Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu

Rostam akathibitishe ukweli kwenye vyombo vinavyotumika kupindisha ukweli? Alichosema Rostam ni ukweli wa wazi.
Hiki chama cha Majaji na mahakimu ni chama cha KINAFIKI sana. Alichosema Rostam ndio ukweli

1. JPM aliposema Serikali ni mhimili uliochimbia chini zaidi , mbona hatukuwasikia hawa Majaji na Mahakimu
2. Kiongozi wao aliposema ' maamuzi yazingatie mihimili mingine' mbona hatukuwasikia
3. JPM alipotunga sheria za kudidimiza haki za watu mbona hatukuwasikia
4. Kesi za watu zina miaka 10 kama zile za Masheikh wakinyimwa haki za kusikiliza, mbona hatukuwasikia
5. JPM alipofanya upuuzi wa plea bargain ikiwa ni dhuluma mbona hatukuwasikia
6. Jaji Mugasha alipotoa angalizo la CJ kuongezewa muda , mbona hatujasikia msimamo wao

Hawa ni wanafiki tu wanaotaka kusikika wateuliwe katika bodi za mashirika na taasisi. Hawa hawana interest na nchi.

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Kuna yule jaji aliewahi sema kati ya vitu ambavyo hawezi sahau ni HUKUMU aliyoandika KUCHANWA CHANWA waziri mkuu mmoja wa hii (wako wengi)

HUKUMU yake iliitwa TAKATAKA na huyo waziri mkuu
Watu wenye pesa na wale wenye madaraka makubwa huwa wanazarau sana Mahakama zetu, na hii imesababishwa na Watumishi wenyewe wa Mahakama kwa kupenda sana kitu kidogo kutoka kwa matajiri hao!!
 
Mbona kasanda kirahisi sana?
Sasa Kama Mtu kapewa mlango wa kutokea( kuomba radhi) unategemea afanye nini!? Majaji walitakiwa wamwambie neno moja tu, nalo ni "Thibitisha" siyo kuambiwa au aombe radhi!!
 
Hiki chama cha Majaji na mahakimu ni chama cha KINAFIKI sana. Alichosema Rostam ndio ukweli

1. JPM aliposema Serikali ni mhimili uliochimbia chini zaidi , mbona hatukuwasikia hawa Majaji na Mahakimu
2. Kiongozi wao aliposema ' maamuzi yazingatie mihimili mingine' mbona hatukuwasikia
3. JPM alipotunga sheria za kudidimiza haki za watu mbona hatukuwasikia
4. Kesi za watu zina miaka 10 kama zile za Masheikh wakinyimwa haki za kusikiliza, mbona hatukuwasikia
5. JPM alipofanya upuuzi wa plea bargain ikiwa ni dhuluma mbona hatukuwasikia
6. Jaji Mugasha alipotoa angalizo la CJ kuongezewa muda , mbona hatujasikia msimamo wao

Hawa ni wanafiki tu wanaotaka kusikika wateuliwe katika bodi za mashirika na taasisi. Hawa hawana interest na nchi.

JokaKuu Pascal Mayalla

Uko sahihi kabisa. Siku za mwanzo za utawala wa Magufuli alisema kuna majaji wanakula rushwa, na majina yao anayo. Na hata wanaowalipia safari zao kwenda nje ya nchi kwa ajili ya likizo anawajua. Kwa kauli toka siku ile ndio ilikuwa mwanzo wa kuinyamazisha mahakama, na mahakama ikaanza kufanya kama atakavyo Magufuli, na sio sheria zitakavyo.

Huyo Rostam kaongea ukweli, kuanzia Rostam, mahakama pamoja na sisi wananchi, wote tunajua kaongea ukweli. Wanachokifanya mahakama ni kumtishia ili awasafishe, lakini ujumbe umefika kiusahihi kuwa mahakama haziko huru.
 
Tarehe Saba Nane
Ni siku ya Ukombozi.
Mahakama itoe haki, rudisheni mkataba huu Dubai.
 
Mnamo tarehe 26 Juni, 2023 manyabiashara Bw. Rostam Azizi wakati akiongea na vyombo vya habari kuhusu masuala ya uwekezaji alinukuliwa akiituhumu aliyoiita Mahakama ya Kisutu kwa kutokuwa huru katika uendeshaji wa shughuli zake.

Kutokana na taarifa hiyo tunapenda kuhabarisha umma yafuatayo:

Hakuna Jaji anayehudumu katika Mahakama hiyo kama ilivyoripotiwa na mzungumzaji wa taarifa hiyo.

Mahakama ya Tanzania ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.

Uongozi wa Mahakama na au Chama Cha Majaji na Mahakimu haujawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha Maafisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika mahakama hiyo.

Kutokana na maelezo hayo Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania tunatoa kauli zifuatazo:
  1. Tumesikitishwa sana na kauli za Bw Rostam Aziz ambaye hatukutegemea aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho.
  2. Matamshi ya Bw Rostam Aziz yanaweza kuhatarisha uhusiano na ushirikiano katika mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi yetu.
  3. Tunaomba wananchi wenye nia njema na Mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na Imani na mfumo wa utoaji haki nchini.
Kwa taarifa hii, Chama Cha Majaji na Mahakimu Tanzania kinamtaka Bw. Rostam Azizi athibitishe kauli yake akibainisha jina la Jaji na lini alipewa maagizo na Kiongozi wa Serikali kutoa maamuzi kinyume na taratibu zilizopo.

Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.

Imetolewa na:
UONGOZI WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU TANZANIA (JMAT)
4 JULAI 2023


Pia soma:
Kumbe walimshika pabaya huyu muajemi anayejidai ni mtanzania kuliko watanzania halisi. Mtu kama yeye ajishughulishe tu na biashara sio kupanda majukwaani kujidai kutetea wananchi.
Pamoja na faida ya uwepo wafanyabiashara, wengi ni wadhambi kwa kuwadhulumu wanyonge. Kwenye biblia yesu hakukataa uwezekano kuingia mbinguni wafanya biashara wakubwa ila akasema uwezekano wao kuona ufalme wa mbinguni ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.
 
Kumbe walimshika pabaya huyu muajemi anayejidai ni mtanzania kuliko watanzania halisi. Mtu kama yeye ajishughulishe tu na biashara sio kupanda majukwaani kujidai kutetea wananchi.
Pamoja na faida ya uwepo wafanyabiashara, wengi ni wadhambi kwa kuwadhulumu wanyonge. Kwenye biblia yesu hakukataa uwezekano kuingia mbinguni wafanya biashara wakubwa ila akasema uwezekano wao kuona ufalme wa mbinguni ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.
Ni mtanzania kama wewe....

Wewe huna utanzania wa kumzidi yeye.....

Baada ya bendera ya UNION JACK kushushwa ule usiku......kila aliyekuwa mkazi wa Tanganyika akawa raia....
 
Back
Top Bottom