Tetesi: Chato kuwa mkoa mpya na jina la mkoa kutangazwa soon na Chato kuwa makao makuu ya mkoa mpya

Ila Msata au Bagamoyo haikua Mkoa kipindi cha JK naamini hata Chato haitakua. JPM is smart hawezi sumbuka na vitu vidogo vidogo
 
Jana mlisema Mwigulu amezuiwa kufanya mkutano na wananchi
 
JPM alishasema kipindi chake hakuna maeneo mapya ya kiutawala
 
Mikoa na Wilaya nyingi sio chachu ya maendeleo hata Marekani kwa miaka nenda rudi wana majimbo 50 na wilaya 435 tu.

Kuongeza hayo siku zote ni kuwaongezea walipa kodi mzigo, hakuna manufaa yoyote wananchi wanayopata kutokana na wingi wa mikoa au wilaya.

Utasikia "Wajinga" wakisema eti ni kuwasogezea wananchi huduma karibu.!! Huduma gani? Wananchi hawana shida na DC au sijui RC bali wana shida na Maji, Afya, Elimu, Miundo mbinu na kuwezeshwa ktk kuboresha shughuli za kilimo. That's All, na hayo hayahitaji uongeze mikoa au wilaya eti ndio zipatikane.

Inayefikiria ktk kuongeza sijui mikoa/wilaya hana lolote ni akili ndogo tu.
 
Aiseeeeh....! yaani wanashindwa kuifanya ifakara kuwa mkoa ( mahenge, mwaya, ifakara, mtimbila) na inavigezo vyote, sijajua kwanini watu wa ifakara na mahenge hawatakiwi kupelekewa huduma jirani ila wana ng'ang'ana na sehemu nyingine tu

Toeni Rais na nyinyi
 
Hii nchi wangegawa tu kuwe na nchi nyingine nyingi kuna watu si wa kukaa nao nchi moja
 
hizi habari za tangu march bado hazija tekelezeka tu??? au ndio muda wowote... hata kama ni 2080
 
Sikubaliani na wewe, watumishi uongezeka, huduma za jamii kama maji, barabara, umeme,hospital/ vituo vya afya, polisi, Benki huongezeka, vyanzo vya mapato huongezeka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…