Chanzo zcha ajali za mabasi ya abiria ni abiria wenyewe

Chanzo zcha ajali za mabasi ya abiria ni abiria wenyewe

BANDOKITITA

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2022
Posts
1,484
Reaction score
2,852
Ajali za barabarani zinaepukika ukiachilia mbali matatizo ya kibinadamu. Kuna sababu nyingi sana zimekuwa zikitajwa, lakini mimi niseme mbali na sababu zote hizo zinazotajwa chanzo kikubwa ni abiria wenyewe.

Sijui ni ukosefu wa elimu ya kwa Watanzania au kudharau au kuona muda wote Mungu yupo upande wao tu. Maana serikali kupitia jeshi la police wamekuwa wakitoa Elimu kwa abiria juu ya madhara ya mwendo kasi, lakini mara nyingi ukiskia ajali ya basi chanzo huwa ni speed.

Tatizo huanzia kwa ujuaji kwa baadhi ya abiria. Ktk safari ya basi huwa kuna mchanyiko wa abiria tofautitofauti. Mimi nataka kuongelea wale wanaotaka kujulikana km na wao wana miliki au wamewahi kumiliki magari. Mkiwa safarini ikatokea abiria mmoja au kadhaa kulalamikia speed ya dereva hawa wajuaji utaskia wanasema "hiyo speed ya kawaida sna labda hujawahi kuendesha gar" au watasema "labda wewe ni mara Yako ya kwanza kusafiri". Kwa ujumla huwa Wana maneno flani ya dharau.

Tatizo lingine ni uharaka wa baadhi ya abiria na kushindwa kukumbuka misemo ya wahenga isemayo "haraka haraka haina baraka au polepole ndiyo mwendo au heri kuchelewa kuliko kutokufika kabisa". Mkiwa safarini akitokea abiria anakemea speed utawaskia wale wanaojifanya wana haraka wanamjibu "kama unaoona speed ni kubwa shuka, wengine tunawahi mambo yetu au wengine tuna wagonjwa humu tuna wawahisha hospitali au watasema, 'wengine tunawahi msibani/tuanawahi biashara zetu".

Ili kudhihirisha wana haraka utaskia wanamwambia dreva, "dreva ongeza speed wengine tunachelewa mambo yetu, km umechoka pisha hapo tukusaidie". Abiria wa namna hii hufikiri yule/wale wanaokemea speed kubwa wao wamepanda km kujionesha au wanatalii tu. Dreva nae aksikia anapata backup ndiyo kwanza anaongeza speed.

Mwisho kuna wale abiria wanaoingiwa na uoga kwa kupigwa mkwara na dreva au kondakta pale abiria wanapoona speed Kali. Abiria wakikemea speed utaskia dreva anajibu "usinifundishe kazi km unaoona speed kubwa shuka". Kwa uoga mkubwa tena fikiria anakuambia ushuke sehemu yenyewe ni porini hakuna huduma yoyote au huenda ni usiku na eneo analokuambia kushuka hakuna hata nyumba, ili kuepuka hili abiria huamua kuufyata na kumuuacha dreva na konda wake wafanye watakavyo. Very sad.

Haya yote hupelekea dreva kujiona yeye ndiyo mmiliki wa gari na Mnyazimungu ni baba yake.

NB:
1) Pamoja na madhaifu haya yote ya abiria, dreva wote wa basi za abiria watambue wamebeba roho za watu, siyo mizigo hiyo au makreti ya soda/bia kwamba basi likianguka wananchi wengine wataburudika. Bali wajue basi likianguka na kuua au kuwaacha vilema familia ndiyo zinapata pigo na uchungu usiomithilika na Taifa hupoteza nguvu kazi ktk ulinzi na uzalishaji mali. Vipi km kwenye hayo mabasi wangekuwa wanabeba na ndugu zao mathalani wake/baba/mama zao wangekuwa wanajibu hovyo hovyo hivyo na kuwa na speed km hiyo?

2) Abiria tuache ushawishii na ujuaji kwa dreva unaoweza kumsababisha aongeze speed na hatimae kusababisha ajali.

3) Abiria tuitumie vyema elimu inayotolewa na jeshi la police na kuachana na tabia ya ouga.

