Chanjo ya Covid ni uongo mtupu kwa viongozi wetu

Chanjo ya Covid ni uongo mtupu kwa viongozi wetu

Candela

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2021
Posts
817
Reaction score
2,180
Siku kadhaa nyuma tuliona viongozi wakichomwa chanjo hadharani.

Hivi karibuni nilimpeleka mtu kuchomwa chanjo baada ya kampuni anakofanya kazi kuamuru hivyo. Zoezi lilikuwa likifanyika hadharani na kila mtu akichomwa kwa zamu.

Jamaa yangu alilipa pesa na zamu yake ilipofika nesi hakumchoma sindano, aliiweka begani na akasukuma dawa kwenye pamba na rafiki yangu akapata cheti cha upimaji corona.

Nachojaribu kuwaza, kama mtu wa kawaida ameweza kufanya hivi, vipi kwa hawa viongozi?

Kama mtu wa afya anadiliki kutoa chanjo ya uongo je hii chanjo ina usalama gani na ulazima gani?
 
Back
Top Bottom