Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Chama Cha Majaji na Mahakimu Tanzania Kwa maelezo haya inaonyesha bado mnamuogopa Rostam kwanini kwa sababu;

1. kinamtaka Bw. Rostam Azizi athibitishe kauli yake BILA KUMPA MUDA MAALUM

2. Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule Je AKIKATAA HAMKUONYESHA HATUA ZA KISHERIA ZA KUMCHUKULIA ROSTAM.

Mahakama ninashauri wawe wakali na Huyu jamaa.

 
Nadhani Majaji sasa Watakuwa wamemwandikia Bw Rostam Notisi mahsusi ya maelezo haya ili atekeleze wanachotaka maana ikiwa ni maagizo tu ya kwenye mitandao sijui mhusika atabanwa vipi katika utekelezaji.
 
Kwahio ni wa Kisutu pekee ? Pengine wapo vizuri ? Je ni taasisi gani ipo sawa unless kwenye sawa tunamaanisha sawasawa yaani zote ni yaleyale...
 
Hawamuwezi Rostam,waachane naye atawaumbua kweupe asubuhi.
 
Ipo mifano mingi mbali ya simu hata matamko Mh.Rais Rejea kesi ya Mbowe, Kesi za Mashehe...
Kwa ufupi muhimili mahakama upiga magoti kwa Rais Rejea mfumo wetu bajeti, hotuba za viongozi Mahakama kuomba na kumshukuru Mh. Rais....
 
Wengi tunakubaliana Rostam ni jambazi wa kiuchumi na mnyonyaji wa Watanganyika.
Ila hata asingesema Rostam kuhusu Mahakama za Tanganyika, isingebadilisha ukweli kwamba zimejaa ubabaishaji na maamuzi mengi yanatolewa kutokana na shinikizo aidha la rushwa, viongozi wa serikali na pengine ngono na urafiki.
 
Na endapo hatotekeleza maagizo ya majaji kati ya hayo mawili ni hatua gani nyingine zitachukuliwa na mahakama dhidi yake.
 
Ndio kusema full maelekezo.., au Rostam sawa na lile jamaa la kale lililosema serikali ipo mfukoni mwangu.
 
Kwani Rostamu kadanganya,tatizo lake ameamua kumwaga mchele kwenye kuku wengi!!,Kwa Majaji inawezekana akakosa ushahidi,Ila huku kwa Mahakimu ni shida tupu!!

nenda pale Kisutu,Kesi inamaliza miaka 2 Upelelezi haujakamilika,na hakimu anaona Sasa tu,
 
Ukweli umewauma na utawagharimu.
Walihendekez vyeo na teuzi sasa Rostam Kawalipua wazi wazi
 
Hata kesi ya Bandari wananchi tukishindwa tutajua Kuna Mtu Mkubwa kawapigia simu.

πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†Yaani hawajui wasimame wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…