Mimi binafsi kwa kutokuwa na tabia ya ouga na kuitumia vyema Elimu inayotolewa na jeshi la police vilishaniwezesha kuepusha mabalaa mengi ktk safari zangu. Nitolee mfano mmoja tu hapa, Kuna siku nilikuwa nasafiri tena safari ya masafa marefu, kumbe yule dreva alikuwa kalewa baadhi ya abiria tukamshitukia tukamwambia asimamishe gari ili tuletewe dreva mwingine, kichotokea ni baadhi ya abiria waliojiona wana haraka na kuanza kupaza sauti zao kuwa "anaetaka kusubiri dreva mwingine au anaogopa speed ashuke". Pasina uoga kati ya abiria wote tulijikuta tumebaki 2 tu tuliokerwa na majibu ya abiria wenzetu.

Tuliungana na yule mwenzangu kuwaelimisha abiria wenzetu juu ya kuendeshwa na dreva mlevi pasipo mafanikio.Na bahati nzuri yule mwenzangua alikuwa askari "kipenyo". Ikabaki mimi na mwenzangu bila kujuana kila mmoja akiwa anafanya awezalo ili kuepusha balaa. Kumbuka hapa huyo mlevi bado anaendeha kwa kubahatisha, mimi nilifikisha taarifa fasta kwa maafisa usalama waliokuwa kituo kinachofuata, kumbe mwenzangu nae keshawaliana na wenzake. Wakati huo dreva na kondakta wake walisha shitukia. Tulipofika tu kituo kilickokuwa kinafuata yule mlevi fasta alijichanganya na abiria akatokomea wakati tunashuka kujisaidia na ghafla aliingia dreva mwingine. Tukapanda na kuendelea na safari.

Abiria tuzitumie namba za makamanda wa police wa kila mkoa, na hata za makao makuu ya police inapoonekana hatua hazichukuliwi kwa wakati muafaka kuepusha ajali zisizo za lazima. Pia Kuna namba za Bure za maafisa wa Tarura kwa kila mkoa. Kizuri zaidi karibu kila basi la Abiria ndani kuna namba za kutolea taarifa kwa matukio ambayo siyo ya kawaida ktk safari, Mfano speed kubwa nk.

Nawatakia kila heri abiria wenzangu, tuchukue tahadhari ajali zinaua na kuziacha familia zetu kwenye huzuni mkubwa na pengo lisilo zibika.🙏🙏
 
Abiria wanaonewa tu. Wa kwanza kulaumiwa ni Askari Polisi na Mamlaka ya Usafiri inayoruhusu mabasi kuvuka vizuizi kabla ya muda stahiki.

Aidha, tunahitaji miundombinu automated ya kukagua magari kama Marekani inapeleka signal mtu kaendesha recklessly akamatwe.

Mwisho, tusipodhibiti rushwa kwa kutoa adhabu kali kwa wala rushwa na watoa rushwa tatizo litaendelea hata tufanyeje.
 
Naunga mkono hoja,,,unakuta abiria wengine wanadiriki kusema gari gani hili halikimbii. Magari yote yameshatupita. Binafsi nimetoka kusafiri juzi tu kutoka mikoa ya kusini na kuja dar es salaam. Mwendo ulikuwa wa kawaida tu abiria wakaanza kulalamika ooh dereva gani mwendo kama huu tutafika dar saa ngapi? Wakaanza kushindanisha magari oooh kuna gari moja ukipanda eti dereva anakuambia kabisa hili gari mwendo wake si wa kawaida kama dereva nitajitahidi kadri ya uwezo wangu lkn tumuachie Mungu.
Kweli kabisa asilimia 90 abiria ndo wanasababisha ajali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja,,,unakuta abiria wengine wanadiriki kusema gari gani hili halikimbii. Magari yote yameshatupita. Binafsi nimetoka kusafiri juzi tu kutoka mikoa ya kusini na kuja dar es salaam. Mwendo ulikuwa wa kawaida tu abiria wakaanza kulalamika ooh dereva gani mwendo kama huu tutafika dar saa ngapi? Wakaanza kushindanisha magari oooh kuna gari moja ukipanda eti dereva anakuambia kabisa hili gari mwendo wake si wa kawaida kama dereva nitajitahidi kadri ya uwezo wangu lkn tumuachie Mungu.
Kweli kabisa asilimia 90 abiria ndo wanasababisha ajali

Sent using Jamii Forums mobile app
Afadhali na wewe umeleta ushuhuda. Yani baadhi ya abiria wanatamani kifo wenywe
 
Mwisho wa siku bado ni uamuzi wa dereva kufuata sheria au lah. Kelele za chura hazimzuii ngo'mbe kunywa maji.
 
