Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Yani huyu muhindi anapambana na mahakama!?? Je mahakama ikiamua kumfikisha mahakamani kwa uchafuzi wa jina si amekwisha asubuhi na mapema
Inaweza pigwa tena simu kuwa aachwe[emoji23].
But huyu jamaaa ana reputation ya utafunaji fedha yes, lakini sijui kama ana histiria ya ujinga wa kuongea hivi hadharani.

Kwanini kaongea kipindi hiki, na sio kipindi cha JPM? Anayajua mangapi, matajiri wanajua mambo mengi sanaaa..
 
Mnamo tarehe 26 Juni, 2023 manyabiashara Bw. Rostam Azizi wakati akiongea na vyombo vya habari kuhusu masuala ya uwekezaji alinukuliwa akiituhumu aliyoiita Mahakama ya Kisutu kwa kutokuwa huru katika uendeshaji wa shughuli zake.

Kutokana na taarifa hiyo tunapenda kuhabarisha umma yafuatayo:

Hakuna Jaji anayehudumu katika Mahakama hiyo kama ilivyoripotiwa na mzungumzaji wa taarifa hiyo.

Mahakama ya Tanzania ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.

Uongozi wa Mahakama na au Chama Cha Majaji na Mahakimu haujawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha Maafisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika mahakama hiyo.

Kutokana na maelezo hayo Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania tunatoa kauli zifuatazo:
  1. Tumesikitishwa sana na kauli za Bw Rostam Aziz ambaye hatukutegemea aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho.
  2. Matamshi ya Bw Rostam Aziz yanaweza kuhatarisha uhusiano na ushirikiano katika mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi yetu.
  3. Tunaomba wananchi wenye nia njema na Mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na Imani na mfumo wa utoaji haki nchini.
Kwa taarifa hii, Chama Cha Majaji na Mahakimu Tanzania kinamtaka Bw. Rostam Azizi athibitishe kauli yake akibainisha jina la Jaji na lini alipewa maagizo na Kiongozi wa Serikali kutoa maamuzi kinyume na taratibu zilizopo.

Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.

Imetolewa na:
UONGOZI WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU TANZANIA (JMAT)
4 JULAI 2023


Pia soma: Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali

Wanajibaraguza tu,ukweli unafahamika mahakama na bunge na rubber stamp kwa mwenyekiti wa chama cha majambazi.

Hii nchi kile kinachoitwa mihimili kujitegemea ni maigizo matupu,kwahili naichukia sana hii nchi.
 
Pamoja kuwa aliteleza na kusema ukweli [emoji3][emoji3],ila aliwakosea sana, kwamba athibitishe ni kumuonea tu kwasababu hakuna mtu asijua hilo na hata kama wengi wetu ni mabush lawyers ila kuna maamuzi yao mengi yanaukakasi......kutetea dp world Rostam simuungi mkono ila Kisutu amewapiga na kitu kizito
Rostam yupo sawa kabisa
 
Athibitishe sasa
Athibitishe wapi? Mahakamani? Achemi mikwara nyie!
Sawa
Athibitishe
Athibitishe kwa nani? Athibitishe wapi? Eti aitishe vyombo vya habari! Nani asiyejua vyombo vya habari navyo vinapokea maagizo? Nchi hii kwa unafiki hamjambo. Je asipothibitisha mtamfanya nini? Mtampeleka Mahakamani, thubutu!

Siku hiyo bila shaka mtamjua Rostamu ni nani! Muulizeni Nape Nnauye aliyeitaka chama tawala, CCM, kujivua magamba. Magamba matatu hadi leo yako pale pale! Mojawapo alikuwa Rostamu na hivi sasa anasaini mikataba huku Rais, anayewateua majaji na mahakimu akishuhudia!! Shauri yenu!
 
Mnamo tarehe 26 Juni, 2023 manyabiashara Bw. Rostam Azizi wakati akiongea na vyombo vya habari kuhusu masuala ya uwekezaji alinukuliwa akiituhumu aliyoiita Mahakama ya Kisutu kwa kutokuwa huru katika uendeshaji wa shughuli zake.

Kutokana na taarifa hiyo tunapenda kuhabarisha umma yafuatayo:

Hakuna Jaji anayehudumu katika Mahakama hiyo kama ilivyoripotiwa na mzungumzaji wa taarifa hiyo.

Mahakama ya Tanzania ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.

Uongozi wa Mahakama na au Chama Cha Majaji na Mahakimu haujawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha Maafisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika mahakama hiyo.

Kutokana na maelezo hayo Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania tunatoa kauli zifuatazo:
  1. Tumesikitishwa sana na kauli za Bw Rostam Aziz ambaye hatukutegemea aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho.
  2. Matamshi ya Bw Rostam Aziz yanaweza kuhatarisha uhusiano na ushirikiano katika mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi yetu.
  3. Tunaomba wananchi wenye nia njema na Mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na Imani na mfumo wa utoaji haki nchini.
Kwa taarifa hii, Chama Cha Majaji na Mahakimu Tanzania kinamtaka Bw. Rostam Azizi athibitishe kauli yake akibainisha jina la Jaji na lini alipewa maagizo na Kiongozi wa Serikali kutoa maamuzi kinyume na taratibu zilizopo.

Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.

Imetolewa na:
UONGOZI WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU TANZANIA (JMAT)
4 JULAI 2023


Pia soma: Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali

1. Asipotaja kama wanavyotaka watamfanyaje?
2. Asipoomba radhi baada ya kutomtaja watamfanya nini?
Hao majaji na chama chao kwa hili tamko lao inaonyesha wanamuogopa, kumfanya chochote hawawezi kisheria la sivyo wangeanisha na hatua ambazo wanaweza kumchukulia kwa kunukuu vifungu vya sheria!
Tamko lao ni useless, Rostam ikibidi arudi tena kwenye media aseme hili tamko ni "professional rubbish" na siyo kuomba radhi!
 
Wanajitutumua hao. Namuunga mkono Rostam .... Huo ndiyo ukweli wenyewe. Hata Jaji Mkuu uteuzi wake ulifanywa na JPM kwa mtindo uleule....!!
Aliteuliwa naibu jaji mkuu,akasotoe hiko cheo karibu mwaka mzima ndo akawa jaji mkuu
 
Rostam sasa ana nguvu zaidi ya mtu yyt Tanzania....kama ameweza kumuweka Mwanasheria mkuu hapo alipo ....Anajua analosema.....! Nina hakika sio kwa bahati mbaya !! Alichofanya....hadi Dowans wanalipwa....tunajua yote ! Wenyewe wamemdekeza....ndio maana anayajua ya ndani sana!
Mkuu kamwekaje Mwanasheria Mkuu!?
 
Ile kauli aliitoa toka moyoni kabisa na hata akikanusha watu wamesha mwelewa na pia yeye atabaki na huo ukweli wake moyoni mwake.

Hizo zitabaki kuwa taratibu tu za kuomba radhi tu.
 
Back
Top Bottom