unajua kulaumu usilolijua! Fanya utafiti kabla ya kuweka Post ili watu wajadili hoja zako.
 
Muziki wa Chadema unaowatia wahuni wa maccm nchi nzima hofu kubwa sana.
 
Field ya Cdm ni kwenye ushindani wa hoja za kisiasa, na kwa upande huo wako vizuri. Naona field unayoiongelea ww ni ya kupambana na polisi wenye silaha. Ungewashauri ccm wajitokeze kwenye midahalo na mijadala ya kisiasa ili wawashinde Cdm, na sio vyombo vya dola huku Cdm wakiwa hawana silaha.
kHui wa mashineni hao, hawana madhara yeyote! Maneno na mikwara miingiiiii, field zero! Chama kikuu cha upinzani makungururu zaidi ya vyote Afrika!
 
Kwanza kabisa acha kusema kwamba CCM wanawa ogopa CHADEMA. Tukili jadili hilo bila upendeleo utagundua kwamba CHADEMA wanahitaji kufanya mengi sana na kwa muda mrefu ili kuweza kupindua meza. Kama chombo kikuu kinacho pigania katiba mpya, mkutano na msajili wa vyama pamoja na polisi labda ungeweza kuwa wa manufaa
Wanawaogopa! Wanatumia Polisi
 
Labda
Kwanza kabisa acha kusema kwamba CCM wanawa ogopa CHADEMA. Tukili jadili hilo bila upendeleo utagundua kwamba CHADEMA wanahitaji kufanya mengi sana na kwa muda mrefu ili kuweza kupindua meza. Kama chombo kikuu kinacho pigania katiba mpya, mkutano na msajili wa vyama pamoja na polisi labda ungeweza kuwa wa manufaa
 
Field ya Cdm ni kwenye ushindani wa hoja za kisiasa, na kwa upande huo wako vizuri. Naona field unayoiongelea ww ni ya kupambana na polisi wenye silaha. Ungewashauri ccm wajitokeze kwenye midahalo na mijadala ya kisiasa ili wawashinde Cdm, na sio vyombo vya dola huku Cdm wakiwa hawana silaha.
Nani mwenye hoja kwa CDM hii ya sasa iliyojichokea? CDM walikuwa na hoja kuanzia 2015 na kushuka chini, hii ya sasa wamejaa wapotoshaji, wakurupukaji, wutukanaji, wazushi na wapinga kila kitu! May be Mkiti ila naye hana back up siku hizi, Mnyika since Lowasa alivyopokelewa kapoa sana! Hawa wengine akina Heche, Lema, Msigwa, Sugu, Pambalu, Kigaila, Lissu hamna lolote wajualo zaidi ya kupayuka majukwaani na uongo! I cant believe nimewahi kuwa die hard fan wa Lissu, Lissu viwango vimeshuka sana kwa sasa, na hivi anavyojiexpose kila siku kwenye "vispaces" uchwara vya wasaka tonge ndiyo anazidi kujishushia thamani yake na kuonesha jinsi gani mweupe kichwani! Kiongozi wa chama kikubwa lazima uwe adimu kupatikana, hata kushiriki mijadala mitandaoni lazima upunguze, sababu unachoongea pale watu wanachukulia chama ndiyo kimeongea hata kama siyo!! Mwisho wa siku anaambiwa hana adabu na "mwanaCCM" Fatma
 
Wanabodi,

Mnamo jana, naibu katibu mkuu wa Chama cha demokrasia na maendeleo Bw Benson Kigaila aliongea na vyombo vya habari ambapo aliezea mambo ambayo lazima yatekelezwe ili kama wana CHADEMA, waweze kushiriki vikao ambavyo msajili wa vyama vya siasa amepanga kufanya. Katika mambo ambayo Benson Kigaila aligusia na kusema kwamba lazima yafanyike ni pamoja na



1. Zuio la vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara liondolewe
2. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe aachiliwe
3. Wana CHADEMA wengine ambao wapo mahabusu tofauti nchini waachiwe

Kwanza kabisa, nina amini kwamba haki ya kujieleza ipo kwenye katiba yetu ila jambo ambalo sielewi ni sababu ya vyombo vya usalama kuhusika kwenye kuwa kamata na kuzuia mikutano ya hadhara au mikusanyiko ya aina yoyote inayofanywa na wana CHADEMA. Vile vile bado kesi za Freeman Mbowe na wana CHADEMA wengine walio kamatwa nchini hazija sikilizwa. Kwasababu hizo sidhani kama matakwa ya wana CHADEMA yanatekelezeka haswa katika muda wanaotaka haya yote kufanyika.

