Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.
Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.
Asante kwa elimu ya uwekezaji (investment). Tatizo linakuja, tukistaafu, ndio tunategemea mafao hayo tukajengee nyumba, je, huo uwekezaji tutauweza? Tunategemea hela hiyo tufanye mambo yote tuliyoshindwa kufanya tukiwa kwenye ajira; kujenga nyumba ya kuishi, kununua gari, shamba, nk, hapo hela ya uwekezaji itabaki? Sio kwamba hatutaki kuwekeza, la hasha, ila uhalisia wa maisha unatupeleka uelekeo mwingine!