Changamoto ya vyoo Tanzania: Tatizo lipo vichwani na si mifukoni

Changamoto ya vyoo Tanzania: Tatizo lipo vichwani na si mifukoni

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Siikumbuki jina la clip.

Katika hiyo clip, Wazungu walikuwa wakijadili changamoto za Afrika, ambapo mmoja alionesha kushangazwa na tabia ya Mwafrika. Alisema kwamba Mwafrika anaweza akanunua simu ya gharama kubwa wakati choo hakina maji.

Siyo Watanzania wote, lakini wengi wanaweza wakaangukia kwenye mojawapo ya hizi changamoto:
1. Kutokujua jinsi ya kutumia choo kiusahihi

2. Kutokuwa na vyoo vinavyoikidhi vigezo vya kiafya na kiusalama

Mbaya ni kwamba hata watu
wanaochukuliwa kuwa wameelimika nao wanaweza wakaangukia kwenye mojawapo ya hayo makundi. Hii ni mifano niliyowahi kuishuhudia:

1. Choo cha nyumbani kisicho na mlango

Kwa wengine inaweza ikawa ni kawaida, lakini mimi nilishindwa kuelewa sababu ya hicho choo kutokuwa na mlango. Hela haikuwa tatizo kwake.
Nyumba yake ilikuwa kubwa na aliizungushia uzio wa tofali/ukuta.
Aliiwekea milango vyumba vyote vya ndani ikiwa ni pamoja na bafu na choo cha ndani.

Lakini choo cha nje, kiliachwa bila mlango. Kwa hiyo mtu aendapo huko, humlazimu kutembea "akiimba" ili kama kuna mtu atoe taarifa mapema.

2. Choo cha shule ya Msingi

Nilikiona miaka ya hivi karibuni wilayani Misungwi. Baada ya kupata fedha za Covid 19, hiyo shule ilizielekeza kwenye ujenzi wa vyoo vya wanafunzi. Vilikuwa vyoo vya shimo. Baada ya kupauliwa, kulijengwa ukuta mbele ya vyumba vyenye matundu ya vyoo ili kuwepo na mlango mmoja wa kuingilia kwenye korido ya vyoo. Lakini vyumba vyenye matundu ya vyoo havikuwekewa milango. Kwa hiyo mwanafunzi apitapo kwenda chooni wakati mwenzake yumo ndani, ana uchaguzi wa kumtazama au la. Hakuna kizuizi chochote cha kumfanya aliyepo chooni awe "faragha"

3. Choo cha shule ya Sekondari

Ilikuwa ni shule binafsi mkoani Mwanza. Na choo hicho klichangiwa na wanafunzi na walimu wao.

Nacho kilikuwa hakina milango, badala yake kulikuwa na ukuta mbele ya vyumba vya vyoo kumzuia aliye nje ya jengo la choo kuona kinachoendelea kwenye vyumba vya vyoo. Lakini ukishaingia kwenye korido la choo, utakwepa tu kumwona aliyemo kwenye chumba cha choo ikiwa utaamua kuangalia upande mwingine unapotembea kuelekea kwenye chumba cha choo ulichochagua ambacho nacho hakina mlango pia.

Lakini hiyo shule siyo kwamba haikuwa na uwezo wa kuweka milango, hapana.
Iweze kulipa mishahara ya walimu, iwe na makompyuta ya kutosha, iwe na magari, imudu kuwa na vifaa vya maabara, n.k., halafu ishindwe kuweka milango ya vyoo?

Ni kwamba milango haikuwa kipaumbele kwa wakati huo. Kama ingelikuwa haina uwezo, ingewakopa hata walimu wake.

Japo kulikuwa na mpango wa kuwekewa milango huko mbeleni, lakini haikuwa sahihi kutumika katika hali hiyo kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Hiyo inaonesha kwamba tatizo kubwa lipo kwenye mitazamo. Suluhisho likipatikana hapo na vyoo safi na salama kwa matumizi sahihi ya binadamu vitapatikana hata kwenye kaya masikini.
 
Siikukumbuki jina la clip.

Katika hiyo clip, Wazungu walikuwa wakijadili changamoto za Afrika, ambapo mmoja alionesha kushangazwa na tabia ya Mwafrika. Alisema kwamba Mwafrika anaweza akanunua simu ya gharama kubwa wakati choo hakina maji.

