Wakati mpira wa Zambia vs Tanzania unaendelea nikasikia commentary anasema "Baada ya Micho kuita kikosi chake Cha CHAN wadau wengi wa soka Zambia walimkosoa kwa kuacha baadhi ya wachezaji, kitendo ambacho kilipelekea Micho awambie wadau wa soka Zambia waite kikosi chao wao ili ipigwe friendly match na kikosi chake, baada ya hiyo mechi Micho aliwaongeza wachezaji wa 5 kwenye kikosi chake kutoka kikosi hicho cha wadau wa soka"
Kwangu Mimi Kuna kitu Cha kujifunza hapa kwa nchi zetu zinazoendelea katika soka ni vizuri kocha kuwa karbu Sana na wadau wa soka na kuwasikiliza walau kidgo, maana wao ndo wanawajua wachezaji kuliko kocha, kocha ametoka Europe, America etc hawezi jua wachezaji wa bongo kuliko wabongo wenyewe
Rejea world cup 2018, Blanc alilaumiwa sana kwa kumucha Giroud lakn akabeba ubingwa na Giroud wake, kumbuka Giroud alizungukwa na Kante, Pogba, Griezmann, Mbappe, Matudi etc yani kifupi quality na experience ilikuwa nayo ya kutosha.. TZ ya leo ilikuwa na wachezaji non experience 9, hivi unategemea kupata matokeo hapo au ndo matokeo ya kimazabe zabe
Ni muda wa kubadilika kwa makocha wetu hasa wa kigeni, kuwasikiliza wadau hata kwa 1%, mtu anaweza akawa hajui ku.koachi lakn haimfanyi kutojua Metacha, Muhhamed Hussein, Mzamiru etc Ni wachezaji wazuri
NOTE: Hii nchi ishakuwa ya kusifu na kuabudu Sana, kesho utasikia wanahabari za michezo wakimtetea Etienne wakati Kama Zambia wangekuwa makin Leo hii ngoma ingekuwa 4+ leo