Ni jana tu nilikuwa naangalia documentary ya Tupac na Biggie,kusema ukweli mpaka mwisho nilivyomaliza kuangalia hiyo documentary nimeconclude kutokana na evidence mbalimbali ambazo muandaaji alizi present kuwa muuaji wa tupac na biggie ni Suge knight pekee...Kwanza kisa hasa cha kuuwawa Tupac ni wazo lake la kuondoka death row records,ambao mpaka muda anaondoka alikuwa anawadai dola mil 10, na alitaka pia kuchukua nyimbo zake ambazo alikuwa tayari amekwisha zirekodi. Pili Hata kifo cha Tupac utaona Suge knight alikipanga, kwa kawaida 2pac huwa na mabodigadi wawili,lakini mmoja alipewa likizo fupi,na wa pili mpaka siku ya tukio aliambiwa aache bunduki yake, tatu kile kisa kilichotokea cha mtu kupigwa na kina tupac walipokuwa wanatoka kuangalia pambano la mike Tyson ni kuwa kuna watu waliambiwa waseme wamwambie tupac kuwa kuna jamaa alishiriki kukupora cheni yako,ambae huyo jamaa yupo kundi la creeps,ili ionekane kuuwawa kwa tupac ni retaliation ya creeps baada ya member wao kupigwa na kudhalilishwa na 2pac.Ukiangalia mtu aliekuwa nyuma ya yote haya ni Suge Knight.Ukija upande wa Big,sio kweli kwamba big alikuwa anamchukia tupac na walikuwa wana beef..huo ni uongo kabisa,na zilikuwa propaganda tu za C.I.A na FBI ambao walikuwa na ajenda zao. Muuaji wa Biggie ni Suge knight,ambae alimpa kazi hiyo Harry Billups a.k.a Amir Muhammad,huyu jamaa wamekuwa wote na Suge knight mtaa mmoja na kwenye documentary hiyo Lil Cease na aliekuwa bodigadi wa Big walimuona siku ya tukio..Ukiangalia documentary hiyo biggie hakuwa ana kinyongo na 2pac kwasababu alikuwa anamjua kichwa moto,na hata ile mara ya kwanza tupac alipigwa risasi 5,biggie alienda kumsalimia hospital na akaongea na baba yake tupac...Unaweza ipakua hii documentary kupitia utorrent ambapo muongozaji amejitahidi sana kuchimba mambo.Peace