Hayo maeneo aliyochania hiyo quran me napajua ni opposite na stendi ya mabasi ya kilosa kuna bar inaitwa Shinyanga then pembeni kuna kijiwe cha bodaboda.
Hao bodaboda huwa wanaanza kuwatania walevi wa hiyo bar kwa kuwaambia kuwa hawawezi kufanya jambo fulani hata akilewa vipi. Sasa mlevi akiona hivyo anatafuta namna ya kudhihirisha atafanya nini ili aonekane jasiri.
Huyo afisa biashara ni mlevi mbwa alikuja kulewa hapo bar, baada ya kulewa ndo akakutana na bodaboda wakaanza kumwita mlokole gani wewe unalewa hovyo, akajibu dini yake ndo bora kuliko dini yoyote hata hao waislam si lolote kwake.
Bodaboda mmoja akampa juzuu amma akamwambia ichane hii kama unaweza. Huyo mlevi akaichukua akaanza kuichana huku wanamrekodi video. Ndio mwanzo wa hiyo issue.
So yawezekana ni kweli karogwa ndo maana anafanya vitu nje ya self control au pombe ndio imempelekea kupata ujasiri wa kuchana maneno ya Allah (s.w)
Mengine nawaachia wahusika!!
Sent using
Jamii Forums mobile app