Chama cha ujamaa na kujitegemea cuk(self reliance and socialist party SSP) na dhamira yake ya gawio la Rasilimali KWA kila mwananchi!je itawezekana!!?

Mbona mnarudi kule kule walipofeli kina Mwalimu
Kila mtu ana uwezo wa akili tofauti na mwenzake Mwalimu sio final say wa taifa hili amekwisha kufa hatuwezi kushindwa kufanya jambo kisa yeye lilimshinda.

Hata China alianza Chairman Mao na Pure Socialism ukamshinda akaja Architecture Deng akafanya Socialism with chinese characteristics akafaulu .

Kwa hiyo inabidi tujifunze mahali aliposhindwa Mwalimu na sisi kufanya tofauti na yeye ili tusije zama kwenye kisima alicho zama Mwalimu.
 
Haitokuwa ya virungu na unyonyaji tena kama ulivyoona KWA miaka Mingi hii!katiba mpya italinda watu na mali zao na serikali kitawekwa misingi mizuri kuhakikisha sekta binafsi haifi bali inalindwa na kustawi kuanzia chini Hadi juu!

TUSUBIRI!
 
Ni jambo zuri hizi mbinu wana zitumia sana China na Vietnam kwa sasa , ujamaa usio faa ni ule wa North Korea.
 
Sawa , lakini hatufahamu ni lini katiba mpya itapatikana ?
Mkuu

Usijali

KWA kuwa chama tawala kimeshatangaza Rasmi mchakato kuendelea maana yake huko jikoni wanapika vikiiva watavileta sebuleni tule!!

Nadhani ndani ya miaka sita hii ijayo katiba itapatikana!
 
Wazo zuri,

Juzi YOWERI MUSEVENI kaongea point muhimu tuifanyie KAZI nanukuu:

"Kuwa na NATURAL RESOURCES ni jambo moja, bt Kuzibadili national Resources Ili ziku TAJIRISHE ni jambo jingine"

Mfano.
1. Tuna ardhi ya kutosha Kwa kilimo bt kilimo chenye kuleta tija kinahitaji uwekezaji kwenye ELIMU na utafiti, Mitaji na vitendeakazi.

Kumbe unaweza kuwa na Mali na Bado ukawa maskini.

Tuna madini Nchi nzima Kweli, bt yatatutajirishaje kama Nchi ikiwa ELIMU na teknolojia ya kuyachimba hatuna,

Kuyabadili madini Ili yawe Vito na yauzwe kibiashara ni jambo jingine, je tuna ELIMU ya kutosha juu ya mambo hayo?

Hatujawekeza vya kutosha Badala yake uchimbaji unaenda kuharibu vyanzo vya maji Kwa kutiririsha zebaki.

3. Tuna Bahari na maziwa ukubwa wa kutosha, bt Umewatajirisha wavuvi na Nchi Kwa kiasi Gani?

Ili bahari itutajirishe tunahitaji Meli za kisasa za uvuvi, je tunaweza kuzitengeneza? Kama ni hapana, itabidi tupate pesa za kuwalipa watujengee au tushirikiane nao na tatizo huanzia hapo!!!

SOLUTION.

1. Raslimali Ili zitutajirishe tunahitaji kuwekeza kwenye ELIMU, ELIMU, ELIMU kama alivyosema Mzee wa mamvi.

Tofauti na hapo lazima tutakuwa vibarua ktk Kuzibadili raslimali zetu wenyewe kuwa matajiri.

ELIMU ni solution no moja. Na zingine zitafuata juu ya msingi wa ELIMU.

Tukiisoma vizuri RASIMU alosimamia Judge WARIOBA imeyaangalia mambo haya vizuri, Tuipambanie itatupa njia hata ya Kupata Vyama vitakavyoendana na Maono yetu kama Nchi.

Ameeeen.
 
Hii Ndio Tanzania ninayoiota usiku na mchana!!

Na iwe Hivyo!!
 
Elimu, Elimu , Elimu [ Elimu ni kama risasi kwenye bunduki , bunduki bila risasi inakuwa haina kazi ].
 
Sekta binafsi inaondoa tatizo la ukosefu wa ajira pia inachochea ongezeko la makusanyo ya kodi
Ni kosa kubwa kama serikali ikiiwekea ukungu wa mafanikio sekta binafsi, inabidi tupeleke vijana China tukajifunze namna wanavyo weza kuendesha haya mashirika na kuleta mafanikio makubwa China na duniani pasipo kuingilia na kuathiriana:- i, STATE OWNERSHIP/STATE OWNERSHIP ENTERPRISES
ii, PRIVATE OWNERSHIP
iii, COLLECTIVE OWNERSHIP
 
Mshafeli kabla hamjanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aaah wapi kama tu kuendesha maisha yao wameshindwa ndo wataweza
 
Sekta binafsi inaondoa tatizo la ukosefu wa ajira pia inachochea ongezeko la makusanyo ya kodi
Baada ya vijana wetu kupelekwa jkt na kutumika KWA Miaka kumi au pungufu ya Hiyo atakua amefanya KAZI sekta nyingi za uchumi na kuiva rasmi KWA kujiajiri mwenyewe!!

Vijana wetu wengi watakuwa na uwezo wa kujiajiri Sana kuliko hata kuajiriwa kama ilivyo Sasa!!

Tusubiri
 
Broo tafuta kazi nyingine ya kufanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aaah wapi kama tu kuendesha maisha yao wameshindwa ndo wataweza
Hilo ni tatizo tulilo nalo , lakini hatupaswi kukubali matatizo yetu yawe sugu kwetu bali inabidi tuya komeshe kwa sheria kali zenye adhabu kali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…