Chama cha wafugaji wa kuku wa kienyeji

Chama cha wafugaji wa kuku wa kienyeji

Fahari

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2014
Posts
1,044
Reaction score
698
Ndugu wana Jf amani iwe nanyi.kwa mda mrefu nimesoma maandiko kadha wa kadha juu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji humu Jf na nimehamasika.kwa kuanzia na kwa mazingira niliyopo nimeanza na kuku 50 wa kienyeji . wiki ijayo nitaongeza kuku 100 .sasa baada ya kusoma post tofauti tofauti juu ya mbinu anuai ningependa kushauri tuanzisheni chama cha wafugaji kuku wa kienyeji.hii itakuwa na faida zifuatazo kwa uchache ;(1) kubadilishana uzoefu na mbinu za ufugaji bora (2) kujenga mtandao wa masoko.karibuni kwa mjadala tuboreshe wazo hili.
 
Nashauri mngejuana ni wangapi mliopo tayari muwe na mikakati na malengo ya pamoja,
then mtengeneze kitu kama kikundi,
mtembeleane pia na kubadilishana uzoefu na baada ya hapo mjipanue zaidi na kutafuta masoko ya bidhaa zitokanazo na kuku iwe ndani na nje ya Tanzania,
kila la kheri
 
Nashauri mngejuana ni wangapi mliopo tayari muwe na mikakati na malengo ya pamoja,
then mtengeneze kitu kama kikundi,
mtembeleane pia na kubadilishana uzoefu na baada ya hapo mjipanue zaidi na kutafuta masoko ya bidhaa zitokanazo na kuku iwe ndani na nje ya Tanzania,
kila la kheri

Good idea
 
Nipo tayari nimeanza na kuku mmoja jike na jogoo nataka niongeze majike 10
Nisaidieni mbinu za ufugaji na sehemu ambayo naweza kupata kuku majike 10

Nipo tayari tukutane tuanzishe kikundi chetu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Siyo kuku wa kienyeji ni kuku wa asiri. wewe ukiitwa wa kienyeji utajisikiaje?
 
Ana ahueni kuliko wewe usiye nae hata mmoja,
kuku mmoja anauwezo wa kutoto vifaranga kumi na zaidi
ukitunza vizuri wanapona na unawaachisha kwa mama baada ya wiki moja,
kuku yule atapumzika kidogo,
baada ya mwezi ataamia tena,
baada ya siku 21 atatotoa tena,
je mtu huyu atakua na kuku wangapi?
Je wewe utakua na kuku wangapi?
Je atakua ni mfugaji ama mfujaji?
kuku mmoja na mtu anajiita mfugaji ?
 
Sina nia ya kuwakatisha tamaa Ila kwa jinsi ninavyowajua wabongo huwa wanakuwa excited wanaposkia kitu kwa Mara ya kwanza Ila linapokuja suala la utekelezaji utaona wanaanza kutoa visingizio mmoja baada ya mwingine mwisho idea inakufa ...ila kwa maoni yangu muunganiko km Huu ndyo inaoweza kutufanya tupate mafanikio mmakubwa tenna kwa pamoja,hebu Just imagine kwa mfano wafugaji 20 muamue kuungana na kuunganisha mitaji halafu mfungue kampuni itakayodili na kuuza na kusambaza kuku na mayai chini ya muungano Huu mtafaidika na mambo mengi kuliko km mgekuwa mmoja mmoja vitu km mikopo itakuwa rahisi kupata ,vile vile masoko pia mtaweza kukabiliana na changamoto mbalimbali kwa urahisi km vile kuku kuumwa mnaweza kuajili dokta ambaye kuku wote watakuwa chini ya uangalizi wake hii kwa kiasi kikubwa itapunguza risk ....umoja km Huu ndyo utatusaidia watanzania kupata maendeleo ya baraka bila kusubiri kusaidiwa na serikal
 
Wazo zuri sana ila naona utekelezaji hakuna maana toka hii mada imeletwa hakuna jipya
 
Mbona kimya jamani?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Ni wazo zuri utakutana na wafugaji wa kuku wa kienyeji tulioanza na kuku wawili leo nina zaidi ya mia moja........kuna uzi humu wa ufugaji kuku uliyeanza ufugaji utafute utapata uzoefu mkubwa........wewe ulieanza na kuku hamsini pambana na hao kuku kwa kuzingatia chanjo ili wakuwe maana ni kazi kubwa kwa mtu anayeanza kuanza na vifaranga .....
 
Back
Top Bottom