Inawezekana kabisa kwa msajili wa vyama vya siasa kuwa na nia nzuri kwa kuchukua hatua hii ya kuzungumza na wahusika wote wakiwemo polisi na wana CHADEMA lakini maswali mengine ya kujiuliza ni kama kweli wana CHADEMA wanataka kufanya maridhiano, kama kweli wanafahamu kwamba matakwa yao hayatekelezeki. Siasa safi, ambazo kila chama kina wafuasi wake na kila chama kina heshimu maamuzi ya chama kingine ni kitu ambacho kinawezekana na jitihada kama hizi za kujenga mahusiano chanya kati ya washika dau wote ni mwanzo wa hatua njema. Kama "Chama cha Demokrasia na maendeleo", huwezi kupungukiwa chochote kwa kukaa chini kwa muda usiozidi masaa mawili au matatu kusikiliza maoni ya mtanzania mwenzako aliye upande wa pili. Inawezekana kwamba wana CHADEMA hawaelewi kuwa maandamano yote na hasira waliyonayo vinaweza kuelekezwa kwa IGP Sirro mezani wakiwa wanaongea naye ana kwa ana na sio kwenye mitandao. Ladba ni kweli, Uanaharakati hauna tofauti sana na ushabiki wa mpira, Chama cha Demokrasia na maendeleo kinaendeshwa kwa fujo na bila mantiki.
Umeandika dude refu lisilo na akili,
Umejiuliza yafuatayo?
1.polisi wanahusika kwenye siasa?
2. Polisi kwanini hawaheshimu katiba badala yake wanaiheshimu ccm tu?
3. Kuwaachia wana chadema waliowabambikia kesi kunahitaji maridhiano gani?

Panasiku polisi na ccm watalipa kwa haya wanayoyafanya kwa wananchi wanaowanyanyasa eti kisha waendelee kubaki madarakani

HAKUNA JAMBO LISILO NA MWISHO

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Nani mwenye hoja kwa CDM hii ya sasa iliyojichokea? CDM walikuwa na hoja kuanzia 2015 na kushuka chini, hii ya sasa wamejaa wapotoshaji, wakurupukaji, wutukanaji, wazushi na wapinga kila kitu! May be Mkiti ila naye hana back up siku hizi, Mnyika since Lowasa alivyopokelewa kapoa sana! Hawa wengine akina Heche, Lema, Msigwa, Sugu, Pambalu, Kigaila, Lissu hamna lolote wajualo zaidi ya kupayuka majukwaani na uongo! I cant believe nimewahi kuwa die hard fan wa Lissu, Lissu viwango vimeshuka sana kwa sasa, na hivi anavyojiexpose kila siku kwenye "vispaces" uchwara vya wasaka tonge ndiyo anazidi kujishushia thamani yake na kuonesha jinsi gani mweupe kichwani! Kiongozi wa chama kikubwa lazima uwe adimu kupatikana, hata kushiriki mijadala mitandaoni lazima upunguze, sababu unachoongea pale watu wanachukulia chama ndiyo kimeongea hata kama siyo!! Mwisho wa siku anaambiwa hana adabu na "mwanaCCM" Fatma

Nimecheka kwa nguvu, eti Cdm walikuwa na hoja 2015 kushuka chini. Maoni haya ni ya wanaccm wote, utasikia huko Cdm aliyekuwa na hoja ni Dr.Slaa, lakini wakati wa Dr. Slaa ndio Cdm ilichafuliwa sana kwa ukristo, uchaga, uongo, fujo, maandamano nk. Hivyo sishangai haya maoni yako ya bendera fuata upepo.
 
Unaweka Post bila kujua tatizo liko wapi, angalau ungejua hata sheria na kanuni zinazoruhusu vyama vya siasa kufanya siasa nchini, hata hilo haulijui ila unajua kulaumu usilolijua! Fanya utafiti kabla ya kuweka Post ili watu wajadili hoja zako.
Wengine wanadhani mambo ya sisa yanafanana na ushabiki wa mpira
 
Back
Top Bottom