Siyo Watanzania wote, lakini wengi wanaweza wakaangukia kwenye mojawapo ya hizi changamoto:
1. Kutokujua jinsi ya kutumia choo kiusahihi

2. Kutokuwa na vyoo vinavyoikidhi vigezo vya kiafya na kiusalama

Mbaya ni kwamba hata watu
wanaochukuliwa kuwa wameelimika nao wanaweza wakaangukia kwenye mojawapo ya hayo makundi. Hii ni mifano niliyowahi kuishuhudia:

1. Choo cha nyumbani kisicho na mlango

Kwa wengine inaweza ikawa ni kawaida, lakini mimi nilishindwa kuelewa sababu ya hicho choo kutokuwa na mlango. Hela haikuwa tatizo kwake.
Nyumba yake ilikuwa kubwa na aliizungushia uzio wa tofali/ukuta.
Aliiwekea milango vyumba vyote vya ndani ikiwa ni pamoja na bafu na choo cha ndani.

Lakini choo cha nje, kiliachwa bila mlango. Kwa hiyo mtu aendapo huko, humlazimu kutembea "akiimba" ili kama kuna mtu atoe taarifa mapema.

2. Choo cha shule ya Msingi

Nilikiona miaka ya hivi karibuni wilayani Misungwi. Baada ya kupata fedha za Covid 19, hiyo shule ilizielekeza kwenye ujenzi wa vyoo vya wanafunzi. Vilikuwa vyoo vya shimo. Baada ya kupauliwa, kulijengwa ukuta mbele ya vyumba vyenye matundu ya vyoo ili kuwepo na mlango mmoja wa kuingilia kwenye korido ya vyoo. Lakini vyumba vyenye matundu ya vyoo havikuwekewa milango. Kwa hiyo mwanafunzi apitapo kwenda chooni wakati mwenzake yumo ndani, ana uchaguzi wa kumtazama au la. Hakuna kizuizi chochote cha kumfanya aliyepo chooni awe "faragha"

3. Choo cha shule ya Sekondari

Ilikuwa ni shule binafsi mkoani Mwanza. Na choo hicho klichangiwa na wanafunzi na walimu wao.

Nacho kilikuwa hakina milango, badala yake kulikuwa na ukuta mbele ya vyumba vya vyoo kumzuia aliye nje ya jengo la choo kuona kinachoendelea kwenye vyumba vya vyoo. Lakini ukishaingia kwenye korido la choo, utakwepa tu kumwona aliyemo kwenye chumba cha choo ikiwa utaamua kuangalia upande mwingine unapotembea kuelekea kwenye chumba cha choo ulichochagua ambacho nacho hakina mlango pia.

Lakini hiyo shule siyo kwamba haikuwa na uwezo wa kuweka milango, hapana.
Iweze kulipa mishahara ya walimu, iwe na makompyuta ya kutosha, iwe na magari, imudu kuwa na vifaa vya maabara, n.k., halafu ishindwe kuweka milango ya vyoo?

Ni kwamba milango haikuwa kipaumbele kwa wakati huo. Kama ingelikuwa haina uwezo, ingewakopa hata walimu wake.

Japo kulikuwa na mpango wa kuwekewa milango huko mbeleni, lakini haikuwa sahihi kutumika katika hali hiyo kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Hiyo inaonesha kwamba tatizo kubwa lipo kwenye mitazamo. Suluhisho likipatikana hapo na vyoo safi na salama kwa matumizi sahihi ya binadamu vitapatikana hata kwenye kaya masikini.
Hapana wazungu ni wabaguzi tu waende India, wajionee uchafu wa vyoo, Africa tuna umasikini na ubovu wa miundombinu, kuna sehemu hata maji salama ya kunywa hayapo ndo usemee maji ya vyooni,......mbona viongozi wanapewa misaada ya V8 badala ya kuwapa misaada ya kusambaza maji wazungu ni wanafiki, sasa itakua je ni sishike simu kisa hakuna maji chooni.
 
Hapana wazungu ni wabaguzi waende India wajionee uchafu wa vyoo.
Ni kweli ni wabaguzi, hilo liko wazi kabisa.

Lakini wewe unalionaje suala la vyoo Tanzania?
 
Ni kweli ni wanafunzi, hilo liko wazi.

Lakini wewe unalionaje suala la vyoo Tanzania?
We are poor country hata kutokomeza saphiris mosquito inao leta maleria imetushinda ndo usemee maji vyooni buana tuwe serious kdgo we ur living below internatinal poverty line
 
We are poor country hata kutokomeza saphiris mosquito inao leta maleria imetushinda ndo usemee maji vyooni buana tuwe serious kdgo we ur living below internatinal poverty line
Hata kama ni nchi masikini lakini si kwa kiasi cha kushindwa kuwa na vyoo salama.

Hata hivyo, ukiyaangilia Mav8 yanyaotumiwa na viongozi wa uma na wewe unakubali kuwa hii ni nchi masikini?
 
