Uchaguzi 2020 CHAUMA tunakwenda vizuri. CCM mjiandae kuondoka 28/10/2020

Uchaguzi 2020 CHAUMA tunakwenda vizuri. CCM mjiandae kuondoka 28/10/2020

Msaliti wa Nchi alikuwa anahongwa mabilion na Mabeberu ili awatetee bungeni kutuibia rasmali zetu
Alihongwa shs ngapi bwashee?? Na wewe ulipata mgao nini???

Ila propaganda hii imechuja bwashee tafuta ingine 😂😂
 
Kama kuna watu walisikiza mahojiano ya itv ya mgombea urais kupitia chauma huyu ndio mgombea bora kupita wote kwani alielezea suluhisho la kuwatoa watanzania kwenye ujinga nacho ni lishe duni, ukiwa na lishe nzuri akili itafanya kazi, hautahongwa fulana, khanga au kitenge, hautadanganywa kwa pesa za mabeberu kwa kifupi seta yake imelenga kila mtanzania apate lishe bora ili kama mwanafunzi asome vizuri na wengine watumie vizuri akili yao kuzalisha
 
Msaliti wa Nchi alikuwa anahongwa mabilion na Mabeberu ili awatetee bungeni kutuibia rasmali zetu

Sio kweli, ebu muulize JIWE imekuwaje amewarusu Barrick waendelee kuchukua makinikia na kuchenjua nje ya nchi kitu ambacho alituaminisha kuwa ilikuwa ndio njia ya madini yetu kuibiwa? Sio hivyo tu, JIWE amewaruhusu kuendelea kutumia mabenki ya nchi za nje kuficha fedha zao kitu ambacho alituaminisha kuwa asingewaruhusu kabla ya washauri wake kubadili msimamo na kukubali matakwa ya Barrick!!
 
Tafadhali mkuu huu uzi ni maalum kwa ajili ya maboresho ya ushindi wa mgombea wa CHAUMA. Tunaomba mawazo yako

Ushindi wa Hashim Rungwe kuwa RAIS wa Jamhuri ya Muungano utakuwa wazi kama ataongeza sahani za ubwabwa kwenye mikutano na hii mikutano sasa iende mikoani ili huko nako wafaidi pilau!!
 
yatashughlikiwa lini kama mmewekewa pamba mdomoni msihoji.Vipi kwanini hamkohiji kabla kupiga kura kwamba yote yaletwe mezani kufanyiwa kazi kwa wakati mmoja mmgepoteza na nini zaidi ya kulinda heshima yenu? Tena kuna malalmiko kibao ya mgombea wa CCM yalitangulia kitambo?
Kesi ikishaletwa mezani huamuliwa. Huwezi kuacha kuamua eti mpk kesi nyingine iletwe.
 
Ushindi wa Hashim Rungwe kuwa RAIS wa Jamhuri ya Muungano utakuwa wazi kama ataongeza sahani za ubwabwa kwenye mikutano na hii mikutano sasa iende mikoani ili huko nako wafaidi pilau!!
Tumeweka wagombea udiwani kila kata na wagombea ubunge kila Jimbo. Kila mmoja anagawa ubwabwa. Hivyo tuna uhakika ubwabwa unaliwa kila kata na kila Jimbo nchini kote.
 
Back
Top Bottom