Chelsea FC inachezea sana hela kwa kuwafidia makocha inayowafukuza ovyo ovyo

Chelsea FC inachezea sana hela kwa kuwafidia makocha inayowafukuza ovyo ovyo

Machame Juu

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2013
Posts
1,514
Reaction score
3,363
1680760492675.png
Huyu kocha Graham Potter aliyefukuzwa majuzi amekuwa millionaire ghafla.

Tangu Chelsea inunuliwe kutoka kwa billionare Roman Abrahamovich chini ya mwaka imeshafukuza makocha watatu Frank Lampard, Thomas Tuchel na sasa Graham Potter kabla ya mikataba yao kuisha na kuwalipa fidia ya mamilion ya pounds.

Na kabla ya hapo walishawafukuza makocha wengine kabla ya mikataba yao kuisha Jose Mourinho, Antonio Konte na Mauricio Petechinno, Thomas Tuchel, Steve Holland, Guus Hiddink, Sarri na kuwalipa mamilion ya fidia.

Huyu Graham Potter wa karibuni kufukuzwa na Chelsea alipewa kitita cha paundi million 27 yeye na team yake ya ukocha alipokuwa anaifundisha Brighton ambayo aliiacha na inafanya vizuri. Pia akasaini mkataba wa miaka mitano ya paundi million 50 ambazo atafidiwa baada ya Chelsea kuvunja mkataba wake na kumfuza.

Miezi sita iliyopita Graham Potter hakuwa millionare lakini sasa hivi ni millionaire.

Chelsea inachezea sana pesa.
 
Ndo maana uku bongo makocha upewa mikataba ya miez sita sita, kazidi sana miaka 2 Ili ata wakikutimua sio mbaya mnaweza kufidiana[emoji4]
 
Umeongea mengi ukituaminisha timu imepata hasara. Ila umeacha kusema kuwa ni timu iliyofanikiwa zaidi kimakombe katika kipindi hicho.

Makombe Ulaya ni pesa na imejenga brand kubwa iliyoijengea hadhi ya kuwa na udhamini mnono tofauti na huko nyuma.
 
Back
Top Bottom