Chama na kipa Ally ndio walioiondosha Simba mashindanoni

... na kumuamini kijana kinda kulisababisha Simba kuingia hasara kubwa sana ya kutolewa mashindanoni na timu dhaifu ya Wydad,
Yaani Wydad imekuwa dhaifu ghafla? Si mlikuwa mnatuambia imeipiga Rivers united 6-0 kwa hiyo na Simba ijiandae na kipigo kikubwa? Baada ya kuona mnyama amekomaa kwa bingwa mtetezi na kumlazimisha ashinde kwa penati, mnaanza kusema eti Wydad ni timu dhaifu!
 
Reactions: Tui
Huwezi kuzuia hisia zetu kwa maneno rahisi TU hayo. Simba na Yanga ndio furaha zetu, Simba ameukimbia urithi kwa Mama ujue wa 10m kila goli. Sasa hivi watatamba Yanga TU kma nao watapita. Tutaficha wp nyuso zetu?
Sasa ulitaka wajilipue? Ndio matokeo hayo. Jifunze kupokea matokeo vyovyote vile yalivyo, vinginevyo utaugua sonona.
 
Reactions: Tui
Hiyo ni mihemko.. Yani sacko na kanoute watoke kwa sababu zipo.. 🤣 🤣 🤣
 
Malengo ya robatihno ilikuwa afikishe timu nusu final, je, malango aliyopewa yamefikiwa? Ana hoja dhaifu eti amelidhika na kiwango. Malengo yalikuwa kupandisha kiwango Cha timu au nusu final?
 
Sasa ulitaka wajilipue? Ndio matokeo hayo. Jifunze kupokea matokeo vyovyote vile yalivyo, vinginevyo utaugua sonona.
Tumeshayapokea hii ni postmortem TU. Hata jogoo akikatwa shingo anaweza kuendelea kuwika kwa muda.
 
Lawama atupiwee kocha na kina mgundaa. Simba ilistahiki kwenda next ¹ step Ila wakakwamishwa na chama na kipa
 
Yagangwe yajayo...
Sasa hivi ni Yanga Yanga Yanga TU kila Kona mpaka Ikulu, hii haikubaliki sisi robo fainali tunaambulia maruturutu TU, wenzetu robo finali 1 TU imezaa nusu finali,
 
Kilichoiua simbà ni kuwa na kikosi chembambà sana Cha wazee wanaocheza mechi zote, Binadamu sio mashine lazima wanapata uchovu na maumivu lakini wanaogopa kusema illi wasieleweke vibaya na kukosa namba. Saido, Kapombe, Shabalala,, onyango, Inonga, Baleke wamechezeshwa mechi zooooote kubwa na ndogo utafhani ni maroboti. Timu inaishia robo finali kila mwaka, haikui kama vile mtoto aliyebemendwa. Timu Ina wachezaji waliosajiliwa kwa 10% ambao hawachezi. Sifa walizopewa akina sawadogo, Qatara, okrah, okwah, sakho, Banda na phiri wakati wakati wanasajiliwa ni nyingi sana kiasi Cha kuachwa kusugua mbao ndefu uwanjani. Timu yetu imejaa wachezaji na viongozi wachawi wanaoamini ulozi kwenye kupata namba na kupata matokeo uwanjani. Timu Ina uwekezaji janjajanja, usajili janjajanja, transformation janjajanja na mipango ya janjajanja. Pesa walizokuwa wakichangishana kujenga uwanja alizosema Barbra ziko wapi na kwa nani. Zile 20b ziko kwenye account ipi, mchakato wa mabadiliko umekwamia wapi?
 
Huyu sio Uto mwenzangu Mkuu! Huyu lazima atakua dunduka, anaongea kwa uchungu mno.
Tatizo Utopolo ni makocha,wachambuzi na wataalamu wa utabiri.Wachezaji hatuwadai chochote Wamejitahidi na penalti zimeamua.Kuhusu Inonga lazima wewe Utopolo uweweseke na kukubali uwezo wake.Alikutungua tarehe 16 April.Inonga ametimiza wajibu wake ndio maana ni beki bora Nchini.
Eti Wydad wamepungua uwezo?
 
Nabi huyo huyo aliyetolewa Champions league na kuangukia Losers Cup au mwingine?Nabi huyo huyo anayeburuzwa na Robertinho kila timu zao zikikutana?Nabi huyo huyo aliyezungumza kipare baada ya Debi kwa kutajiwa jina la Robertinho?
 
Hao mnaowaita "wazee" waliwatungua 2 nunge.Mkapoteana kila mmoja akabaki kusema lake. Wanayefungwa na "wazee" wanakua nani?Viwete??
 
Ajabu waliyetolewa Simba na wanaoumia ni Gongowazi!
Simba huwasikii hata wakilalamika.
 
Wydad wabovu tu Mkuu.
 
Hizi ni kauli dhaifu sana kutoka kwa mtu asiyekuwa makini. Hata kupiga na kudaka penati kuna kwata (drill) yake wakati wa mazoezi uwanjani. Ni mtu wa hovyo kabisa anaefurahia kushindwa kwa njia ya penati. Kwani hiyo bahati isiwaangukie Simba iende kwa Wydad ambao wapigaji wao wote walifunga na kipa wao kudaka penati mbili? Unahalalisha uzembe utumike kuficha ukweli. Kupiga penati na kudaka penati kunahitaji ufundi pia sio bahati peke yake inayoamua penati. Yaani Simba kuishia robo finali mara 4 unasema ni kwa bahati mbaya tu, Simba tuna matatizo makubwa sana ambayo yanaigharimu timu. Kocha Robatihno analazimika kutumia wachezaji haohao kila mechi kwa dk 90 kwasababu walioko kwenye benchi ni malonyalonya tu, haoni ni nani anaweza kumuingiza kuchukua nafasi ya Onyango hata kama Onyango hafanyi vizuri, haoni mbadala wa Baleke, chama, saido, shabalala, kapombe, inonga, Kibu wala Mzamiru hata kama kama wawe wamepewa kadi ya njano, wameumia, wamechoka au wameamkaa vibaya siku hiyo. Lazima wanasimba wote wapaze sauti kuuanika ukweli huu kwa wafanya maamuzi., Simba ni mbovu sana hata hapo ilipofika ni kwahisani ya Vipers, Big Bullets, de agosto. Horoya na Wydad mbovu msimu huu. Uchochoro wa simba treet inawezekana umepatikana kwa bahatibahati tu au kwa njia ya mchongo fulani.
 
Lawama atupiwee kocha na kina mgundaa. Simba ilistahiki kwenda next ¹ step Ila wakakwamishwa na chama na kipa
Simba bado iko kwenye uendeshaji wa aina ileile ya zama za akina Gulamali za kuagiza bure bila ushuru makontena 5 ya tv na kuwapa wachezaji tv 25 tu kama zawadi ya kutwaa ubingwa.
 
Wewe mbona unaumia kuliko hata wanasimba?Au Haji Manara in disguise?
Mpira una matokeo matatu.Au upo deluded na hujui chochote kuhusu mpira?Una timu yako hayo mawazo peleka huko.
Ulikuwa wapi walipofungwa 2?Na walipotolewa Champions League?Kocha uchwara!
 
Msimu ukiisha Inonga ni Mwananchi.
 

Baki na Yanga yako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…