Madereva wa mabasi ndio chanzo kikubwa nimeshuhudia basi lina ovateki hata roli tatu dereva wa basi anaheshimu gari kubwa tu mbele yake
 
Tatizo ni speed za magari makubwa kama yangedhibitiwa kwa speed yote na kuondoa hizo speed za 50km/ h kila baada ya mda nafikiri wangeendesha vizuri tu
La pili ni sign post hakuna maana dereva imekuwa kama anaendesha kwa mazoea wakati mwingine anajisahau kwa speed analala nayo na analala kweli

Alama za hatari lazima ziwepo na hilo ni jukumu la wizara wana bajeti yao ila hawafanyi la kuzuia maafa

La 3 ni polisi waroho wanaosimamisha magari halafu unakuta dereva hashuki kwa sababu anamuona huyo ni pimbi tu mwenye njaa ya elftatu hivyo anamtuma konda akamalizane nae na njaa zake

Ila hajui wajibu wake kwa hiyo elfu 30 anaachia bus ambalo tairi zimeisha au haina break ila anaona wakafe watu huko ili yeye amalizie nyumba yake

La 4 dereva hafundishwi kukimbiza na msafiri bali ni upumbavu wake tu na kibri ya kuwa akikamatwa atatoa hela
 
Mi nnaona tusiwabanie sana kwenye spidi maana ukipunguza sana ndio wataona sheria haitekelezeki wanaamua kuvunja. Sio lazima kila sehemu kuwa 80 waongeze ifike hata 90 halafu kingora kianzie zaidi ya hapo.

Mfano mzuri ni kale kasauti kakingora kaongezwe kiwango cha kuanza kulia maana kakilia kila saa kanapoteza maana kanakuwa tu sehemu ya muziki sasa.

Kalie kuanzia labda 110km/hr hivi ili hata kila mtu ashtuke na akiangalia kweli iwe speed. Sio kanaanza hadi abiria unakereka tu af unajiuliza 'Spidi yenyewe ndogo hivi, kelele ni za nn sasa😒'

Ushauri kwa wenye magari/mabasi na serikali: ni ukaguzi wa magari, uzito yanayobeba, vipuri vihakikiwe ubora na service kwa wakati ili kuruhusu gari kutembelea sehemu kubwa ya spidi iliyoandikiwa kwenye kisahani chake.

Ushauri kwa abiria: Fungeni mikanda, timizeni wajibu wenu wa kujilinda halafu ya dereva muachie dereva.

Ushauri kwa dereva: Hakikisha uimara na service ya gari yako inakuruhusu kutembea spidi unayoitembea. Bila kusahau bara.......... anyway ya dereva nakuachia mwenyewe dereva. Kimsingi tu usitucheleweshe tunapoenda na usituwahishe huko 'afterlife'.
 
Madereva wa mabasi ndio chanzo kikubwa nimeshuhudia basi lina ovateki hata roli tatu dereva wa basi anaheshimu gari kubwa tu mbele yake
Wewe unakaribia kiasi kwenye kiini cha tatizo. Ajali nyingi zinatokana na overtaking za malori. Kwa nini overtaking? Kwa sababu maroli yanaenda mwendo wa Kobe. Je basi linaweza kuendana na mwendo wa malori. Hapana! Hivyo lazima ataovertake tu!
Malori yamekuwa mengi kupita kiasi, yanayoenda ni mengi na yanayorudi pia ni mengi. Kwa hiyo dreva wa basi anapambana ayapite yanayoenda na ayakwepe anayopishana nayo. Ni mpambano wa zaidi ya saa 17!

Suluhisho ni nini?
Suluhisho ni kutafuta usafiri mbadala wa abiria ili highway zibaki za malori na usafiri za kitalii na dharula ndogondogo Abiria watumie train za mwendokasi na ndege
 
Back
Top Bottom