Dr. Zaganza
JF-Expert Member
- Jul 15, 2014
- 1,414
- 2,181
1. Wakati unasumbuka na tatizo la ndoa, kumbe robo tatu ya watoa ushauri hawajawahi kuishi na ndoa zaidi ya kudanda danda tu hapa na pale.Kwa kifupi hawajawahi saini mkataba mbele ya mashahidi na viongozi wa dini kwamba changamoto na furaha atazikabili. Mikataba alosaini ya kisela tu. Robo tatu ya wachangiaji utaona michango yao hailengi kutatua tatizo kumbe kiuhalisia umewapeleka kina kikubwa cha maji.umewapeleka madarasa ya mbeleni mnoo, zamani wazee ndo washauri kwa kuwa washafika mwisho kiuzoefu.Unakuwa unaulizia vifaa vya ujenzi kwenye duka la vipodozi.
2. Wakati unaleta mgogoro wako na ndugu zako unavyokukosesha amani, uzito wa undugu unaoelewa wewe kumbe na uelewa wa wachangiaji ni mbingu ni ardhi. Robo tatu yao utaskia mimi nishafuta namba zao. Wengine nishaacha kuhudhuria vikao vya familia. Umetaka kingine, unapewa kingine.Tuko na kizazi hakisumbui kichwa kutafuta suluhu, akikosa kazi ,anakuwa chawa. akizidiwa na tatizo au hasira anaua au kujiua, na kila mtu ana simu janja ya kukushauri.
MUHIMU: mfahamu unayemuomba ushauri ana uzoefu gani eneo hilo
2. Wakati unaleta mgogoro wako na ndugu zako unavyokukosesha amani, uzito wa undugu unaoelewa wewe kumbe na uelewa wa wachangiaji ni mbingu ni ardhi. Robo tatu yao utaskia mimi nishafuta namba zao. Wengine nishaacha kuhudhuria vikao vya familia. Umetaka kingine, unapewa kingine.Tuko na kizazi hakisumbui kichwa kutafuta suluhu, akikosa kazi ,anakuwa chawa. akizidiwa na tatizo au hasira anaua au kujiua, na kila mtu ana simu janja ya kukushauri.
MUHIMU: mfahamu unayemuomba ushauri ana uzoefu gani eneo hilo