Hapana wazungu ni wabaguzi tu waende India, wajionee uchafu wa vyoo, Africa tuna umasikini na ubovu wa miundombinu, kuna sehemu hata maji salama ya kunywa hayapo ndo usemee maji ya vyooni,......mbona viongozi wanapewa misaada ya V8 badala ya kuwapa misaada ya kusambaza maji wazungu ni wanafiki, sasa itakua je ni sishike simu kisa hakuna maji chooni.
1. Kwa sababu India kuna vyoo vichafu basi sisi tusiambiwe kuwa vyoo vyetu ni vichafu? Tukiambiwa ukweli huo ni ubaguzi?
2. Kukosekana kwa maji salama ya kunywa imekuwa sababu ya kutokuwa na vyoo visafi?
3. Tunaonunua ma Vieiti ni sisi. Hao wazungu unaowasema ndio wanaofadhili ( au kutukopesha) miradi karibu yote ya maji nchini. Ni sisi ndio tunaamia kununua mavieiti badala ya magari nafuu kutoka hizo fedha za msaada.
4. Haukatazwi kushika simu unayoipenda. Siku hiyo I phone 15 Pro Max itakapo dumbukia kwenye choo chako cha shimo ndio utaelewa kwa nini haukufanya uamuzi wa busara.

Amandla...
 
Hapana wazungu ni wabaguzi tu waende India, wajionee uchafu wa vyoo, Africa tuna umasikini na ubovu wa miundombinu, kuna sehemu hata maji salama ya kunywa hayapo ndo usemee maji ya vyooni,......mbona viongozi wanapewa misaada ya V8 badala ya kuwapa misaada ya kusambaza maji wazungu ni wanafiki, sasa itakua je ni sishike simu kisa hakuna maji chooni.
Mleta mada kasema walikuwa wanaongelea changamoto za Africa, wangekuwa wanazungumzia India pia wangeweka wazi huo uchafu.
Tuna shida mahali. Uchafu umekuwa ni sehemu ya maisha na wala hatushtuki. Pita masokoni uone vyakula vinapouzwa, au ingia jikoni mgahawa unaokula chakula ujionee.
 
Mleta mada kasema walikuwa wanaongelea changamoto za Africa, wangekuwa wanazungumzia India pia wangeweka wazi huo uchafu.
Tuna shida mahali. Uchafu umekuwa ni sehemu ya maisha na wala hatushtuki. Pita masokoni uone vyakula vinapouzwa, au ingia jikoni mgahawa unaokula chakula ujionee.
Mkuu uchafu na umasikini are inseparable, wasijifanye kutojua hayo, wanatujadili kama nani, wakati wao ndo chanzo cha umasikini wetu.
 
Mkuu uchafu na umasikini are inseparable, wasijifanye kutojua hayo, wanatujadili kama nani, wakati wao ndo chanzo cha umasikini wetu.
1. Nafikiri ingekuwa vizuri zaidi ungesema ujinga na uchafu. Ujinga ndiyo chanzo kikuu cha maswaibu yote.

2. Wazungu wanaweza wakawa na sababu ya kuwajadili Waafrika kwa sababu wameshatoa michango yao ya hali na mali kwa lengo la kuboresha maisha yao lakini matokeo chanya ni kidogo sana. Kwa hiyo wanawaona Waafrika kama ni viumbe vigumu kuvisaidia.

3. Hakuna ulazima wowote wa Wazungu kuwasaidia Waafrika. Wazungu siyo baba wala mama wa Waafrika.
 
Hapana wazungu ni wabaguzi tu waende India, wajionee uchafu wa vyoo, Africa tuna umasikini na ubovu wa miundombinu, kuna sehemu hata maji salama ya kunywa hayapo ndo usemee maji ya vyooni,......mbona viongozi wanapewa misaada ya V8 badala ya kuwapa misaada ya kusambaza maji wazungu ni wanafiki, sasa itakua je ni sishike simu kisa hakuna maji chooni.
Naona unataka kuhalalisha uchafu wako kwa uchafu wa wahindi.
 
Zinaptikana pande zipi? Natarajia kwenda huko mwaka huu. Nataka nikifika huko nikajionee mwenyewe.
Zipo tu. Usiende kama mtalii na kuishia Darajani. Nenda sehemu wanazoishi wazanzibari wa kawaida. Bububu, Nungwi na hata Ng'ambo zipo nyumba zilizochoka. Sitashangaa kuzikuta hata Kizimkazi. Pemba nako zipo nyingi tu.

Amandla...
 
Back
Top Bottom