Tetesi: Chato kuwa mkoa mpya na jina la mkoa kutangazwa soon na Chato kuwa makao makuu ya mkoa mpya

Tetesi: Chato kuwa mkoa mpya na jina la mkoa kutangazwa soon na Chato kuwa makao makuu ya mkoa mpya

Siamini hii habari. JPM alisema katika kipindi chake hakutakuwa na mikoa mipya, wilaya mpya wala majimbo ya uchaguzi mapya. Kama hili linalosemwa ni kweli, sielewi JPM tutamweka kundi gani kuhusiana na yale anayoyatamka.
Wakati anaapa alisema atailinda katiba,anailinda??????wabongo bana,kama mtu anafanya kinyume na katiba atashindwa kufanya mkoa ambao ipo ndani ya mamlaka kisheria?
 
Wakati anaapa alisema atailinda katiba,anailinda??????wabongo bana,kama mtu anafanya kinyume na katiba atashindwa kufanya mkoa ambao ipo ndani ya mamlaka kisheria?
Kuna mengi ameenda kinyume. Kama na hili alilolisema mwenyewe akashindwa kulisimamia, sijui tutamwitaje!!!
 
Wewe unayeongelea Njombe, unafahamu mazingira yaliyokuwepo. Ukumbuke kuwa Njombe ilikuwa ni sehemu ya Iringa. Kutoka Njombe mpaka Iringa ni km 210, zaidi ya kutoka Mwanza mpaka Geita (~100km) na ni zaidi ya kutoka Mwanza mpaka Shinyanga (164km).

Mkoa wa Katavi, kutoka Sumbawanga mpaka Mpanda ni zaidi ya 200km. Lakini kutoka Chato mpaka Geita ni kama 100km tu. Huo ni umbali wa kawaida kwa wilaya nyingi kutoka makao makuu ya wilaya mpaka makao makuu ya mkoa.

Lakini ukumbuke pia kuwa Rais alisema katika kipindi chake hakutakuwa na uongezaji wa wilaya, mikoa au majimbo ya uchaguzi. Ndiyo maana siiamini hii taarifa.
Dunia ya sasa ni kama kijiji Kaka. Suala sio kuanzisha mikoa na mbwembwe zake na gharama zake za kisiasa. Suala ni kuimarisha MAWASILIANO. Miundombinu iwe mizuri. Tanzania hii ni jimbo moja la Marekani.
 
Mbona hamna shida Apo n Jambo LA kawaida Hilo ili kurahisisha utendaj kwa wananch
 
Hakuna Tatizo Kwa kuwa Hata Sumaye akiwa PM ndio Manyara ikazaliwa kutoka Arusha

Katavi ilizaliwa kutoka Rukwa wakati wa Pinda

Tunategemea Pia Mkoa wa Ruangwa kutokea Lindi

Tulikuwa tunamsakama Jakaya anapendelea kwao Bagamoyo sasa tumepata Mtu anaetufundisha maana ya kupendelea kwao
Isipokuwa Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Msuya, Warioba na Kawawa hawakuzalisha mikoa sehemu wanazotoka. Hongera ila chato mpaka inakuwa mkoa itakuwa imejengeka sana. Uwanja wa ndege wa kisasa, stadium, traffic lights, bank kubwa imeshafungua tawi na hata bandari inaweza kuanzishwa soon. Congratulations Chato people under Mbunge wenu
 
Ukubwa wa Arusha unafikia wa Morogoro? Kwanini mpaka Leo Moro haujagawanywa?

Unajua Idadi ya Wilaya za Mkoa Katavi
Arusha ile ilikuwa kubwa kuliko Morogoro.

Hata Tabora ni kubwa kuliko Morogoro

Mkoa wa Katavi una wilaya tatu na Halmashauri 5
 
wajenge hapo na chuo kikuu kama cha UDOM

'hii inaitwa Kwetu Raha'

usiyempenda kaingia
 
DYbLF83WkAAncC4.jpg:large
 
Yaan wameshindwa kuipa kaham kua mkoa maan ni wilaya ya mda mrefu. Ila powa tu maan yote ni Tanzania. Akimaliza aipe jiji kabisa ili tuwe na majiji mengi ili bdae iwe repblic of Chato kabisa.
 
Asante JPM ,kusogeza huduma ukanda huo, nashauri Mkoa mpya ujumuishe Ngara pia mapori akiba yapandiswe hadhi,kuna hali ya hewa nzuri sana,tufufue utalii mbali ya Rubondo park.
 
Back
Top Bottom